KIKOSI cha ulinzi cha Chama Cha Mapinduzi (CCM), wilayani Njombe,
mkoani Iringa kimewashushia kipigo wanachama wa Chama cha Demokrasia na
Maendeleo (CHADEMA) na kumvunja taya mwanachama, Ally Kalonga.
Licha ya kushusha kipigo hicho, Mkuu wa Polisi wilayani Njombe, Lucy
Mwakafirwa, amelaumiwa kuwakumbatia watuhumiwa makada wa CCM, huku
akiwasweka ndani wanachama wa CHADEMA.
↧