MWALIMU wa Shule ya Msingi Mwang’osha Kata ya Nyamalongo wilayani Shinyanga, Christipian Mafuru (24) amefariki dunia baada ya kujinyonga kwa madai ya msongo wa mawazo.
Mafuru ambaye alitumia kamba ya katani na kujinyonga kwenye choo chake. Ameacha ujumbe uliosomeka ‘Msongo wa mawazo umenilazimu nifanye hivi, poleni sana walimu wenzangu, samahani wazazi wangu, kwa heri mwanangu Ray.’
↧