Watu wasiojulikana wamelichoma moto na kuliteketeza Kanisa la Evangelical Assemblies of God wilaya ya Kakonko mkoani Kigoma na kuteketekeza kila kitu kilichokuwemo ndani ya kanisa hilo.
Mkuu wa Wilaya ya Kibondo, Venance Mwamoto amesema kuwa tukio hilo la mwanzoni mwa wiki hii, limeacha athari kubwa za mali na kwamba hakuna mtu yeyote ambaye amepata madhara kuhusiana na uharibifu.
↧