Idadi ya wagonjwa wa virusi vya corona nchini Kenya imeongezeka hadi 2,767 baada ya wagonjwa wengine 167 kupatikana na virusi hivyo kutoka sampuli 2,833 zilizofanyiwa vipimo.
Akitoa taarifa za kila siku kuhusu mwenendo wa ugonjwa huo Waziri wa Afya Mutahi Kagwe amesema kwamba wagonjwa hao wapya wanaume 125 na wanawake 42.
Bwana Kagwe amesema hatahivyo wagonjwa wengine 46 wamepona, hatua inayoongeza idadi ya wagonjwa waliopona kufikia 752.
Amesema kwamba mgonjwa mwingine mmoja amefariki kwa ugonjwa huo na kufanya idadi ya waliofariki kufikia 84.
Akitoa taarifa za kila siku kuhusu mwenendo wa ugonjwa huo Waziri wa Afya Mutahi Kagwe amesema kwamba wagonjwa hao wapya wanaume 125 na wanawake 42.
Bwana Kagwe amesema hatahivyo wagonjwa wengine 46 wamepona, hatua inayoongeza idadi ya wagonjwa waliopona kufikia 752.
Amesema kwamba mgonjwa mwingine mmoja amefariki kwa ugonjwa huo na kufanya idadi ya waliofariki kufikia 84.