Mpango wa kuligawa Shirika la Umeme (Tanesco) kuwa mashirika mawili umeiva, baada ya Serikali kupitisha Mkakati na Mwelekeo wa Sekta Ndogo ya Umeme (ESI).
Mpango huo utekelezaji wake unaanza Agosti mwaka huu, na lengo lake ni kuhakikisha uzalishaji wa umeme, unaongezeka kutoka megawati 1,583 zinazozalishwa kwa sasa hadi kufikia uzalishaji wa megawati 10,000 ifikapo mwaka 2025.
↧