Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji
Joseph Warioba amesema waliokuwa wajumbe wa tume hiyo hawajawahi kudai
malipo ya pensheni ya Sh200 milioni kama inavyodaiwa.
“Wajumbe wa Tume hawajatoa madai ya kulipwa
shilingi milioni mia mbili. Hakuna mjumbe yeyote aliyetoa dai kama hilo
na Serikali inajua,” alisema
Jaji Warioba katika taarifa yake kwa vyombo vya
↧