MBUNGE wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo (CHADEMA), amesema
matatizo yanayokikumba chama hicho kwa sasa yanatokana na kundi la watu
wachache wenye uchu wa madaraka, ambao pia wanatumiwa na Chama Cha
Mapinduzi (CCM).
Ndesamburo alisema kuwa wanaosababisha hali hiyo ni vijana ambao
hawana uchungu na CHADEMA, na hivyo kushauri uongozi uchukue hatua
stahiki ya kinidhamu kwa watu hao.
↧