Mbunge wa Mbeya mjini, Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ amelishutumu Jeshi
la Polisi mkoani humo kuwa ndiyo chanzo cha vurugu baada ya juzi
kutumia mabomu ya machozi kuwazuia wafuasi wa Chadema na waombolezaji
kuubeba mikononi mwili wa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Itiji,
Ezekiel King kwa lengo la kutembea nao kwa miguu kutoka Hospitali ya
Rufaa Mbeya hadi nyumbani kwake Itiji kuuzika.
↧