BAADHI ya madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Itilima mkoani Simiyu wameomba itungwe sheria ndogo, kushinikiza wanaume kushiriki huduma ya kliniki kwa lazima.
Wametaka sheria itungwe ili atakayekaidi, achukuliwe hatua za kisheria na kupata adhabu kali. Walisema kuwepo kwa sheria hiyo, kutapunguza idadi ya wanawake wanaokwenda kliniki peke yao, na kusaidia wajawazito kupata huduma mbalimbali.
↧