MBUNGE wa Karagwe, Gosbert Blandes
(CCM), amehoji lini serikali itapitisha Kiswahili kitumike kuanzia Shule
za Msingi hadi Vyuo Vikuu. Aidha, alisema mwaka 2004, Umoja wa Afrika
ulipitisha Kiswahili kiwe ni lugha ambayo itatumika katika mikutano na
shughuli mbalimbali.
“Je, serikali imejiandaa vipi kupeleka wakalimani wa kutosha kutoka Tanzania ili waweze kujipatia ajira?” alihoji.
↧