Wajumbe wanawake wa Bunge Maalumu la Katiba na wageni wa jinsi
hiyo watakaovaa nguo fupi ‘vimini’ au nguo za kubana, hawataruhusiwa
kuingia ndani ya Ukumbi wa Bunge.
Hayo yamo katika mapendekezo ya rasimu ya kanuni
za uendeshaji wa Bunge hilo, zilizowasilishwa katika semina mahsusi ya
kupokea rasimu hizo, iliyowasilishwa na Mwenyekiti wa Kamati Maalumu,
Profesa Costa Mahalu.
↧