Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Vanessa Mdee avalishwa pete ya Uchumba na Mpenzi wake Rotimi

$
0
0

MWANAMUZIKI wa Tanzania, Vanessa Mdee, amevalishwa pete ya uchumba na mpenzi wake Rotimi ambaye ni msanii wa filamu ambapo wote kwa sasa wanaishi nchini Marekani.

‘Videos clips’ ambazo zimepostiwa kwenye mitandao ya kijamii zimeonyesha Rotimi akiwa amepiga magoti mbele ya Vanessa huku akimvalisha pete hiyo ya uchumba, kisha wakakumbatiana na kuanza kupigana mabusu.
 
Vanessa amethibitisha hilo kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo ameweka video mbili moja ikionesha pete aliyovishwa huku nyingine ikiwa ni kipande cha video ya mahojiano aliyowahi kufanya na moja ya vyombo vya habari na kusema ilimgharimu siku mbili tu kujua kwamba Rotimi ndiye atakayekuja kuwa mume wake.

“Mwaka mmoja na nusu uliopita dunia ilicheka niliposema kuwa nilijua kuwa wewe utakuja kuwa mume wangu muda mfupi baada ya kukufahamu, sikuwalaumu kwani hisia unayoipata pale unapokutana na mpenzi wa maisha yako si ya kawaida na haiwezi kuelezeka lakini pia wao walikuwa wakimfahamu Vanessa ambaye hakuwa na mpango wa kuolewa kwa wakati huo,” ameandika Vanessa.

Rotimi naye kupitia ukurasa wake wa Instagrama ameweka video fupi ya pete aliyomvalisha Vanessa akiambatanisha na ujumbe unaoelezea namna anavyompenda mrembo huyo.

“Unanifanya niwe mwanaume bora. Nina deni kwa Mungu kwa kunipa wewe na nitamlipa kwa kukupenda na kukupa kila kitu unachostahili, nakupenda,” ameandika Rotimi.

Uhusiano wa wawili hao ulianza mwaka 2019 baada ya Vanessa kuachana na aliyekuwa mpenzi wake, mwanamuziki wa Tanzania, Jux.

Kwa sasa Vanessa ambaye mwezi Juni alitangaza kuachana na shughuli za muziki anaishi Marekani pamoja na mwanume huyo na mara kadhaa amekaririwa akimsifia kuwa ni mwanaume aliyefanya aitambue thamani ya maisha yake.

Mwanzoni mwa mwezi wa kumi mwaka 2020, Vanessa  na Rotimi walishea picha mitandaoni zikiwaonyesha wamechorana ‘tattoo’ zenye majina yao kwenye miili yao.


Waziri wa Mambo ya Nje wa China kufanya ziara Tanzania

$
0
0


Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Profesa Palamagamba Kabudi amesema mtazamo wa Tanzania kwa Bara la Afrika ni kuona linajitegemea kwa kutumia rasilimali zake kufanya maendeleo.
 
Waziri Kabudi ameyasema hayo jijini Dar es salaam wakati wa mkutano wake na Waandishi wa habari, ambapo pamoja na mambo mengine amezungumzia ujio wa Waziri wa Mambo ya Nje wa China Wang Yi Januari 7 mwaka 2021.

Ziara ya siku mbili ya Wang Yi hapa nchini, ni muendelezo wa uhusiano wa muda mrefu baina ya Tanzania na China.

Rais Magufuli Arejesha Fomu zake za maadili katika ofisi ya makao makuu ya Sekratarieti ya Maadili ya viongozi

$
0
0


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 31 Desemba, 2020 amewasilisha fomu zake za maadili katika ofisi ya makao makuu ya Sekratarieti ya Maadili ya viongozi Jijini Dodoma.

Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike amekabidhi fomu hizo kwa Kamishna wa Maadili, Jaji wa Mahakama ya Rufani Mhe. Sivangilwa Sikalalilwa Mwangesi.

Leo ni siku ya mwisho ya kuwasilisha fomu za maadili kwa viongozi wote kwa mujibu wa Sheria namba 13 ya mwaka 1995 ya Maadili ya Viongozi wa Umma

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa January 1, 2020

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi January 2

Serikali Kuweka Mazingira Wezeshi Ya Kuendeleza Vijana Wabunifu Wa Tehama

$
0
0


Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Dkt. Faustine Ndugulile amesema kuwa Serikali itaweka mazingira wezeshi ya kuendeleza vijana wabunifu wa TEHAMA nchini

Ndkt. Ndugulile ameyasema hayo jana  wakati wa ziara yake ya kutembelea Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) na Ndaki ya TEHAMA ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (COICT) zilizopo Dar es Salaam

Amesema kuwa vijana wanabuni mifumo mbali mbali ya TEHAMA ya kutatua changamoto za wananchi ila wanakosa mazingira wezeshi ya kuendeleza na kukuza bunifu zao kama vile kupatiwa muda maalumu wa kuingiza sokoni bunifu zao kwa kufanya majaribio ya bunifu hizo kukubalika kwa wananchi bila kulazimika kulipia gharama za usajili, kupata masoko, malipo ya kodi na leseni kuendana na matakwa ya uendeshaji wa kampuni na biashara nchini

Amesisitiza kuwa azma ya Serikali ni kuendeleza wabunifu wa TEHAMA ili waweze kutengeneza mifumo kuendana na mahitaji ya wananchi badala ya kuendelea kununua mifumo hiyo kwa gharama kubwa kutoka nje ya nchi ambapo Serikali inatumia fedha nyingi kununua mifumo ya TEHAMA

Amefafanua kuwa utengenezaji wa mifumo ya TEHAMA hapa nchini utaongeza wigo wa matumizi ya intaneti na huduma za mawasiliano na itajibu changamoto za wananchi na ametoa rai kwa watanzania kujenga imani ya kutumia teknolojia rahisi zinazobuniwa na vijana wa ndani ya nchi bila kujali umri, uzoefu au majina ya kampuni zao

Naye Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH, Dkt. Amos Nungu amesema kuwa vijana haom wameanzisha kampuni zaidi ya 20 za mifumo ya TEHAMA na tayari mifumo hiyo inasaidia kukusanya kodi kwenye halmashauri; kuwawezesha vijana kusoma VETA kwa njia ya mtandao na TIGO kuweza kuhifadhi taarifa za wateja wake

Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu, utafiti na ubunifu, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Prof. Benadetha Kiliani na Mkuu wa Ndaki ya TEHAMA ya Chuo hicho, Dkt. Mussa Kisaka wamesema kuwa Chuo kiko tayari kushirikiana na Wizara ili kuendeleza vijana wabunifu na watafiti wa TEHAMA nchini

Akizungumza kwa niaba ya vijana wabunifu wa TEHAMA, Geofrey Magila ameiomba Serikali kuwawezesha wakubalike na kuaminika na wapewe kazi badala ya kampuni zao kufanya kazi kwa kutumia mgongo na majina ya kampuni nyingine kwa kuwa kampuni zao ni changa na hazina mtaji wa kutosha kuingia kwenye ushindani wa zabuni zinazotangazwa zinazohusu mifumo ya TEHAMA

“Tulipata kazi kutoka kampuni ya AIS ya simu za mkononi ya Malyasia yenye wateja zaidi ya milioni 50 ambao walituamini na tuliwatengenezea mifumo ya kulinda taarifa za wateja wao, ndipo baadae baadhi ya kampuni za ndani ya nchi zikaanza kutuamini,” amesema Magila

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari


Chukueni Hatua Kali Kwa Wanaoharibu Miundombinu Ya Barabara – Kasekenya

$
0
0


Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, amezitaka Mamlaka mkoani Rukwa kusimamia kikamilifu Sheria ya Mazingira ya mwaka 2004 inayozuia shughuli za kibinadamu katika maeneo ya hifadhi ili kulinda barabara na madaraja katika bonde la mto Rukwa.

Amesema hayo mara baada ya kukagua barabara ya Ntendo – Muze Kilometa 37 na barabara ya Kasansa – Kilyamatundu Kilometa 175 ambazo zimeathiriwa na mafuriko ya mvua kutokana na shughuli za kibinadamu za ukataji miti, kilimo na ufugaji katika safu za milima ya ukanda wa bonde hilo.

“Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi na Wenyeviti wa vijiji na vitongoji hakikisheni tabia ya uharibifu wa mazingira zinazofanywa na wananchi zinakomeshwa maramoja ili kulinda hifadhi za misitu na miundombinu ya barabara na madaraja”, amesisitiza Mhandisi Kasekenya.

Naibu Waziri huyo amesema zaidi ya shilingi Bilioni 4.4 zimetengwa kwa ajili ya kuhakikisha barabara hizo zilizoko katika bonde la mto Rukwa ambalo ni maarufu kwa uzalishaji wa mazao ya chakula zinakarabatiwa ili kupitika wakati wote wa mwaka na kutoathiri uchumi wa wakazi wa mkoa huo.

Naye Kaimu Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) mkoa wa Rukwa,  Mhandisi Jotrevas August, amesema zaidi ya madaraja madogo 19 yamebomolewa na mvua hizo zinazoendelea kunyesha katika ukanda huo na hivyo Wakala umejipanga kuhakikisha kuwa ujenzi wake unaendelea ili kutoathiri huduma ya usafiri katika barabara hizo.

Kwa upande wake Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dakta. Khalfan Haule, amemhakikishia Naibu Waziri kwamba kwa kushirikiana na watendaji wa kata na vijiji watahakikisha miundombinu ya barabara na madaraja inayojengwa inalindwa ili ikamilike kwa wakati.

Naibu Waziri Kasekenya yuko katika ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa miundombinu katika mikoa ya Mbeya, Songwe, Rukwa na Katavi.

Naibu Waziri Mabula Awashukia Wakurugenzi Halmashauri Kuzitelekeza Idara Za Ardhi

$
0
0


Na Munir Shemweta, WANMM KIBAHA
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendelea ya Makazi Dkt Angeline Mabula amewajia juu baadhi ya wakurugenzi wa halamashauri kwa kushindwa kuzihudumia idara za ardhi katika halmashauri zao na kuzifanya idara hizo kufanya kazi katika mazingira magumu.

Akizungumza na watendaji wa sekta ya ardhi, uongozi wa mkoa wa Pwani na Wakurugenzi wa halmashauri za mkoa huo tarehe 31 Desemba 2020 akiwa katika ziara ya kukagua utendaji kazi wa sekta ya ardhi na kukagua miradi inayotekelezwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) katika mkoa wa Pwani, Dkt Mabula alisema kuna baadhi ya wakurugenzi wa halmashauri wamekuwa wakorofi na kuziona idara za ardhi kama siyo sehemu ya idara zao na kuziacha bila kuzihudumia.

Alisema, baada ya kutoka waraka uliohamisha Maafisa Ardhi kurudi Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi kuna baadhi ya Wakurugenzi wa Halmashauri waliamua kujivua kuzihudumia idara hizo kwa kisingizio kuwa idara hizo sasa haziko chini yao na zimerejeshwa Wizarani.

Dkt Mabula alisema, waraka uliotolewa na kusambazwa kwa Makatibu Tawala wa Mikoa  ulieleza wazi kuwa wajibu wa Wizara ya Ardhi kwa watumishi wa sekta hiyo utakuwa kwenye  masuala ya sera, ajira na nidhamu lakini usimamizi utaendelea kubaki kwa wakurugenzi wa halmashauri.

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, majukumu ya kupanga miji ni ya halmashauri za miji , manispaa na majiji hivyo wakurugenzi wa halmashauri bado wana wajibu wa kuzihudumia idara hizo ili ziweze kupanga miji vizuri pamoja na kutoa huduma zinazohusiana na masuala ya ardhi.

‘’Hawa ni watumishi wenu kama walivyo wale wa idara nyingine za afya, elimu nk hivyo mnapaswa kuwahudumia vizuri ikiwemo kuwapatia vitendea kazi ili waweze kufanya kazi vizuri’’ alisema Dkt Mabula.

Aliwataka Wakurugenzi wa Halmashauri kubadilika na kuanza kuzihudumia idara za ardhi vizuri kwa kuzipangia idara hizo bajeti ya kutosha pamoja vitendea kazi kama magari na vifaa vya kupimia ili ziweze  kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi.

Akigeukia suala la ukusanyaji maduhuli ya serikali kupitia kodi ya pango la ardhi, Naibu Waziri Mabula aliwataka wakurugenzi wa halmashauri zote nchini kuziwezesha idara za ardhi ili ziweze kufuatilia madeni ya wadaiwa sugu wa kodi ya ardhi katika maeneo mbalimbali.

Kwa mujibu wa Dkt Mabula, mkoa wa Pwani pekee unadai bilioni 32, 762,665,972 za kodi ya pango la ardhi kutoka kwa wadaiwa mbalimbali na kusisitiza kuwa kama  idara za ardhi zitawezeshwa vizuri zinaweza kukusanya mapato mengi  yatakayosaidia utekelezaji  miradi mbalimbali kama vile ya afya, elimu na miundombinu ukilinganisha na idara nyingine.

Kwa upande wake Mkuu wa Kitengo cha Kodi Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Denis Masamia alisema, pamoja na mikakati iliyowekwa na Wizara yake katika kukusanya kodi bado kuna kazi kubwa ya kufanya katika suala hilo kutokana na hadi kufikia Desemba 31, 2020 ni Bilioni 61 ndizo zilizokusanywa na kutaka juhudi za makusanywa kuongezwa katika kila halmashauri. Malengo ya Wizara katika mwaka wa fedha 2020/2021 ni bilioni 200.

Katika hatua nyingine, Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula ametembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa Ofisi ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) Kanda ya Mashariki uliopo wilayani Kibaha mkoani Pwani mradi unaojengwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC).

Akiwa katika mradi wa ujenzi wa Ofisi hiyo , Dkt Mabula alilipongeza Shirika la Nyumba la Taifa kwa kazi nzuri ya ujenzi wa miradi mbalimbali iliyokabidhiwa na kulitaka kuhakikisha ujenzi wa miradi hiyo unakamilika kwa wakati na kwa ubora ili kujenga imani kwa wateja.


Halmashauri Zaonywa Wafanyabiashara Kuchanja Mifugo, Mikataba Yao Kuvunjwa

$
0
0


Na. Edward Kondela
Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki amepiga marufuku halmashauri zote nchini kutotumia wafanyabiashara kuchanja mifugo na kutaka kuvunjwa kwa mikataba hiyo mara moja.

Waziri Ndaki amebainisha hayo  (31.12.2020) alipofanya ziara ya kikazi ya siku moja Mkoani Shinyanga ambapo alipokuwa katika josho la kuogeshea mifugo la Kijiji cha Mipa kilichopo Wilaya ya Kishapu mkoani humo kwa ajili ya kushuhudia uogeshaji mifugo na utoaji wa chanjo ya homa ya mapafu kwa ng’ombe, wafugaji wamemlalamikia kuwa baadhi ya ng’ombe kijijini hapo wamekuwa wakivimba na wengine kufa baada ya kupatiwa chanjo.

Waziri Ndaki akiwa ameambatana na Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Pauline Gekul amesema kuanzia sasa chanjo zote nchini zitatolewa na wataalamu wa wizara ambao wamethibitishwa na kugoma kushuhudia zoezi la uchanjaji lililokuwa limeandaliwa baada ya kukasirishwa na uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu kutokuwa na takwimu yoyote ya idadi ya ng’ombe waliovimba na wengine kufa baada ya kuchanjwa.

“Halmashauri zetu zote kuanzia sasa hivi ni marufuku kutumia wafanyabiashara kuchanja mifugo yetu, halmashauri zitumie wataalamu wa wizara ambao wamethibitishwa waweze kuchanja mifugo ya wananchi wetu, hao wafanyabiashara kama mmeingia mikataba nao hiyo mikataba ivunjeni haraka iwezekanavyo hatuwezi kuchezea akili za watu namna hii hatuwezi kutuma wafanyabiashara waende kuchanja ng’ombe wanavimba na wanakufa halafu taarifa hatuna.” Amesema Mhe. Ndaki

Aidha, Waziri Ndaki katika ziara yake ya siku moja Mkoani Shinyanga amefika katika mnada wa upili wa Mhunze ambao ni moja ya minada inayosimamiwa na wizara na kumuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu kumuondoa mara moja kazini mhasibu wa halmashauri hiyo anayefanya kazi katika mnada huo Bw. Athanas Msiba kwa tuhuma za kutokuwa mwaminifu katika kuandika idadi ya mifugo inayoingia na kutoka katika mnada huo hali inayosababisha wizara na halmashauri kukosa mapato stahiki.

“Mkurugenzi huyu Athanas Msiba siyo mwaminifu hafai kukaa hapa tena aondoke sasa hivi ulete mtu mwingine, watu wakipita hapa na mbuzi watano anaandika watatu anaandika kidogo hafai aondoke hapa.” Amesema Mhe. Ndaki

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Bw. Emmanuel Johnson amesema amepokea maelekezo hayo na atayafanyia kazi kwa kuihusisha pia Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) ili ifanye ufuatiliaji kwa kuwa serikali haiko tayari kuwa na watu wenye tabia ya namna hiyo.

Akiwa katika mnada huo Waziri Ndaki amepata fursa ya kusikiliza kero mbalimbali kutoka kwa wafanyabiashara na wafugaji ikiwemo ya kuzuiwa kuondoa mifugo mnadani kabla ya saa 12 jioni hali inayohatarisha maisha yao kutokana na uwepo wa fisi wengi kwenye maeneo ya mashamba wakati wa kurudi nyumbani majira ya jioni hali iliyomlazimu Waziri Ndaki kuutaka uongozi wa mnada utafute utaratibu wa kuwaruhusu wafanyabiashara kuondoka kabla ya muda huo wakiwa wamemaliza shughuli zao.

“Mtu amemaliza biashara yake mkagueni vizuri kwenye mlango wa kutokea aende zake akimaliza hapa akikaa saa mbili aondoke, akikaa dakika 15 aondoke ili mradi amemaliza shughuli zake siyo unawaleta unawafungia humu haka kamekuwa kajela kadogo? Hapana hiyo.” Amefafanua Waziri Ndaki

Akiwa Mkoani Shinyanga Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe. Mashimba Ndaki na Naibu Waziri Mhe. Pauline Gekul, ametembelea ujenzi wa mradi wa machinjio ya kisasa yaliyopo katika Manispaa ya Shinyanga unaogharimu Shilingi Bilioni 5.5 ambapo tayari zimelipwa Shilingi Bilioni 5.1 na umefikia asilimia 97 hadi kukamilika kwake.

Mara baada ya kukamilika machinjio hayo Mwezi Februari Mwaka 2021, yatakuwa na uwezo wa kuchinja ng’ombe 500 mbuzi na kondoo 1,000 kwa siku.

Siku moja kabla ya kuanza ziara ya kikazi Mkoani Shinyanga, Waziri Ndaki akiwa na Naibu Waziri Mhe. Pauline Gekul walifika katika shamba la mifugo la serikali Shishiyu Holding Ground lililopo katika Wilaya ya Maswa Mkoani Simiyu, ambapo Waziri Ndaki amesema shamba hilo lenye ekari 10,240 halina tija kwa sasa kwa kuwa limebaki pori na hakuna mifugo.

Ameongeza kuwa Wizara ya Mifugo na Uvuvi inataka maeneo yote ya mashamba ya serikali ya mifugo ambayo yapo chini ya wizara kuyaweka chini ya Kampuni ya Ranchi za Taifa (NARCO), ili NARCO washughulike nayo kwa sababu ni chombo pekee cha wizara kinachokubaliwa kufanya biashara ya kupangisha maeneo kwenye mashamba ya wizara.

Waziri Ndaki amefikia hatua hiyo baada ya Halmashauri ya Wilaya ya Maswa kuomba ekari 1,500 ili kuendeleza shamba hilo kwa ajili ya kunenepesha mifugo ikiwemo kuotesha malisho pamoja na kuelimisha wananchi namna ya kufuga mbegu bora za mifugo, ambapo Waziri Ndaki amesema atatoa maamuzi ya ombi lao haraka iwezekanavyo.

Amefafanua kuwa haina maana wizara kuwa na maeneo makubwa katika mashamba yake ambayo hayatumiki huku wafugaji wakiwa hawana maeneo ya malisho yao hivyo ni bora kuyapangisha ili serikali iweze kupata mapato kupitia mashamba hayo.

Waziri Kalemani Aigiza Tanesco Kuwaombea Ajira Watumishi Walioajiriwa Kwa Mikataba Ya Muda Mfupi Kwa Kipindi Kirefu.

$
0
0


Na Dorina G. Makaya – Shinyanga.
Waziri wa Nishati Mhe. Dkt. Medard Kalemani, ameliagiza Shirika la TANESCO nchi nzima, kuwaombea ajira watumishi walioajiriwa kwa vipindi vifupi na kuitumikia TANESCO kwa muda mrefu.

Waziri Kalemani ametoa agizo hilo tarehe 30 Mwezi Desemba, alipokuwa akizungumza na watumishi wa TANESCO wa Mkoa wa Shinyanga, katika kikao kazi cha kufahamiana, kusikiliza kero na kutoa maelekezo ya kazi ili kuliwezesha shirika la TANESCO nchini kufanya kazi kama timu moja kwa kasi kwa ubunifu na kwa usahihi ili kufikisha huduma ya umeme kote nchini na kuongeza mapato ya Serikali kutokana na Sekta ya Nishati.

Akizungumza baada ya kusikiliza Kero za Watumishi wa TANESCO mkoa wa shinyanga, Waziri Kalemani ameweka bayana kuwa, watumishi hao wanaoajiriwa kwa vipindi vifupi ndio wanaokutana na wateja moja kwa moja na kujenga taswira ya TANESCO (Visibility) kwa wateja wanaohitaji na kutumia huduma ya umeme hapa nchini.

Amesema, kufanya kazi kama kibarua kwa miaka mingi bila ya kuajiriwa kwa watumishi hao, kunapunguza na pengine kuondoa hari ya kufanya kazi watumishi hao, kuleta mianya ya rushwa na hata kutengeneza vishoka.

Dkt. Kalemani ameeleza kuwa, anaamini kuajiriwa kwa watumishi hao, kutawajengea kufanya kazi kwa uaminifu na kwa kujituma kwani watahitaji kutunza ajira zao na kuonya kuwa, mtumishi yeyote atakayebainika anaomba rushwa  kutoka kwa wateja na kutumia lugha zisizofaa, huyo atondolewa mara moja na hatua za kinidhamu kuchukuliwa dhidi yake.

Akielezea kuhusu umuhimu wa kikao kazi hicho, Waziri Kalemani amefafanua kuwa, ili kuwezesha utekelezaji mzuri wa kazi, ipo haja ya kuonana na watumishi, kufahamiana, kujionea mazingira halisi ya kazi, kusikiliza kero zao na kuzitolea ufumbuzi na kisha kutoa mwelekeo na maelekezo ya kazi kufikia malengo yaliyowekwa kwenye Sekta ya NIshati.

“Unaweza kuwa unaagiza nataka kazi hii ifanyike leo na kukamilika leo hii hii, na kumbe unayempa maelekezo hayo ni mlemavu na hana uwezo wa kwenda kwa kasi hiyo. Ukaagiza afukuzwe kwa kushindwa kutekeleza kazi husika, lakini kumbe uliyemwagiza ni mlemavu. Hivyo ni muhimu kufahamiana. Amesema Dkt. Kalemani.”

Aidha, Waziri huyo wa Nishati  ameiagiza TANESCO, kuwanunulia pikipiki watumishi walio katika vitengo vya upimaji  kwa ajili ya kufikisha umeme kwa wateja ( surveyors ) ili kuwezesha utendaji kazi kwa haraka na kuwaelekeza watumishi hao kuzitumia pikipiki hizo kwa shughuli za kikazi. “msije mkazigeuza pikipiki hizo kuwa bodaboda!  Tena mziandike SU. Nataka mfanye kazi kwa kasi, kwa ubunifu, na kwa usahihi,  amesema Waziri Kalemani.

Nataka kila ofisi ya TANESCO ninayo kwenda nione kuna ongezeko la mapato, nione kuna ongezeko la wateja sugu kulipa madeni  wanayodaiwa TANESCO.

Waziri Kalemani ameigiza TANESCO na REA kuhakisha vijiji vyote nchini viwe vimeunganishwa na umeme, ifikapo Septemba 2022.

Dkt. Kalemani pia ameiagiza TANESCO kutumia nguzo za zege kwenye maeneo korofi yenye maji (Swamp areas) ili kuepusha gharama za matengenezo zinazotokana na nguzo kuanguka mara kwa mara na wateja kukosa umeme wakati matengenezo yanapokuwa yanafanyika kurejesha umeme. Aidha, Waziri Kalemani ameielekeza TANESCO nchini, kutoza gharama za uunganishwaji wa umeme kwa wateja kwenye vijiji na vitongoji kwa gharama ya shilingi 27,000 tu kwa wateja wanaotumia njia moja ya umeme isipokuwa katika maeneo ya majiji.

Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya Azitaka Taasisi Kujipanga Upya

$
0
0

Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Mhandisi Godfrey Kasekenya, amezitaka taasisi zilizo chini ya Wizara hiyo kufanya kazi kwa bidii na ubunifu ili kutatua kero na malalamiko ya wananchi kwa wakati katika miradi na huduma wanazozitoa.

Akizungumza mkoani Rukwa mara baada ya kukagua ujenzi wa barabara ya Sumbawanga –  Matai – Kasanga Port yenye urefu wa kilometa 112  na upanuzi wa bandari ya Kasanga, Naibu Waziri Kasekenya ameridhishwa na utekelezaji wa barabara hiyo na kumtaka mkandarasi China Railway 15 Group kukamilisha sehemu iliyobaki yenye urefu wa mita 150 katika kipindi cha siku 45.

Aidha, amemtaka Mkandarasi Shanxi Construction Engineering anaetekeleza mradi wa upanuzi wa bandari ya Kasanga kutathmini kazi anayoifanya kama iko katika viwango vinavyokubalika kwa mujibu wa mkataba kabla ya kuchukuliwa hatua.

“Hakikisheni kazi za ujenzi wa barabara na upanuzi wa bandari zinakamilika katika kipindi kifupi kuanzia sasa, kwa kuwa muda uliopangwa kimkataba umemalizika”, amesema Naibu Waziri Kasekenya.

Naibu Waziri huyo amemuagiza Mkurugenzi wa Huduma za Uhandisi wa Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA) na Meneja wa Bandari ya Kigoma kufika eneo la mradi ndani ya wiki moja kwa ajili ya kukagua maendeleo ya mradi huo na kutoa ripoti.

Kukamilika kwa barabara ya Sumbawanga – Matai – Kasanga Port na upanuzi wa bandari ya Kasanga ni mkakati wa Serikali wa kuhuisha uchumi katika ukanda wa Magharibi wenye mikoa ya Songwe, Rukwa na Katavi na hivyo kuchochea biashara kati ya Tanzania na nchi za Zambia, Burundi na Congo DRC.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Kalambo, Karolius Misungwi, amemhakikishia Naibu Waziri huyo kuwa kukamilika kwa miradi hiyo kuchochea shughuli za kibiashara za Wilaya na kuiomba Serikali kuendelea kuibua fursa za kiuchumi kwenye ukanda huo wenye uzalishaji mkubwa wa mazao ya chakula na biashara.

Naibu Waziri Kasekenya yupo katika ziara ya kukagua miradi ya ujenzi wa miundombinu katika Ukanda wa mikoa ya Magharibi ambapo pamoja na mambo mengine anakutana na watumishi wa Wizara ili kubadilishana uzoefu.

NFRA Wajipange kununua Mahindi mengi kwa Wakulima – RC Wangabo

$
0
0


Wakati Utekelezaji wa lengo la Serikali kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) la kuweka mfumo wa kisasa wa kutunza mazao kufikia asilimia 80. Wakala hao wameshauriwa kujiandaa kununua mahindi mengi Zaidi ili kuwahakikishia wakulima soko la mazao yao katika kipindi cha msimu wa 2020/2021

Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Mh. Joachim Wangabo amesema kuwa ni vyema NFRA wakaongeza fedha za kununua mahindi na kisha kutafuta soko nje ya nchi hasa katika nchi za Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) Pamoja na nchi nyingine ili kuwapa fursa wakulima nchini kufanya biashara na NFRA ili kuepuka kuhangaika kutafuta soko la mazao yao.

“Mkoa wa Rukwa tumezalisha tani za mahindi tani 585,000 na matumizi yetu ya ndani ni tani 291,000 kwahiyo tulikuwa tuna ziada ya tani 294,000, sasa ukiangalia kwamba tani 294,000 halafu mahindi yananunuliwa tani 11,000 kwahiyo mahindi mengi yalibaki ndio kikawa kilio cha wakulima wa mkoa wetu wa Rukwa kwahiyo nategemea kwamba ukamilishwaji wa vihenge hivi NFRA itakuwa na uwezo wa kuchukua tani 58,500, hii kwa sisi mkoa wa Rukwa ni sawa na kuingiza na kutoa ili wawauzie watu wengine.”

“Kwahiyo niwaombe NFRA ndio wamekuwa mkombozi sasa kwa wakulima, mjipange vizuri ili kuongeza fedha muweze kununua mahindi mengi kwa wakulima vinginevyo wakulima watakata tamaa na sasa wanaendelea kuzalisha baada ya kuona kwamba hivi vihenge hapa vinakwenda kukamilika kwahiyo uwezo wa NFRA utakuwa mkubwa Zaidi wa kununua mahindi kwa wakulima, ninyi mnao uwezo wa kuona wapi muyapeleke hayo mahindi, ninyi mfanye biashara na nje na sisi tufanye biashara na nyie,” Alisema.

Kwa upande wake Mhandisi Mkazi kutoka Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Mhandisi Haruna Kalunga amesema kuwa hadi tarehe 28.12.2020mkandarasi ameshatumia muda wake wa miezi 15 sawa na asilimia 83 ya muda aliopewa kwenye mkataba huku utekelezaji ukiwa ni asilimia 80 na hivyo kuufanya mradi kuwa nyuma kwa asilimia 3 na kuongeza kuwa ucheleweshwaji huo umechangiwa na kucheleweshwa kwa msamaha wa kodi wa vifaa vinavyotoka nje ya Tanzania.

Kwa mkoa wa Rukwa mradi huo unatekelezwa na Mkandarasi Unia Araj kutoka Poland ikisaidiana na Mkandarasi Mzawa Elerai kutokea Arusha kwa thamani ya Dola za marekani 6,019,399.00 ambayo ni asilimia 30 ya mradi mzima unaotekelezwa katika mikoa mitatu Pamoja na Mkoa wa Katavi na Manyara wenye jumla ya thamani yad ola za marekani 20,280,906.00.

Taarifa Ya Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) ya Makusanyo Ya Kodi Mwezi Desemba 2020

$
0
0


Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imevunja rekodi kwa kukusanya mapato ya Shilingi Trilioni 2.088 ikiwa ni sawa na ongezeko la asilimia 101, katika robo ya pili ya mwaka wa fedha wa 2020/2021 ikilinganishwa na Shilingi Trilioni 1.664 iliyokusanywa katika robo ya kwanza iliyoishia mwezi Septemba mwaka 2020.

Akitoa taarifa hiyo jijini Dar es salaam, Kamishna Mkuu wa TRA Dkt Edwin Mhede amesema, kiwango hicho cha ukusanyaji.mapato kimevuka lengo walilojiwekea la kukusanya Shilingi Trilioni 2.072.

Amewaambia Waandishi wa habari kuwa, ongezèko hilo la ukusanya mapato kwa kiasi kikubwa limechangiwa na mwamko wa Walipa kodi ambao wamekuwa wakilipa kodi zao kwa hiari.

Kwa mujibu wa Dkt Mhede, Idara ya walipa kodi wakubwa  kwa  mwezi Desemba mwaka 2020 pekee ilikusanya takribani Shilingi Trilioni Moja, Idara ya forodha ilikusanya mapato ya asilimia 97 ikikuatiwa na Idara ya walipa kodi.

Benard Membe Atangaza Kung'atuka ACT- Wazalendo

$
0
0


Aliyekuwa mgombea urais kupitia chama cha ACT Wazalendo, Bernard Membe ametangaza rasmi kujiuzulu uanachama na  nafasi ya mshauri mkuu wa chama hicho.

Amesema kwa sasa, atabakia kuwa mshauri kitaifa na kimataifa wa kushughulikia na kupigia debe masuala ya demokrasia kwa taifa lake.

Hatua ya kujiuzulu ameitangaza kijiji kwao Rondo- Chiponda Mkoani Lindi, nchini Tanzania jana Ijumaa tarehe 01 Januari 2021, wakati akizungumza na DW.

Hata hivyo, hakutoa ufafanuzi zaidi juu ya sababu ya kuchukua maamuzi hayo.

Membe amesema,tayari ameandika barua ya kujiuzulu kwa kiongozi wa ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe kama utaratibu unavyotaka.

Hata hivyo, waziri huyo wa zamani wa mambo ya nje wa Tanzania katika utawala wa awamu ya nne ya Jakaya Mrisho Kikwete amesema, kwa sasa ni mapema kubainisha mwelekeo wake unaofuata katika vyama vya siasa.

Membe aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania kati ya 2007 hadi 2015 ametangaza uamuzi huo leo akiwa nyumbani kwake kijijini Rondo Chiponda, Wilaya ya Mtama Mkoani Lindi ambapo amesema hajafanya uamuzi huo kwa shinikizo lolote na kwamba kwa sasa atakuwa mshauri wa masuala mbalimbali yanayoihusu nchi ya Tanzania na kupigania demokrasia ya kweli.

Mwanadiplomasia huyo alitangaza kuhamia Chama cha ACT Wazalendo miezi michache kabla ya uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2020 baada ya kufukuzwa uanachama wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) tarehe 28 Februari 2020 na Kamati Kuu ya chama hicho, kisha uamuzi huo kubarikiwa na Mkutano wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), tarehe 10 Julai 2020.

Membe alifukuzwa kwa tuhuma za ukiukwaji wa maadili ya CCM, pamoja na kuonywa mara kadhaa, pasina kubadilika.

Baada ya kuhamia ACT Wazalengo, Membe alitangaza kugombea kiti cha Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama hicho.

Uingereza sasa rasmi iko nje ya umoja wa Ulaya

$
0
0


Nchi ya Uingereza, imeanza ukurasa mpya wa kujitegemea kutoka umoja wa Ulaya, baada ya usiku wa kuamkia jana kukamilisha rasmi safari ya kujitoa kwenye umoja huo.

Uingereza, iliacha kufuata sheria za umoja wa Ulaya kuanzia saa sita usiku kuamkia Ijumaa, ambapo sasa itakuwa na sheria zake za kusafiri, biashara, uhamiaji na usalama.

Waziri mkuu wa Uingereza, Boris Johnson, amesema "uhuru uko mikononi mwao" na kuwa na uwezo wa "kufanya vitu tofauti na kwa namna bora", akisema mchakato wa muda mrefu wa kujitoa umekamilika.

Licha ya hatua hii, wanasiasa na watu waliopinga nchi hiyo kujitoa umoja wa Ulaya, wanasema hali itakuwa mbaya zaidi.

Waziri wa kwanza wa Uscotishi, Nicola Sturgeon, ambaye mara zote amekuwa akitaka nchi yake kubaki kwenye umoja wa Ulaya, amesema kupitia ukurasa wake wa kijamii wa twitter "Scotland itarejea karibuni kwenye umoja wa Ulaya, kuweni na imani".

Mawaziri wa Uingereza, wameonya kuhusu uwezekano wa kushuhudiwa sintofahamu katika baadhi ya mambo, wakati huu taifa hilo likitekeleza sheria zake tofauti na zile za umoja wa Ulaya.

 

-RFI


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumapili January 3

Ajali ya treni yaua na Kujeruhi Jijini Dodoma

$
0
0

Watu watatu wamefariki dunia na wengine zaidi ya thelathini wamejeruhiwa, baada ya treni waliyokuwa wakisafiria kutoka jijini Dar es salaam kuelekea mkoani Kigoma, kupata ajali katika eneo la Kigwa wilayani Bahi mkoani Dodoma.





Makamu Wa Rais Mhe. Samia Awafariji Majeruhi Wa Ajali Ya Treni Dodoma

$
0
0


Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan amewatembelea majeruhi wa ajali ya treni katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma ambapo ametoa maagizo kwa mkoa kuhakikisha wanasaidiwa kufika makwao mara watakapopata nafuu.

Samia alitoa kauli hiyo baada ya kuzunguka katika wodi zote walikolazwa majeruhi hao na kuzungumza nao lakini akasema ameridhishwa na hali zao pamoja na huduma wanayopata wagonjwa hao.

Kiongozi huyo amefika hospitali ya rufaa ya Mkoa wa Dodoma mapema saa moja asubuhi na mbali na kuzungumza na majeruhi wa treni lakini amezungumza na wagonjwa wengine akiwafariji.


 

Naibu Waziri Ummy Akemea Vitendo Vya Udhalilishaji Kwa Watu Wenye Ulemavu

$
0
0


Na: Mwandishi Wetu
Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Wenye Ulemavu Mhe. Ummy Nderiananga amekemea vikali vitendo vya udhalilishaji Watu wenye Ulemavu ikiwemo suala watu ambao wamekuwa wakitumia kundi hilo kujinufaisha.

Hayo yameelezwa wakati alipofanya ziara ya kushitukiza katika maeneo mbalimbali ambayo wanahifadhiwa Watu Wenye Ulemavu katika Mtaa wa Tandale, Jijini Dar es Salaam, Naibu Waziri alieleza kuwa kumekuwa na vitendo vya udhalilishaji wa watu wenye ulemavu ambavyo vimekuwa vikiendelea katika jamii na vitendo hivyo vinapelekea ukiukwaji kwa haki zao.

“Watu wenye Ulemavu wanahaki zao za msingi na ndio maana Serikali imekuwa ikuchukua hatua mbalimbali kuzuia vitendo vya udhalilishaji kwa kundi hilo na katika kulitambua hilo sheria mbalimbali zimekuwa zikitungwa lengo hasa ni kulinda maslahi na kuboresha maisha ya watu wenye ulemavu,” alisema Waziri Ummy

Alisema kuwa, wapo baadhi ya watu ambao ni kama mawakala “dealers” ambao wanawatoa watu wenye ulemavu katika mikoa mbalimbali na kuwaleta jijini Dar es Salaam kwa lengo la kuwafanya ombaomba mitaani.

“Inastahajabisha kuona mtu anawachukua watu wenye ulemavu na kuwakodisha viti mwendo “wheelchair” ili wakaombe mtaani huku kila siku anachukua fedha hizo kwa wenye ulemavu lengo ikiwa ni kujinufaisha kwa maslahi binafsi,” alisema Ummy

Mheshimiwa Ummy alieleza kuwa upo umuhimu wa kufanya utambuzi mapema wa mapema wa watu wanaofanya vitendo hivyo kwa kundi hilo ili kuzuia vitendo hivyo kuendelea katika jamii.

“Serikali itahakikisha ina shughulikia suala hili la udhalilishaji wa watu wenye ulemavu ili waweze kupata haki zao, sambamba na kuwalindwa na kufanya kundi hilo liheshimike katika jamii,” alieleza Naibu Waziri Ummy

Aidha, Mheshimiwa Ummy amewataka wananchi kutowaonea aibu wahusika wanaofanya vitendo hivyo badala yake wawe huru kutoa taarifa katika vyombo vya kisheria ili wachukuliwe hatua.

Sambamba na hayo, Naibu Waziri alitumia fursa hiyo kuwaelimisha watu wenye ulemavu juu ya fursa ya mikopo inayotolewa na serikali kupitia halmashauri (2% Watu wenye Ulemavu) ili waweze kuanzisha shughuli zitakazo wapatia kipato badaya ya kuombaomba mitaani.

Kwa Upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Mhe. Daniel Chongolo alikiri kupokea maelekezo yaliyotolewa na Naibu Waziri na alieleza kuwa tayari wameshachukua hatua kwa baadhi ya wahusika wanaojishughulisha na vitendo hivyo.

Naye, Bw. Steven Fotnatus alisema kuwa wapo tayari kuacha tabia ya kuombaomba mitaani maana wamegundua kuwa wamekuwa wakirubuniwa na baadhi ya watu ambao hawana nia njema nao.

Halmashauri Za Bagamoyo Na Mkuranga Mkoa Wa Pwani Zamkuna Naibu Waziri Mabula

$
0
0


 Na Munir Shemweta, WANMM PWANI
Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula amefurahishwa na kuzipongeza halmashauri za wilaya ya Mkuranga kwa kununua vifaa vya upimaji na Bagamoyo kwa kuandaa mpango Kabambe.


Akizungumza na watendaji wa sekta ya ardhi, viongozi wa mkoa wa pwani na wakurugenzi wa halmashauri za mkoa huo mwishoni mwa wiki, wakati wa ziara yake ya kukagua utendaji kazi wa sekta ya ardhi Dkt Mabula alisema uamuzi wa halmashauri kununua vifaa huku nyingine ikitenga fedha kwa ajili ya mpango kabambe ni kuonesha kuwa wakurugenzi wake wako makini kuhakikisha maeneo ya halmashauri hizo yanapangwa na kupimwa.


Akielezea uamuzi wa kununua vifaa vya upimaji katika halmashauri ya Mkuranga mkoa wa Pwani, Naibu Waziri Dkt Mabula alisema ni jukumu la halmashauri kuihudumia idara ya ardhi ili iweze kufanya kazi vizuri na kwa ufanisi.


Alisema, halmashauri ikinunua vifaa kwa ajili ya idara ya ardhi itaiwezesha idara hiyo kupima maeneo mengi na hivyo kuifanya kuwa na maeneo mengi yaliyopimwa na kupangwa na kuepukana na migogoro ya ardhi.


“”Ukiwa na kifaa chako cha upimaji cha RTK biashara yako ya upimaji katika halmashauri yako ni kazi rahisi sana na unaweza kupima wilaya yako na kuondokana na migogoro ya ardhi” alisema Dkt Mabula.


Aliitaka halmashauri ya Mkuranga kuhakikisha kifaa ilichokabidhiwa kinatumiwa badala ya kukihifadhi na kushauri kuwa pale halmashauri nyingine katika mkoa huo zenye uhitaji wa kukitumia zitakapohitaji ziazimwe ili kuongeza kasi ya upimaji katika mkoa wa Pwani.


Kwa upande wa halmashauri ya wilaya ya Bagamoyo, Naibu Waziri wa ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi aliipongeza halmashauri hiyo kwa uamuzi wake wa kutenga fedha shilingi milioni 230 kwa ajili ya kuandaliwa mpango Kabambe wa mji wa Bagamoyo.


Alisema, mbali na halmashauri hiyo kutenga kiasi hicho cha fedha kwa ajili ya ‘Master Plan’ lakini pia imeweza kufanya vizuri katika ukusanyaji mapato yatokanayo na kodi ya pango la ardhi ambapo hadi kufikia Desemba 2020 imeweza kufikia asilimia 54 ya makusanyo yake.


Viewing all 45270 articles
Browse latest View live
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>