CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimesema watendaji waliohusika kusababisha mgogoro katika Kiwanda cha Chai Mponde, kilichopo Jimbo la Bumbuli, Wilaya ya Lushoto, mkoani Tanga, wanapaswa kuwajibishwa pamoja na kuachia ngazi.
Â
Kauli hiyo imetolewa juzi na Katibu Mkuu wa chama hicho, Bw. Abdulrahman Kinana katika mkutano wa hadhara uliofanyika Kijiji cha Mponde, Jimbo la Bumbuli, wilayani humo.
↧