Zikiwa zimesalia saa 24 kabla ya kumalizika kwa muda uliotolewa
na Rais Jakaya Kikwete kwa wahamiaji haramu kuondoka nchini au
kuhalalisha ukaazi wao na wenye silaha kuzisalimisha, makundi ya
wahamiaji hao, yameanza kuondoka kwa hiari.
Wastani wa wahamiaji haramu 150 wanaendelea
kujiandikisha kuvuka mpaka katika Kituo cha Rusumo, Ngara mkoani Kagera
kutekeleza agizo hilo.
↧