Watendaji wa Halmashauri waliokaa kwenye vituo vya kazi kwa zaidi ya miaka 10, wataanza kuhamishwa wakati wowote kuanzia sasa kuleta ufanisi katika utendaji na kukomesha kufanya kazi kwa mazoea.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda (pichani) ameagiza ofisi za mikoa ziainishe majina ya watendaji husika, utaratibu wa kuwahamisha ufanyike kunusuru utendaji wa kazi kwenye maeneo walikokaa muda mrefu.
↧