Waziri wa Katiba na Sheria, Mathis Chikawe amesema Rais Jakaya
Kikwete hana mpango wa kuongeza muda wa uongozi wake baada ya 2015 kama
baadhi ya wanasiasa wanavyodai.
Kadhalika, waziri huyo amesema hakuna sheria
inayomlazimisha Rais kusaini muswada wa sheria yoyote inayopitishwa na
Bunge na wala inayoweka muda maalumu wa kutekeleza wajibu huo.
↧