Baadhi ya wajumbe wa iliyokuwa tume ya mabadiliko ya katiba wameitaka
serikali ichapishe kwa wingi na kuzisambaza kwa wananchi nakala za
katiba pendekezwa, ili wananchi waisome, waitafakari na kuielewa kabla
ya kuipigia kura ya maoni huku wakitahadharisha uwezekano wa nchi kuwa
na katiba isiyokidhi matarajio na maslahi ya wananchi endapo wataipigia
kura kabla ya kuisoma na kuiielewa.
↧