WAZIRI
MKUU Mizengo Pinda amesema Serikali haitataifisha shule, zahanati,
hospitali wala Vyuo Vikuu vinavyoendeshwa na taasisi za kidini na
amewahimiza wajenge zaidi na zaidi ili kuisaidia jamii kubwa ya
Watanzania.
Ametoa
wito huo wakati akizungumza na walimu, wazazi na wahitimu wa kidato cha
nne wa shule ya sekondari Magnificat iliyoko Sanya Juu, wilayani Siha
mkoani Kilimanjaro.
↧