Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, Sheikh
Ponda Issa Ponda amesema alichanganyikiwa kiasi cha kushindwa kujielewa
kwa muda baada ya kupigwa risasi.
Akizungumza
katika mahojiano maalumu na Mwananchi kwenye wodi binafsi ya Taasisi ya
Tiba ya Mifupa Muhimbili (Moi) alikolazwa jana, Sheikh Ponda alisema
kutokana na hali hiyo hakumbuki matukio yaliyofuata baada ya hapo.
↧