Kampuni ya bia ya Serengeti Breweries leo imetoa zawadi ya Limo Bajaji kwa Bw. Mfaume Hassan Lwembe (43) ambaye ni dereva taxi na mkazi wa Mbagala katika kampeni yake inayoendelea ya “Tutoke na Serengeti”. Hii imetangazwa leo katika droo inayofanyika kila wiki makao makuu ya SBL yaliyopo Chang’ombe jijini Dar es Salaam chini ya usimamizi wa PWC na bodi ya michezo ya bahati nasibu Tanzania.
↧