Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) limewataka vijana waliomaliza katika jeshi hilo, kutambua kuwa walikula kiapo cha utii wakati wa kuhitimu mafunzo, hivyo suala la kuandamana ni kinyume na kiapo chao.
Vijana hao waliotumikia Jeshi la Kujenga Taifa Operesheni za nyuma na kumaliza mkataba wa miaka miwili, wameambiwa shinikizo lao la kulazimisha ajira kwa kuandamana ni kinyume cha sheria za nchi.
↧