Mtanzania Agnes Gerald, maarufu Masogange, ameachiwa huru na
Mahakama ya Kempton ya jijini Johannesburg, baada ya kulipa faini ya
R30,000 (Sh4.8 milioni) kwa kosa la kubeba kemikali zinazotumika
kutengeneza dawa za kulevya.
Wakati Masogange akitozwa faini hiyo mwenzake,
Melissa Edward ameachiwa huru na mahakama hiyo, baada ya kukosekana
ushahidi wa kumtia hatiani.
↧