WINGU zito limetanda kwa askari wa Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ),
katika nchi za Sudani Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Wakati Watanzania wakiendelea kuomboleza vifo vya wanajeshi saba wa
jeshi hilo waliopoteza maisha katika Jimbo la Darfur, Sudani kwa
kushambuliwa na waasi, nchini DRC yamezuka mapigano makali baina ya
waasi na majeshi ya Serikali.
↧