JESHI la Polisi katika Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, linawashikilia watu nane wanaotuhumiwa kuwa ni majambazi sugu. Wawili kati yao wanahusishwa na tukio la kuuawa kwa Sista Cresencia Kapuri (50) wa Kanisa Katoliki Jimbo Kuu la Dar es Salaam katika Parokia ya Makoka.
Kamanda wa Kanda Maalumu ya Polisi Dar es Salaam, Suleiman Kova alisema hayo alipozungumza na waandishi wa habari, jana.
↧