Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Waziri Mkuu Atoa Siku Mbili Sekondari Ya Tunduru Ipelekewe Gari

$
0
0


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amempa siku mbili Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Tunduru mkoni Ruvuma, Gaspar Balyomi awe amepeleka gari katika shule ya Sekondari Tunduru kwa ajili ya kuwahudumia walimu na wanafunzi shuleni hapo.

Ametoa agizo hilo jana (Jumamosi, Januari 2, 2021) wakati alipokagua ukarabati wa Shule ya Sekondari Tunduru. Waziri Mkuu ametoa agizo hilo baada ya mbunge wa Tunduru Kusini, Daimu Mpakate kumueleza kuwa shule hiyo inakabiliwa na changamoto ya usafiri.

“Mkurungezi Jumatatu lete gari moja hapa likiwa limeandikwa Shule ya Sekondari Tunduru lije kutoa huduma kwa watoto na walimu wetu. Hii shule inawanafunzi zaidi ya 600 na walimu 28 lazima iwe na usafiri ambao hata mtoto akiugua afikishwe hospitali.”

Kuhusu ukarabati uliofanyika shuleni hapo, Waziri Mkuu amesema ameridhishwa na ametumia fursa hiyo kumpomgeza Mkuu wa Shule, Mwalimu Amini Limia pamoja na kamati ya ujenzi kwa kazi nzuri ya usimamizi waliyoifanya.

Waziri Mkuu amesema Serikali ya Awamu ya Tano ilipoingia madarakani ilianzisha mkakati wa kukarabati shule zote kongwe nchini ikiwemo ya Shule ya Sekondari ya Tunduru ambayo ukarabati wake umegharimu zaidi shilingi milioni 700. Mkoa wa Ruvuma umepewa jumla shilingi bilioni 3.7 kwa ajili ya ukarabati wa shule kongwe za sekondari ikiwemo ya Tunduru.

Pia, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwasihi wanafunzi wazingatie sheria, kanuni na taratibu zilizowekwa shuleni hapo ili waweze kuishi vizuri. “Someni hasa sasa hivi ni wakati wa likizo mpo hapa mnaendelea na masomo hatutarajii mpate daraja la nne wala sifuri. Kila mmoja ahakikishe anasoma na kupata daraja litakalomfikisha chuo kikuu.”

Waziri Mkuu amesema amefurahishwa na ufualu wa wananfunzi wa shule hiyo katika kipindi cha miaka mitatu mfululizo ambapo wanafunzi wote wa kidato cha sita walifaulu kwa zaidi ya asilimia 90. Amesema anatarajia katika matokeo ya mwaka huu watafaulu kwa asilimia 100.

Awali, Mkuu wa Shule hiyo, Mwalimu Limia alisema walipokea zaidi ya shilingi  milioni 792 kutoka Serikali kupitia mpango wa EP4R kwa ajili ya ukarabati wa majengo 15 ambayo yalikuwa yanakabiliwa na uchakavu mkubwa kutokana na kujengwa miaka 38 iliyopita.

Alisema ukarabati huo pia ulihusisha ujenzi wa majengo mengine mawili ambayo ni matundu 12 ya vyoo kipya cha wanafunzi na kibanda cha mlinzi. “Majengo yaliyokarabatiwa ni jengo la utawala, bwalo na jiko, madarasa vyumba 16, mabweni sita, jingo la zahanati, jingo la duka na stoo, vyoo majengo manne pamoja na kukarabati mfumo wa maji taka nje ya majengo.”

Shule ya Sekondari Tunduru ni miongoni mwa shule kongwe nchini ambayo ilianzishwa mwaka 1982 na ni ya wavulana kwa kidato cha tano na sita katika michepuo ya PCM, PCB, PGM, CBG, HGL, HGK NA HKL na ina jumla ya wanafunzi 682 na walimu 28.


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumatatu January 4

Mazungumzo ya Trump ya siri Georgia, kujaribu kubadilisha matokeo ya uchaguzi yanaswa

$
0
0


Kanda ya sauti imepatikana ambamo Rais Donald Trump wa Marekani anasikika akimshinikiza kamishna wa uchaguzi katika jimbo la Georgia kutafuta kura za kumsaidia Trump kushinda jimbo hilo katika uchaguzi wa rais wa Novemba iliyopita.

 Katika kanda hiyo Trump anasikika katika mazungumzo ya simu na kamishna huyo, Brad Raffensperger akimtaka waziwazi kutafuta kura karibu 12,000 na kurudia mahesabu ya kura ili Trump atangazwe mshindi. 

Kanda hiyo imewekwa hadharani na gazeti la Washington Post kuthibitisha hatua hiyo ya Rais Donald Trump, ambaye amepoteza kwa kura chache jimbo hilo la kusini mashariki mwa Marekani ambalo miaka ya nyuma lilikuwa ngome ya kutegemewa ya chama cha Republican chake rais Trump. 

Makamu wa rais mteule, Kamala Harris amesema kitendo hicho cha Rais Trump ni matumizi mabaya ya madaraka.

Nancy Pelosi achaguliwa tena kuwa Spika wa Baraza la Wawakilishi Marekani

$
0
0


Bunge la Marekani limewachagua viongozi wake wapya, wiki mbili na nusu tu kabla ya rais mteule Joe Biden kuchukua madaraka rasmi. 

Kwa mara nyingine Baraza la Wawakilishi limemchagua Nancy Pelosi kuwa Spika wake, japo kwa kura chache ikilinganishwa na muhula uliopita. 

Kwa uchaguzi huo Bi Pelosi mwenye umri wa miaka 80 anaendelea kushikilia mojawapo ya ofisi zenye mamlaka makubwa kabisa nchini Marekani.

 Hata wajumbe wa Baraza la Seneti walikula kiapo, lakini uongozi wa baraza hilo utajulikana bayana baada ya uchaguzi wa marudio wa majimbo mawili ya ubunge katika jimbo la Georgia ambao unafanyika kesho Jumanne. 

Matokeo ya uchaguzi huo ndio yataamua uwezo atakaokuwa nao rais mpya katika kupitisha sera zake.

Tozo Za Masoko Ya Samaki Ya Kimataifa Kuwasilishwa Wizarani

$
0
0


 Na. Edward Kondela
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki amewataka wakurugenzi wa halmashauri zenye masoko ya samaki ya kimataifa kuacha kupanga tozo za mazao ya uvuvi bila kuwasiliana na wizara hiyo ili kuondoa kero za tozo zinazowakumba wananchi wanaofanya biashara katika maeneo hayo.

Akizungumza jana (03.01.2021) mara baada ya kutembelea mnada wa mifugo uliyopo Kijiji cha Buzirayombo Kata ya Bukome na soko la samaki la kimataifa lililopo Kijiji cha Kasenda Kata ya Muganza, Wilaya ya Chato Mkoani Geita, Waziri Ndaki amesema wizara haitaki kusikia kero za wafanyabiashara kuhusu tozo zisizo rafiki katika masoko hayo likiwemo soko la samaki la kimataifa la Kata ya Kirumba lililopo Wilaya ya Ilemela jijini Mwanza.

“Kuhusiana na tozo niseme tu kwa wakurugenzi walio na masoko haya ya kimataifa kwa maana ya soko la Kirumba na Kasenda, sisi wizara hatutaki kusikia kelele katika haya masoko mnapopanga tozo zenu hakikisheni kwa masoko haya mawili tuwasiliane ili tupange tozo za kwenu na kwetu ambazo zitakuwa rafiki.” Amesema Mhe. Ndaki

Kwa upande wake Mbunge wa Jimbo la Chato Dkt. Medard Kalemani amemuomba Waziri Ndaki kupitia vikundi vya wavuvi vilivyosajiliwa, wizara ione namna ya kuwasaidia wavuvi mikopo yenye riba nafuu pamoja na kuwanunulia nyavu ili kuacha kujihusha na uvuvi usiofuata utaratibu.

Nao baadhi ya wavuvi na wananchi wanaofanya shughuli za kibiashara katika soko la samaki la kimataifa lililopo Kijiji cha Kasenda wamesema wanashirikiana na serikali kuhakikisha wanadhibiti uvuvi haramu.

Aidha, wameipongeza Wizara ya Mifugo na Uvuvi namna inavyofanya jitihada za kuhakikisha inaboresha mazingira ya wavuvi ili sekta ya uvuvi iweze kuwa na tija kwa wadau wa sekta hiyo na hatimaye waweze kunufaika kiuchumi.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki amekagua pia ujenzi wa machinjio ya kisasa yanayojengwa katika eneo la mnada wa mifugo Kijiji cha Buzirayombo Kata ya Bukome, Wilaya ya Chato Mkoani Geita.

Naibu Waziri Mabula Aelezea Namna Bilioni 2.175 Za Urasimishaji Zilivyoliwa

$
0
0


Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amebaini ubadhilifu wa zaidi ya Bilioni 2 uliofanywa na Wakufunzi wa Chuo Cha Ardhi Morogoro (ARIMO) na kumuelekeza Mkuu wa Chuo Huruma Lugala kumsimamisha  kazi mara moja Mkuu wa Utawala wa Chuo Michael Lori kwa  tuhuma ya kushirikiana na wakufunzi wawili wa chuo hicho waliofanya ubadhilifu katika zoezi la urasimishaji.

Dkt Mabula alitoa maelekezo hayo mwishoni mwa wiki mkoani Morogoro wakati akizungumza na watendaji wa sekta ya ardhi pamoja na uongozi wa mkoa wa Morogoro akiwa katika ziara yake ya siku moja kukagua utendaji kazi wa sekta ya ardhi pamoja na miradi inayotekelezwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).

Alisema, Wizara yake ilifikiri kushirikisha makampuni binafsi katika zoezi la urasimishaji ingerahisisha kazi ya kupima na kumilikisha wananchi maeneo yao lakini matokeo yake baadhi ya makampuni na watu wachache wametumia nafasi hiyo kufanya ulaghai wa kuchukua fedha za wananchi bila kukamilisha kazi ya urasimishaji.

Kwa mujibu wa Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Mkuu wa Utawala katika Chuo cha Ardhi Morogoro ameonekana kushirikiana na watuhumiwa kwa namna moja ama nyingine na uamuzi wa kumsimamisha ni kupisha uchunguzi wa tuhuma zinazomkabili.

Naye, Katibu Tawala Mkoa wa Morogoro Mhandisi Emanuel Kalobelo ameeleza namna anavyosikitishwa na baadhi ya watumishi wa sekta ya ardhi mkoani hapo wanavyofanya Kazi na kumtia aibu katakana na utendaji wao mbovu, na ameahidi kuwasimamia kikamilifu ili muleta ufanisi.

Awali Dkt Mabula alielezwa na Mkuu wa Chuo cha Ardhi Morogoro Huruma Lugala kuwa wakati uongozi wa chuo hicho ukifanya jitihada za kukiboresha chuo ikiwemo kudhibiti hujuma mbalimbali ilibainia baadhi ya Wakufunzi wake kujihusisha na kazi ya urasimishaji katika maeneo mbalimbali kwa kutumia jina la chuo kujipatia fedha.

Alisema, chuo chake baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa wananchi na kubainia udanganyifu kwa baadhi ya watumishi wake kiliamua kuwasimamisha Wakufunzi wawili kupisha uchunguzi na kuwataja watumishi hao kuwa ni Adolf Milungala anayetuhumiwa kujipatia shilingi Bilioni 1.9 na Hamis Abdalah Kindemile milioni 275 fedha zilizokuwa malipo ya urasimishaji katika mitaa 43 Morogoro.

Waziri wa Ujenzi Aiagiza Tanroads Kupunguza Gharama Za Mradi

$
0
0


 Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Leonard Chamuriho, ameiagiza Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), Mkoa wa Mara , kuhakikisha wanapunguza  gharama za miradi, hususani wanapofanya upembuzi yakinifu.


Alitoa agizo hilo akiwa katika ziara wilayani Bunda, akikagua ujenzi wa barabara ya Nyamuswa-Bunda-Kisorya yenye urefu wa kilometa 121.9, pamoja na kipande cha barabara ya lami kutoka Bulamba-Kisorya (kilometa 51).


Akiwa katika ukaguzi huo, Waziri Chamuriho alisema barabara ya Nansio, ambayo inaanzia Nyamuswa-Bunda hadi Kisorya ni muhimu kwa  wananchi wa Wilaya ya bunda, kwamba itafungua fursa nyingi ikiwamo usafirishaji wa mazao.


Naye Mkuu wa Wilaya ya Bunda, Lydia Bupilipili alimpongeza  mkandarasi  anayesimamia ujenzi wa barabara hiyo na TANROADS kwa kazi nzuri walioifanya katika ujenzi wa barabara hiyo.


Bupilipili alisema: “Kasi ya ujenzi ilikuwa kubwa katika ujenzi wa barabara hii na imetoa  ajira kwa vijana wazawa wa  Wilaya ya Bunda na Mkoa wa Mara. Niwapongeze na niwapongeze TANROADS kwa kazi nzuri wanayoifanya katika Wilaya hii ya Bunda mjini”.


Kwa upende wake Meneja wa TANROADS, Mkoa wa Mara, Mhandisi Mlima Ngaile, akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo alisema mkataba ulisainiwa na makubaliano yalikuwa ya miaka miwili, ila kutokana na kasi ya mkandarasi aliahidi kumaliza kazi hiyo kabla ya muda uliopangwa.


“Thamani ya mkataba Sh.bilioni 46.5 na unasimamiwa na  kampuni ya wahandisi ya ushauri kutokea TANROADS na hadi kufikia sasa mkandarasi ameshaanza kazi mbalimbali ikiwamo kujenga nyumba ya msimamizi ambayo imefikia  asilimia 50 na amesafisha barabara kutoka Bunda kwenda Bulamba," alisema mhandisi Ngaile.


Waziri Lukuvi Awataka Wamiliki Wa Ardhi Kujenga Kwa Kufuata Sheria

$
0
0


Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi amewataka wamiliki wa ardhi wanaotaka kujenga kuhakikisha wanafuata sheria na  taratibu zote wakati wa kufanya ujenzi.

Waziri Lukuvi alisema hayo mwishoni mwa wiki hii katika ofisi yake ya ardhi ya mkoani Dar es salaam na Pwani. Alisema sheria inamtaka mmiliki wa ardhi anayetaka kufanya ujenzi kupata kibali kutoka  halmashauri za miji, manispaa na majiji na kuongeza kuwa sheria hiyo inakataza kufanya ujenzi bila kibali kutoka mamlaka husika.

”Naelekeza watendaji wote wawe wa ardhi au mipango miji kuhakikisha sheria zinafuatwa kwa kudhibiti ujenzi holela na sheria inakataza kabisa kujenga bila kupata kibali kutoka katika mamlaka husika” alisema Lukuvi.

Kwa mujibu wa Lukuvi, zoezi la urasimishaji linaloendelea sasa maeneo mbalimbali ni kwa majengo yaliyojengwa tu na kusisitiza kuwa zoezi la urasimishaji isiwe sehemu endelevu ya kuvunja sheria na kubainisha kuwa angetaka kuona maeneo yote ya miji hasa Dodoma yanajengwa kwa kupatiwa kibali.

Aliwataka wataalamu wote hasa waliopo halmashauri  katika yale  maeneo yaliyotangazwa kimji kwa mujibu wa sheria wananchi wake waelimishwe  kujenga katika viwanja vilivyopangwa na kupimwa na wawe wamepatiwa vibali na mamlaka za halmashauri husika.

” Hatua zichukuliwe kuzuia jambo hili tunataka miji endelevu ambayo wananchi wanaishi na kujenga kwa mujibu wa sheria” alisema Lukuvi.


Naibu Waziri wa Afya Dkt Mollel Ataka Wataalam Wa Tehama Kutengeneza Mfumo Wa Ufutaliaji Wa Dawa Hospitalini

$
0
0


Na Englibert Kayombo – WAMJW, SONGWE
Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Godwin Mollel amewataka wataalam wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano katika hospitali kutengeneza mfumo wa ufutaliji wa dawa hospitalini ili kuwa na kanzidata ya matumizi sahihi ya dawa.

Dkt. Mollel ametoa agizo hilo alipokutana na Wataalam kutoka Kurugenzi ya Afya, Ustawi wa Jamii na Lishe kutoka Ofisi a ya Rais Tawala za Mikoa na Serkiali za Mitaa (TAMISEMI) na timu ya uongozi wa afya ya Mkoa wa Songwe kwenye kikao kazi kilichofanyika katika ofisi za Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi.

“Kila dawa inayokuja mtutengenezee mfumo ambao tunaona dawa kutoka taifa, unaiona inaingia mkoani, Hospitali ya Wilaya, vituo vya vyote na tuone ni aina gani ya dawa imeingia” Amesema Dkt. Mollel

Dkt. Mollel amesema inawezekana kutengenezwa mfumo rahisi kwa kutumia programu ya ‘Excel’ kwa wataalam hao wakawa na taarifa sahihi ya dawa inayoonyesha matumizi ya dawa toka walivyopokea.

Amesema mfumo huo utawasaidia kutambua mgawanyo wa dawa katika vituo vya kutolea huduma za afya pamoja na kuwasaidia viongozi kuwa na taarifa sahihi wakati wanashughulikia malalamiko ya uhaba wa dawa katika vituo vya kutolea huduma za afya hivyo kuwasaidia katika kufanya maamuzi.

Aidha Dkt. Mollel amewataka wataalam wa afya nchini kuboresha taarifa za takwimu ziwe za ukweli ili kuwasaidia viongozi kufanya maamuzi sahihi kulingana na mahitaji.

“Mnafeli kwenye kufanya maamuzi na wakati mwingine tunaona hamjafanya maamuzi ya busara kumbe mmejifelisha kwa sababu mnashindwa kupata takwimu halisi za magonjwa, idadi ya wagonjwa na mahitaji ya dawa” Amefafanua Dkt. Mollel

Amesema kushindwa kwa wataalam hao kuwa na takwimu sahihi zinasababisha kuwa na mahitaji yasiyo na uhalisia upatikanaji wa dawa.

“Unapoamua kuagiza dawa ni lazima uwe na takwimu sahihi kuanzia taarifa za wagonjwa wa nje hadi wagonjwa waliolazwa, tukiweza kuboresha takwimu zikawa vizuri, tutaweza kuagiza dawa kwa busara na kuhakikisha rasilimali ambazo serikali inatuletea zinatumika kwa busara” amesema Dkt. Mollel

Waziri Mkuu Aagiza Madiwani Watatu Mbingavijijini Wakamatwe

$
0
0


WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemuagiza Kamanda wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) mkoa wa Ruvuma, Hamza Mwenda ahakikishe anawakamata madiwani na watendaji wa Halmashauri ya Mbinga Vijijini ili wajibu tuhuma za rushwa zinazowakabili.

Madiwani wa kata za Mkumbi (Bruno Kapinga), kata ya Lukalasi (Bosco Ndimbo) na wa kata ya Linda (Haule) wanadaiwa kuchukua fedha kutoka kwa watendaji wa AMCOS kwa ajili ya kwenda kushawishi kuhamishwa kwa eneo la ujenzi wa makao makuu ya halmashauri hiyo.

Ametoa agizo hilo leo (Jumatatu, Januari 4, 2021) baada ya kuzindua jengo la utawala la Halmashauri ya Mji wa Mbinga akiwa wilayani Mbinga mkoa wa Ruvuma. Waziri Mkuu amemuagiza Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Christine Mndeme asimamie ujenzi wa halmashauri hiyo unaoendelea katika eneo la Kigonsera.

Hatua hiyo imekuja baada ya kuwepo kwa mvutano wa Madiwani wa Halmashauri ya Mbinga Vijijini ambao baadhi yao hawataki makao makuu ya halmashauri hiyo yajengwe Kigonsera na kuamua kuendesha mchakato wa kushawishi wengine wagomee mradi huo jambo ambalo linakwamisha maendeleo kwa sababu tayari mradi huo umeshaanza kujengwa.

Mvutano huo unaongozwa na Madiwani wa Kata tatu za Mkumbi, Lukalasi na Linda ambao wanataka makao makuu yajengwe kwenye kata ya Mkumbi katika eneo ambalo litailazimu Serikali ilipe fidia ya zaidi ya shilingi milioni 400 huku kukiwa na eneo la bure la ekari 150 ambalo ndiko yanakojengwa makao makuu.

“Hatuwezi kukubali huko mnakotaka nyie ni lazima tulipe fidia ya zaidi ya shilingi milioni 400 na kuna eneo la bure ekari zaidi ya 150, hii haikubaliki hatuwezi kufanya mambo ya siasa kwenye fedha za wananchi haiwezekani. Mmeamua kila AMCOS ichange shilingi 600,000 mpate milioni tatu mfanye kampeni ya kutaka halmashauri ijengwe kweni hiyo ni rushwa.”

Waziri Mkuu ameongeza kuwa “Kwa kuwa zile ni fedha za wakulima, Kamanda wa TAKUKURU kawakamate watendaji wa AMCOS hizo wahojiwe kwa nini walitumia fedha za kuwapa Madiwani wakahonge ni lazima wahojiwe waeleze ni nani aliyetoa maagizo ya kutoa shilingi milioni tatu. Hatuwezi kutumia fedha za wananchi kwa ajili ya kuhonga watu lazima fedha hizo za wakulima zirudishwe ni mali ya wakulima.”

Mapema, Waziri Mkuu alizindua jengo la utawala la Halmashauri ya Mji wa Mbinga na kukagua ujenzi wa nyumba nane za watumishi wa halmashauri hiyo na amesema kwamba ameridhishwa na utekelezaji wa miradi hiyo iliyogharimu shilingi bilioni 3.7

Pia, Waziri Mkuu alitumia fursa hiyo kumpongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Mbinga, Grace Quintine kwa usimamizi mzuri wa miradi hiyo ambayo imejengwa kwa viwango bora na majengo hayo yanalingana na kiwango cha fedha kilichotolewa.

“Tulimletea shilingi milioni 350 hapa kwa ajili ya ujenzi wa nyumba saba za watumishi na ametumia milioni 321 na tulimletea shilingi milioni 300 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba ya Mkurugenzi lakini ametumia shilingi milioni 251 na hakuna ubabaishaji majengo yote yamejengwa kwa viwango bora. Nampongeza sana Mkurugenzi huyu amefanya vizuri sana endelea kujenga miradi mingine ikiwemo na ya vyumba vya madarasa.”

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Mbinga, Grace Quintine amesema halmashauri yao katika mwaka wa fedha 2019/2020 ilipekea shilingi milioni 650 kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za watumishi zikiwemo saba za Wakuu wa Idara na moja ya Mkurugenzi.

Amesema gharama za ujenzi wa nyumba saba za Wakuu wa Idara ni shilingi milioni 321.771 ambapo kila nyumba iligharimu shilingi milioni 45.967 kati ya shilingi milioni 50 zilizoidhinishwa za kupokelewa ambapo kila nyumba ilikadiriwa kutumia shilingi milioni 350 kwa nyumba zote.

“Ujenzi wa nyumba ya ghorofa moja ya Mkurugenzi wa Mji umegharimu shilingi milioni 251.780 kuhu makadirio yakiwa ni shilingi milioni 300. Lengo la miradi hii ni kuboresha mazingira ya makazi ya watumishi wa halmashauri ikiwa ni pamoja na kupunguza kilipa posho za nyumba kwa kila mwezi.”

Amesema shilingi milioni 28.228 zilizobaki katika ujenzi wa nyumba za Wakuu wa Idara zitatumika kujenga mnara wa tenki la maji na uwekaji wa tenki moja la maji kwa kila nyumba na kuanza ujenzi wa uzio kuzunguka nyumba zote saba.

Mkurugenzi huyo amesema mbali na utekelezaji wa ujenzi wa miradi hiyo ya nyumba za makazi, pia Serikali ilitoa shilingi bilioni 3.1 kwa ajili ya ujenzi wa jengo la utawala la halmashauri hiyo ambalo lilijengwa na kampuni ya SUMA-JKT Kanda ya Mtwara.

Amesema ujenzi wa jengo hilo la utawala lenye jumla ya vyumba 52 vikiwemo vyumba vya ofisi za watumishi na Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji, ukumbi mkubwa wa mikutano na ukumbi mdogo kwa ajili ya vikao vya Wakuu wa Idara na Vitengo. “Ujenzi umekalika na lilianza kutumika Januari 2020. Naishukuru Serikali kwa utekelezaji wa miradi hii.”


 (mwisho)
IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU

Taarifa Ya Matumizi Ya Tiketi Mtandao Kwenye Mabasi

Dr. Mollel Asisitiza Uwajibikaji, Utoaji Huduma Za Afya

$
0
0


Nteghenjwa Hosseah, Songwe
Naibu Waziri wa Afya Ustawi wa Jamii na Lishe Mhe. Dr. Godwin Mollel amewataka watoa huduma za Afya kuwajibika ipasavyo katika kuwahudumia wananchi.

Dr. Mollel ametoa kauli hiyo wakati akiongea na wataalamu watendaji wa Afya wa Mkoa wa Songwe katika ukumbi wa Halmashauri ya Songwe tarehe 03/01/2021.

Amesema watumishi wa Serikali kada ya Afya kuna sehemu hawawajibiki ipasavyo ndio maana malalamiko hayaishi kutoka kwa wananchi.

“Ninyi mmeajiriwa na Serikali na kila kitu kinatolewa na Serikali lakini utashangaa mtu anashindwa kutoa huduma bora
Kwa mwananchi ila mtu huyo huyo jioni unamkuta kwenye kituo binafsi anahudumia vizuri ina maana huku Serikalini anafanya makusudi kwa kutokumjali mteja? Alihoji Dr. Mollel.

Aliongeza kuwa kutokana na hali hiyo unakuta wananchi wanakimbia Kituo cha Serikali wanaenda kwenye kituo binafsi ilihali Serikalini ndio kuna wataalamu wabobezi kuliko hata huko binafsi ila kutokana na huduma zisizoridhisha mwananchi anaona bora aende akalipe hela nyingi apate huduma kuliko kutibiwa kwenye gharama nafuu hii tabia ikome kuanzia sasa na kila mmoja awajibike ipasavyo.

“ Inabidi tuanze kunyooshana pale tunaposkia malalamiko ili hadhi ya Vituo vya kutolea huduma za Afya vya Serikali irudi watu wapewe huduma bora na wafurahie huduma hizo zinazotolewa na Serikali yao hii itasaidia kuongeza mapato ya Serikali na kuendelea kuboresha huduma kwa ujumla.

Watumishi wa Afya lazima wafanye kazi kwa weledi na kufuata kanuni za maadili ya utoaji wa huduma za Afya ili kufikia malengo ya upatikanaji wa huduma bora za Afya kwa wote.

Mwisho Dr.Mollel asisitiza usimamizi makini wa miradi ya maendeleo huku akitolea mfano hospitali ya Wilaya ya Ileje inayojengwa kwa gharama ya shilingi bil 1.8 ilihali maeneo mengine wakiwa wamemaliza kiasi hicho cha fedha na ujenzi haujakamilika.

“Nizitake Halmashauri zingine ziende kujifunza Ileje ambapo wametumia bilioni 1.8 kujenga jengo zuri la Hospitali ilihali halmashauri hii iko pembezoni hata upatikanaji wa vifaa ni mgumu lakini halmashauri zingine za mjini kabisa hawajakamilisha ujenzi na fedha wamemaliza na wanaomba kuongezewa fedha nataka niwaambie tu kuwa hakuna fedha za nyongeza na hospitali hizo zikamilike” Alisema Dr Mollel.

Naye Mkurugenzi wa Huduma za Afya Ustawi wa Jamii na Lishe Dr. Ntuli Kapologwe amemshkuru Naibu Waziri wa Afya kwa maelekezo aliyoyatoa kwa watumishi watendaji wa Afya Mkoa wa Songwe na ameahidi kusimamia utekelezaji wa maagizo hayo.

Pia amewataka waganga wafawidhi wa vituo vyote vya Kutolea Huduma za Afya kuhakikisha wananunua Computer na kufunga mfumo wa GoT-HoMIS ili kudhibiti mapato ya Vituo.

IGP Sirro : Makosa Ya Usalama Barabarani Yamepungua Kwa Asilimia 34

$
0
0


Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro amesema makosa ya ajali barabarani nchini yamepungua kwa asilimia 34 kutokana na madereva wengi kuendelea kutii sheria na alama za barabarani kunakochangiwa na usimamizi mzuri wa askari wa usalama barabarani.

IGP Sirro amesema hayo jana wakati alipofanya kikao kazi na maofisa na askari wa Kikosi cha usalama barabarani wa mikoa ya Kanda maalum ya DSM, Rufiji na mkoa wa Pwani huku akiwataka askari wa Jeshi hilo kupunguza malalamiko kutoka kwa wananchi wanaowahudumia na hasa kuacha kujihusisha na vitendo vya rushwa na kuwasisitiza suala la kutoa huduma bora kwa mteja

Uhakiki Wa Taasisi Za Kidini Na Jumuiya Za Kijamii Katika Kanda Ya Kaskazini Kuanzia Tarehe 15 Februari

Naibu Waziri Bashe Atoa Maagizo Kwa Tume Ya Taifa Ya Umwagiliaji

$
0
0


 Na Mwandishi Wetu – Dodoma.
Naibu Waziri wa Kilimo Mhe. Hussein Bashe, Ameitaka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji, kutumia wataalamu na rasilimali za ndani katika kazi za upembuzi yakinifu katika ujenzi wa Miundombinu ya Umwagiliaji,ili kupunguza gharama za ujenzi wa miradi ya miundombinu hiyo.

Bashe aliliyasema hayo Jijini Dodoma alipokutana na Management ya Tume ya Taifa ya Umwagiliaji na Wahandisi wa Umwagiliaji nchini nakuagiza Mitambo 56 inayomilikiwa na Tume popote ilipo nchini ikaguliwe nakufanyiwa matengenezo huko iliko na yenye hali mbaya iletwe katika ofisi za makao makuu ya Tume jijini Dodoma kwa matengezo zaidi.

Sambamba na hilo aliagiza Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ifanye Utaratibu wa kuyutambua maeneo yote ya kilimo cha umwagiliaji nchini yapo wapi yana ukubwa gani na yanalima mazao gani ilikuweza kujua ni maeneo gani yanayoweza kufanyiwa maboresho na kumwagiliwa kihalisia.

Naibu Waziri Bashe aliwashauri wataalamu hao, kuweza kuona namnayakuhusisha sekta binafsi katika kuboresha miundombinu ya umwagiliaji na kuanzisha kilimo Biashara kupitia sekta ya umwagiliaji, pamoja, nakuwaagiza kuainisha eneo litakalotumika kwa kilimo cha umwagiliaji katika Bwawa la mwalimu Nyerere, nakuliwekea mipaka ili lisiweze kuvamiwa na shughuli nyingine za kibinadamu.

Aidha, Naibu Waziri Bashe ameiagiza Tume hiyo iwe na mpango mkakati wa miaka mitano wautekelezajiwa kuongeza eneo la Umwagiliaji, lenye ukubwa wa Hekta milioni moja sambamba na hilo kuangalia litazalisha mazoa ya aina gani, kwa kiasi gani litakuwa katika vijiji gani na litatumiwa na wakulima wangapi.

“Pamoja na hili mkaena Tasisi ya kuzalisha Mbegu (ASA), Taasisi ya Tafiti ya Mazao ya Kilimo (TARI) ili katika eneo hilo kuweza kutenga walau asilimia ishirini 20% ya eneo kwa ajili ya kuzalisha mbegu”.Alisisitiza.

Naibu Waziri Bashe, Aliitaka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Ifanye ukarabari wa mundombinu ya Umwagiliaji katika skimu kwa kuwwashirikisha wakulima.


TCRA yaifungia Wasafi TV miezi sita kwa kosa la kukiuka kanuni za utangazaji

$
0
0


Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imekifungia kwa miezi sita kituo cha teloevisheni cha Wasafi kwa kosa la kukiuka kanuni za utangazaji katika matangazo yake ya moja kwa moja ya tamasha la ‘Tumewasha na Tigo’.


 Uamuzi huo umefikiwa leo Jumanne Januari 5 baada mamlaka hiyo kukutana na uongozi wa Wasafi TV na kusikiliza utetezi wao.


Kaimu Mkurugenzi wa TCRA, Johanes Kalungule amesema ukiukwaji huo ulifanyika Januari 1, 2021 ambapo televisheni hiyo ilirusha maudhui yaliyomuonyesha msanii Gigy Money akicheza katika mitindo iliyoonyesha utupu wake.


Kalungule amesema kosa hilo ni kinyume na kanuni za utangazaji, hivyo kuanzia muda uliotolewa uamuzi huo Wasafi TV imetakiwa kusitisha matangazo yake na kuomba radhi mfululizo.

Jaji: Assange atajiua akihamishwa hadi Marekani

$
0
0


 Mahakama ya Uingereza imekataa ombi la Marekani la kumuhamisha mwanzilishi wa mtandao wa WikiLeaks, Julian Assange hadi Marekani anapokabiliwa na mashtaka ya ujasusi.

Mahakama imeamua kuwa hatua ya kumuhamisha Assange, ni “Ukandamizaji” kutokana na Afya yake ya kiakili.

Jaji Vanessa Baraitser amesema Assange huenda akajiua iwapo atahamishwa hadi Marekani. Hata hivyo, serikali ya Marekani imesema itakata rufaa juu ya uamuzi huo.

Waendesha mashtaka wa Marekani wanamshtumu Assange kwa makosa 17 ya ujasusi na matumizi mabaya ya Kompyuta kwa kuchapisha mtandaoni nyaraka za siri juu ya oparesheni za jeshi la Marekani nchini Iraq na Afghanistan muongo uliopita.

Iwapo atapatikana na hatia, Assange huenda akapewa kifungo cha miaka 175 jela.

Tito Magoti na mwenzake wahukumiwa kulipa fidia

$
0
0

 


Afisa wa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Tito Magoti na mwenzake Theodory Giyan, leo wameachiwa huru na kukubali kulipa faini ya milioni 17, baada ya kukamatwa Desemba 2019 na kufunguliwa mashtaka matatu ikiwemo la utakatishaji wa fedha.

Hukumu hiyo imetolewa leo Januari 5, 2021 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Janeth Mtega, baada ya washtakiwa hao kukiri makosa yao kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini Tanzania( DPP), ambapo mbali na faini hiyo, mahakama pia imewahukumu adhabu ya kutokutenda kosa lolote la jinai kwa kipindi cha mwaka mmoja kuanzia leo Januari 5, 2021.

Awali, jopo la mawakili wawili wa upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Paul Kadushi, akishirikiana na wakili wa Serikali Mwandamizi, Wankyo Simon, ulidai kuwa kesi hiyo iliitwa kwa ajili ya uamuzi baada ya washtakiwa kukiri makosa yao kwa Mkurugenzi wa Mashtaka nchini( DPP).

Wakili Kadushi ameongeza kuwa washtakiwa hao walikuwa wanakabiliwa na mashtaka matatu, lakini baada ya kufanya majadiliano na DPP walifutiwa mawili na kubakisha shitaka moja ambalo ni kuongoza genge la uhalifu.

Katika kesi ya msingi Tito na Theodory, pamoja na wenzao ambao hawakufikishwa mahakamani wanadaiwa kati ya Februari mosi na Desemba 17, 2019, jijini Dar es Salaam na katika maeneo mbalimbali ya Tanzania, kwa makusudi walishiriki makosa ya uhalifu wa kupanga kwa kumiliki programu za kompyuta iliyotengenezwa mahususi kwa ajili ya kufanya uhalifu na kupelekea kujipatia fedha kiasi cha shilingi milioni 17.

Hata hivyo, kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, mawakili wa washtakiwa hao, Flugence Massawe, Jebra Kambole na Pacience Mlowe waliiomba mahakama hiyo kuwapunguzia adhabu kwa sababu ni vijana wadogo na wanategemewa na familia zao.

Tito Magoti na mwenzake Theodory Giyan walifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza Desemba 24, 2019, na kufunguliwa mashtaka matatu, ikiwemo la kushiriki genge la uhalifu, kumiliki programu ya kompyuta iliyotengenezwa kwa lengo la kutenda uhalifu na utakatishaji wa fedha kiasi cha shilingi milioni 17.


Gigy Money afungiwa miezi sita kutojishughulisha na sanaa

$
0
0


Baraza la Sanaa Taifa ( BASATA ) limemfungia miezi sita msanii wa muziki ‘Gigy Money kutojushughulisha na shughuli zozote za muziki.

Katika taarifa yao, Basata imeeleza kuwa imefikia hatua hiyo baada ya msanii huyo kuvaa nguo zisizo na maadili katika Tamasha la Wasafi ililofanyia Alhamisi iliyopita jijini Dodoma, hivyo kukiuka kanuni za kifungu cha 4(L) cha sheria namba .23 ya mwaka 1984.

Basata imesema adhabu hiyo inaendana na faini ya Sh milioni moja na kwamba adhabu hiyo imezingatia kanuni ya 64 (1)( a)-(i) za Baraza la Sanaa Tanzania mwaka 2018.

Dkt. Ndugulile Awataka Wafanyakazi Wa Wizara Kuacha Kufanya Kazi Kwa Mazoea

$
0
0


 Na Prisca Ulomi, WMTH
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile amewataka wafanyakazi wa Wizara yake kuacha kufanya kazi kwa mazoea badala yake wafanye kazi kwa ubunifu, kujituma, watumie TEHAMA kutatua changamoto za wananchi, wahakikishe TEHAMA inachangia kikamilifu pato la taifa kwa kuwa Mkongo wa Taifa wa Mawasiliano ni barabara ya dunia ya sasa ya kidijitali

Dkt. Ndugulile ameyasema hayo wakati wa kikao chake na wafanyakazi wa Wizara hiyo kilichofanyika Dodoma na kuhudhuriwa na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Dkt. Zainab Chaula, Naibu Katibu Mkuu, Dkt. Jim Yonazi na wajumbe wa Menejimenti ya Wizara hiyo mpya

Amewataka wafanyakazi hao kuacha kufanya kazi kwa mazoea na yeye sio muumini wa michakato bali anahitaji kuona matokeo ili kuhakikisha kuwa TEHAMA inatumika kujibu changamato za wananchi ili mwananchi apate huduma za Serikali mahali popote alipo badala ya kufuata watendaji walipo

“Nataka kuona bwana shamba anatumia mawasiliano kupata mbegu, pembejeo na wakulima watumie TEHAMA kupata masoko, waalimu tulionao watumie TEHAMA kufundishia wanafunzi kwa kuwa Wizara hii ina dhamana na masuala ya TEHAMA, ndiyo yenye sera ya TEHAMA, inatoa miongozo, sheria, kanuni na viwango kwa taasisi zote za Serikali, sekta binafsi na wananchi”, amesisitiza Dkt. Ndugulile

Amefafanua kuwa sasa hivi Serikali inatumia fedha nyingi kununua mifumo ya TEHAMA nje ya nchi, hivyo anataka wabunifu wa TEHAMA wazuri waliopo nchini watumike kutengeneza mitandao yetu ya kijamii na mifumo yetu ya TEHAMA ambayo ina jibu changamoto za wananchi ili Tanzania tuwe na mitandao yetu na mifumo yetu ya TEHAMA ili kuongeza pato la Taifa

Katibu Mkuu wa Wizara, Dkt. Zainab Chaula amesema kuwa kikao hicho kitawawezesha wafanyakazi kuwa na dira na mwelekeo wa pamoja katika kutekeleza majukumju ya Wizara mpya na Naibu Katibu Mkuu, Dkt. Jim Yonazi amemshukuru Waziri kwa kikao hicho na kuongeza ari kwa wafanyakazi kutumikia wananchi

Naye Mwenyekiti wa TUGHE wa Wizara hiyo, Laurencia Masigo amemweleza Dkt. Ndugulile kuwa wafanyakazi wako tayari kufanya kazi kwa ushirikiano, kujituma na kushirikiana na Menejimenti na kushauri yapi yafanyike katika nyanja ya TEHAMA ili kukuza uchumi wa taifa letu

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini

Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>