Kikao cha Bunge la Afrika Mashariki (EALA), jana kilivunjika kwa
mara ya pili baada ya Wabunge wa Tanzania, kutoka ndani ya ukumbi
wakipinga kanuni kuvunjwa juzi.
Baada ya wabunge wa Tanzania kutoka nje, Spika wa
Bunge hilo, Margareth Zziwa aliahirisha Bunge kwa dakika 15 ili kuweka
mambo sawa, lakini jitihada za kuwashawishi ziligonga mwamba na kuamua
kuahirisha Bunge hadi leo.
↧