MWANAFUNZI wa kidato cha pili mwenye umri wa miaka 15 anayedaiwa kubakwa na askari wa Jeshi la Polisi mkoani Shinyanga, usiku wa kuamkia Januari 6 mwaka huu, ametoweka katika mazingira ya kutatanisha.
Tukio la kubakwa mwanafunzi huyo (jina tunalo), aliyekuwa aingie kidato cha pili Sekondari ya Sakwe, iliyopo Bariadi, mkoani Simiyu, lilitokea eneo la Ndembezi, Manispaa ya Shinyanga.
↧