Makubaliano baina ya Rais Jakaya Kikwete na viongozi wa Kituo
cha Demokrasia Tanzania (TCD), kutaka Bunge Maalumu lifikie ukomo Oktoba
4, mwaka huu yamezua sintofahamu mjini hapa huku uamuzi huo ukionekana
kuwachanganya viongozi wa Bunge hilo.
Kutwa nzima ya jana, viongozi wa Bunge Maalumu
walishinda kwenye vikao vya mashauriano huku wabunge wa CCM wakitarajiwa
kukutana jana usiku
↧