Shirikisho
la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) tunalaani vikali fujo na uhabirifu wa
mali unaofanywa na washabiki viwanjani wakati mechi mbalimbali zikiwemo
zile za kimataifa na ligi za hapa nchini.
Tunaiomba
radhi Serikali kwa uharibifu wa viti uliotokea kwenye mechi ya Ligi ya
Mabingwa Afrika kati ya Yanga ya Tanzania na Al Ahly ya Misri
iliyochezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
↧