Baadhi ya wachumi na wadau mbalimbali wa nishati ya umeme
wameikosoa hatua ya Shirika la Ugavi wa Umeme Tanzania (Tanesco) baada
ya kuongeza gharama za umeme kwa maelezo kuwa hatua hiyo itamkandamiza
mwananchi wa kawaida.
Kauli hizo zimekuja siku moja baada ya Mamlaka ya
Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) kutangaza bei mpya za
umeme huku kukiwa na ongezeko kubwa.
↧