TAKRIBAN wiki moja baada ya kumaliza eda tangu alipofariki mumewe
Juma Kilowoko ‘Sajuki’ Januari 2, mwaka huu, staa mkubwa wa filamu za
Kibongo, Wastara Juma anagombewa na midume ikitaka kumuoa.
Akizungumza na mwandishi wetu akiwa nchini Oman,
Wastara alifunguka kuwa tangu amalize eda yake hiyo amekuwa akipata
usumbufu mkubwa kutoka kwa wanaume mitandaoni na wanaomtamkia mwenyewe.
↧