TUHUMA za ubabe
na usultani wa baadhi ya viongozi wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA), bado umeendelea kukitesa na kukipasua vipande chama hicho.
Hatua hiyo
imetokana na baadhi ya viongozi, akiwemo Mwenyekiti wake Taifa, Freeman
Mbowe, kupigwa ‘stop’ kuwania tena nafasi hiyo baada ya kubainika Katiba
ya CHADEMA imechakachuliwa ili kuondoa kipengele cha ukomo wa viongozi.
↧