WIZARA ya Katiba na Sheria imesema iko haja ya hukumu zinazotolewa katika Mahakama nchini, ziandikwe katika Kiswahili kuwezesha haki kutendeka na ionekane imetendeka.
Naibu Waziri, Ummy Mwalimu alisema hayo jana wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu, Amina Mwidau (CUF) aliyeshauri serikali kuangalia uwezekano wa hukumu kutolewa kwa lugha hiyo.
“Ni kweli kwamba kuna haja
↧