Mfanyabiashara wa magari, Gabriel Munisi (35), jana alijiua
baada ya kumuua mtu mmoja na kujeruhi wengine watatu jijini Dar es
Salaam katika tukio linalohusishwa na wivu wa mapenzi.
Munisi, ambaye alikuwa mkazi wa Mwanza, aliwapiga
risasi watu watatu akiwamo mchumba wake, Christina Alfred katika Mtaa wa
Bungoni Wilaya ya Ilala, Dar es Salaam.
↧