Mkazi wa Kimara Temboni, Felix Makundi (90) amekufa papo hapo baada ya kuteketea kwa moto wakati akiwa amelala.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Camillius Wambura alisema kuwa mzee huyo aliteketea juzi baada ya moto kuzuka katika nyumba yenye vyumba vitatu mali ya Benson Makundi na kumuunguza mzee huyo mwili mzima hadi kufa pamoja na kuteketeza mali zote zilizokuwamo ndani.
↧