Basi la kampuni ya Sumry limetumbukia mtoni na kuua watu tisa na kujeruhi wengine hamsini na tatu.
Ajali hiyo imetokea katika kijiji cha Sitalike wilaya ya Mlele mkoani Katavi
Tukio
hilo la kusikitisha lilitokea saa sita usiku kuamkia Julai 5, 2013 basi
hilo lilipokuwa likitokea mjini Sumbawanga kuelekea Mpanda mkoani
Katavi likiwa na abiri waliokuwa wametoka Mbeya.
↧