Baraza la Mitihani la Tanzania linapenda kuwakumbusha watu wote
wanaotaka kufanya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) na Maarifa (QT)
mwezi Novemba, 2014 kama Watahiniwa wa Kujitegemea kwamba kipindi cha
usajili kilichoanza rasmi tarehe 1 Januari, 2014 kwa ada ya Shilingi
50,000/=kwa wanaojisajili CSEE na Shilingi 30,000/= kwa wanaojisajili QT
kitaishia tarehe 28 Februari, 2014.
↧