WANAJESHI wapatao wanane wanadaiwa kuwatesa na kuwapiga vijana watatu katika eneo la Ubungo Kibangu, Dar es Salaam pasipokuwa na sababu maalumu.
Wakizungumza na mwandishi wetu jana, vijana hao walieleza kuwa walikamatwa na wanajeshi hao na kupelekwa porini kisha wakateswa na kupigwa kwa zaidi ya saa tano bila kufahamu kosa lao na hata walipohoji waliambiwa hawaruhusiwi kuhoji wanajeshi.
↧