Waziri Mkuu, Mizengo Pinda leo anakwenda Wilaya ya Kiteto,
Arusha kutafuta suluhu ya mapigano baina ya wakulima na wafugaji katika
Hifadhi ya Embroi Murtangosi yaliyosababisha vifo vya watu 10.
Mwandishi wa Habari wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Irene
Bwire alisema jana: “Ni kweli Waziri Mkuu atakwenda kutembelea wilayani
Kiteto ili kuongoza juhudi za kupata ufumbuzi wa tatizo hilo.”
↧