Wakati raia tisa wa China wakibainika kuugua ugonjwa wa dengue
na kulazwa hapa nchini, Rais Jakaya Kikwete amevunja ukimya na kuagiza
wizara zake mbili kukabiliana na ugonjwa huo kwa dharura.
Ugonjwa huo uliingia nchini tangu mwaka 2010
lakini mlipuko wake mkubwa ulibainika Machi mwaka huu na hadi jana
wagonjwa zaidi ya 400 walikuwa wameambukizwa, huku watatu wakiripotiwa
kufariki
↧