Shule
ya Msingi Mtambani iliyoko Kinondoni jijini Dar es Saalam, haina
samani hali inayosababisha wanafunzi kukaa chini, wakati walimu
wanalazimika kutandaza khanga wanazokalia chini ya miti.
“Shule hii ina upungufu wa madawati, nusu ya wanafunzi wanakaa chini,
hatuna ofisi za kutosha za walimu wale wasio na nafasi wanakaa chini
ya miti”, alisema Mwalimu Mkuu Emmanuel Munisi.
↧