TAASISI ya Masheikh na Wanazuoni wa Kiislamu Tanzania, imepinga tamko la
maaskofu kuhusu kuzuia kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi na kusema hatua
hiyo ni sawa na kuingilia uhuru wa Bunge.
Kutokana na hali hiyo, wametaka maaskofu hao kupitia Jukwaa la Wakristo
Tanzania (TCF), kuwaacha wabunge ili waweze kujadili muswada huo kwa
uhuru bila kuwapo shinikizo katika suala hilo.
↧