Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Makamu wa Rais na Mkurugenzi Mkuu wa UNIDO wafanya mazungumzo kuhusu viwanda

$
0
0
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan jana amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Maendeleo ya Viwanda (UNIDO) Bw. Li Yong.

Katika mkutano huo ambao ulikuwa na lengo ya kujadiliana masuala mbalimbali ya uendelezaji Viwanda nchini Tanzania.

Mkurugenzi huyo amemjulisha Makamu wa Rais kuwa Tanzania ni nchi ya nne kuitembelea tangia ateuliwe .

Aidha katika mazungumzo hayo Mkurugenzi wa UNIDO amesema anajua Tanzania ajenda yao kuu ni uanzishwaji wa Viwanda na alimhakikishia Makamu wa Rais kwamba UNIDO itajitahidi kusaidia ajenda hiyo.

“Kuna umuhimu wa kuzingatia sekta binafsi na viwanda vidogo na vya kati wakati wa uanzishwaji viwanda ili vijana na wanawake wapate ajira,” alisema Mkurungenzi Mkuu wa UNIDO.

Mkurugenzi Mkuu wa UNIDO Bw. Li Yong amesema pia suala la uanzishwaji na Uendelezaji wa Viwanda  ni lazima lizingatie masuala ya upatikanaji wa nishati na mabadiliko ya tabia nchi.

Aidha Mkurugenzi huyo alisifia mabadiliko ya kiuchumi na kijamii yanayoendelea ndani ya Serikali ya awamu ya tano na kusema UNIDO suala muhimu ni Utekelezaji.

Pia aliupongeza uongozi wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania na mashirikiano mazuri na Serikali.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alimhakikishia Mkurungenzi huyo wa UNIDO ushirikiano wa hali ya juu kutoka Serikalini na alimuomba kuipa Tanzania kipaumbele  katika programu yake muhimu itakayochochea maendeleo ya Viwanda ya “Programmes For Country Partnership-PCP”.

Mwisho Kiongozi huyo aliishukuru Tanzania kwa mapokezi mazuri na programu nzuri walizompangia.

Viongozi wengine walioshiriki kwenye mazungumzo hayo ni Waziri wa Viwanda, Bishara na Uwekezaji Mhe. Charles Mwijage, Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Philip Mgango pamoja na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Augustine Mahiga ambapo pia Waziri wa Viwanda , Biashara na Uwekezaji alitia saini pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa UNIDO Bw. Li Yong 

Tamko la Kusudio la kuanzisha (Declaration of Intention) Mpango wa UNIDO unaojulikana kama “Programmes For Country Partnership-PCP”  ambapo Makamu wa Rais alishuhudia kusainiwa kwa Tamko hilo,kusainiwa kwa tamko hilo kutarahisisha mchakato wa  wa kukamilika kwa uwasilishwaji wa ombi la Tanzania kuomba iingizwe katika Mpango Maalumu wa UNIDO  ambao ni muhimu katika kuchochea maendeleo ya Viwanda.

Mrembo Aliyedaiwa Kuolewa na Alikiba Afungukia Tuhuma Hizo

$
0
0
Video vixen maarufu kutoka nchini Kenya anayejulikana kama Tanasha  Donna Barbieri Oketch ‘Zahara Zahire’ ambaye alionekana kwenye video ya wimbo wa Alikiba na Christian Bella ‘Nagharamia’ amekataa kuwa na uhusiano na Alikiba.

Kwa wiki sasa kumekuwa na taarifa zilizokuwa zinaenea mtandaoni ambazo zinadai kuwa supastaa huyo wa Bongo fleva Alikiba anatarajia kufunga ndoa hivi karibuni lakini tatizo likawa bibi harusi hajulikani ni nani.

Lakini mara moja habari zilianza kuenea kuwa mrembo ambaye anatarajiwa kuolewa na Alikiba ni mkenya anayeishi Moombasa na baadae kuja kusikika bibi harusi ni Tanasha.

Tanasha amejitokeza na kukataa kata kata taarifa hizo za kuolewa na Alikiba wala kuwa na uhusiano naye wa kimapenzi. Tanasha aliweka wazi ujumbe huo kwenye ukurasa wake wa SnapChat ambapo aliandika;

Kwenye ujumbe huo Tanasha ameelezea kuwa taarifa zinaoenea kwenye mitandao Tanzania kuwa ana uhusiano na Alikiba ni za uongo na uzushi na kudai aliwahi kutokea kwenye video yake moja tu ya wimbo wake lakini hawajawahi kuwa wapenzi.

Mbasha Amlalamikia Mzazi Mwenzie Kumnyima Mtoto.

$
0
0
Msanii wa muziki wa injili nchini Emmanuel Mbasha amefunguka katika ukurasa wake wa instagram kwa kumuandikia barua ndefu aliyekuwa mke wake wa ndoa Florah Mbasha kuhusu kumnyima mtoto wake wa kike waliezaa nae walipokuwa wakikaa wote miaka ya nyuma.

Emanuel Mbasha na Flora Mbasha walifunga ndoa kanisani na kuishi pamoja na hata kufanya kazi zao za muziki wa injili pamoja lakini walikuja kuachana na hata  kupelekana mahakamani kwa makosa ya kubaka ambapo baada ya upelelezi kukamilika ilikuja kuonekana kwamba Florah Mbasha alitunga kesi hiyo na kumsingizia  mume wake hivvyo Emanuel Mbasha alichukua jukumu la kumtaliki mwanamke huyo.

Lakini Emanuel Mbasha anaonekana kuumia kukaaa mbali na mtoto wake wa kike walimpata  na mzazi mwenzie huyo ambae alipewa mamlaka ya kukaa na mtoto huyo na mahakama kutokana na umri wa mtoto, Mbasha anasema kuwa pamoja na kwamba mahakama iliamuru mtoto kukaa na mama yake na yeye kuruhusiwa kumuona kwa muda tu lakini hata muda kidogo amekuwa akinyimwa na mzazi mwenzie huyo.

"Happy women’s day, ila ulinizalia mtoto mzuri mno nakushukuru sana,nimemmiss sana lizy unipage basi hata mtoto , unaninyima hata kumuona , karibia mwaka wa 2 unaelekea wa 3 sasa sijawahi kumuona mtoto daah mie babake tu ila naomba siku moja moja nifurahie maisha , aah nakuomba nimuone mwanangu lizy,najua hata mtoto amenimiss sana maana najua ameonoka kwangu akiwa mkubwa na nimemlea tamgu akiwa mtoto , atakuwa anshindwa tu kusema ila amenikumbuka sana.mahakama iliamua mtoto akae na mama ila niwe namuona mtoto ,sasa unapingana na mahakama…. sitaki povu hapa naongea na mzazi mwenzangu maana naona njia za kawaida zimeshinikana sasa inabidi nikuombe insta."

Mbasha anAsema kuwa ameamua kutuma ujumbe huo kwa Florah Mbasha ambae kwa sasa ameshaolewa na mwanaume mwingine kupitia instagram kwa sababu hakuna njia nyingine wanaweza kuwasiliana zaidi ya hiyo,

Mnara wa simu wajeruhi askari

$
0
0
JENGO la ofisi ya serikali ya mtaa katika eneo la Goba jijini Dar es Salaam ambalo hutumiwa na polisi, limeangukiwa na mnara wa simu kutokana na mvua iliyonyesha juzi usiku na kumjeruhi askari.
 
Mvua hiyo ambayo ilianza majira ya jioni ikiambatana na upepo mkali, ilisababishia mnara huo kuanguka na kumjeruhi askari ambaye alikuwa anatoa huduma kwa wananchi katika eneo hilo.
 
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Jumanne Murilo, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa eneo hilo linalotumika na askari sio jengo lao, bali ni mali ya ofisi ya serikali ya mtaa.
 
“Katika hilo eneo hatuna kituo cha polisi, ila polisi wetu wanakuwa wapo mobile kwa hiyo tukiwa kwenye majengo ya serikali ya mtaa tukiwa tunatoa huduma ina maana ni kituo cha polisi. Hivi kituo cha polisi kinakuwa na chumba kimoja ina maana ukipita sehemu ukaona polisi watatu hicho ni kituo cha polisi,” alihoji Kamanda Murilo.
 
Alifafanua kuwa wakati jengo hilo linaangukiwa na mnara kulikuwa na askari mmoja ambaye alikuwa anatoa huduma za kiusalama katika eneo la Goba na alipata majeraha kadhaa na hali yake inaendelea vizuri.
 
Alisema askari huyo alikwenda kupatiwa matibabu katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) na sasa yupo nyumbani akiendelea vizuri.

Mkuu wa Mkoa Alexander Mnyeti atengua agizo la Waziri Dr. Kigwangalla

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti ametengua agizo la Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk Hamisi Kigwangalla aliyewapa miezi tisa wananchi wa Kijiji cha Kimotorok kuondoka katika maeneo wanayoishi wakidaiwa kuvamia Hifadhi ya Tarangire wilayani Simanjiro.

Akizungumza na wanakijiji hao juzi, Mnyeti alisema hakuna atakayekwenda kuwafukuza na kama hilo lipo, yeye ndiye atawaambia wanafukuzwa au la, hivyo wawe na amani.

Mnyeti alisema ofisi ya mkoa inajiandaa kutuma wataalamu kwenda kupima eneo hilo ili kutatua mgogoro.

Februari 25, Waziri Kigwangalla aliwapa wananchi wa kijiji hicho, vitongoji vya Massas na Loon’benek miezi tisa wawe wamehama kwa kuwa wamevamia eneo la Hifadhi ya Tarangire.

Baadaye alitoa ufafanuzi akisema kabla ya kuondoka, Serikali itawalipa fidia na watatafutiwa maeneo mengine ikiwa ni pamoja na kujengewa zahanati nje ya hifadhi kutokana na iliyokuwapo kuwa ndani.

Dk Kigwangalla alipotafutwa jana kuzungumzia kauli ya Mnyeti alisema, “Sijapata taarifa rasmi kwa maandishi. Siwezi kufanyia kazi taarifa za kwenye mitandao. Nitasubiri barua kama itakuja. Hata hivyo, sina hakika kama mkuu wa mkoa anaweza kusema hivyo.”

Mkuu wa mkoa Mnyeti alitoa kauli baada ya msafara wake kusimamishwa na wananchi wa Kimotorok alipokuwa akienda kwenye mkutano wa kuwapokea wanachama zaidi ya 3,000 wa CCM kutoka vyama vingine.

Wananchi wa kijiji hicho walimuomba mkuu wa mkoa kuingilia kati suala hilo kwani watu wa hifadhi wanataka kuwapora ardhi yao bila hata kuwashirikisha katika jambo lolote wanalofanya, ikiwamo kuweka alama  ndani ya ardhi ya kijiji hicho ambacho kina hati miliki tangu mwaka 1970.

Akijibu hoja za wananchi, Mnyeti aliomba apewe siku 10 awe amefanya utaratibu wa kupeleka wataalamu kutoka Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambao wako katikati ya wananchi na hifadhi hivyo hawatapendelea upande wowote.

“Sasa chagueni kamati ndogo au Serikali ya kijiji watakaokwenda na wataalamu kukagua alama za mipaka. Watapitia mipaka yote kujua ramani maana hifadhi nayo ina umuhimu wake, hivyo muwe tayari kukubaliana na majibu yatakayosomwa na mtaalamu baada ya ukaguzi maana hata ofisi ya ardhi mkoa haijui utekelezaji wa uwekaji alama hizo,” alisema Mnyeti.

Alisema, “Lakini pia inawezekana mko sahihi maana tunajua hawa watu wa hifadhi mara nyingi wao wanataka kusogeza tu eneo, kila siku wanataka eneo liongezeke, leo anaweza akaja akaishia hapa kesho akija anaishia hapa, sasa tunaleta mtu ambaye yuko katikati ya hifadhi na wananchi na atapima kuleta ukweli.”

Trump akubali mualiko wa kukutana na Kim Jong Un

$
0
0
Rais Donald Trump wa Marekani amekubali ombi la Kiongozi wa Korea kaskazini Kim Jong Un la kutaka wakutane mapema ndani ya mwezi mei mwaka huu,na hivyo kuweka historia kufuatia  kutokuwepo rais wa Marekani ambaye amewahi kuonana na kiongozi mkuu wa Korea kaskazini.

Hata hivyo mahala watakapokutana viongozi panasalia kuwa siri kwa sasa,na pia Marekani imesisitiza kuwa pamoja na kukubali ombi hilo la rais Kim Jong Un lakini bado vikwazo vitasalia pale pale.

Tangazo hilo la kwamba rais Trump amekubali kukutana na Kim Jong Un,limetolewa na viongozi wa juu wa Korea Kusini uliofika mjini Washington kuwasilisha barua ya ombi hilo kutoka kwa Korea Kaskazini.

Kim pia amekubali kusitisha mpango wake wa nyuklia na majaribio yake ya makombora,msimamo ambao ni tofauti na aliokuwa nao rais huyo Kim Jong Un.

Hatua hii iliyofikiwa ya rais Kim Jong Un kulegeza msimamo ni matokeo ya mazungumzo mazito yaliyofanywa wiki chache zilizopita ujumbe wa Korea Kusini kukutana na kiongozi huyo.

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218 TUNAPATIKANA BUGURUNI SOKONI STENDI ya musanga

Tiba Asili ya Kuondoa Chunusi, Kupunguza Tumbo, Maziwa Makubwa na Nguvu za Kiume

$
0
0
Asilimia 90 ya wanaume hushindwa kufanya tendo la ndoa kikamilifu kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za kiafya  kama vile kisukari, punyeto ambayo huathiri mfumo mzima wa wa misuli inayozalisha vichocheo ashiki , kutopata choo vizuri hali ambayo huchakiwa na kula chakula kisicho na asili,tumbo kuunguruma, kujaa gesi,kiuno kuuma, mgongo na miguu kufa ganzi

SUPER HOLO; Ni dawa itokanayo na miti shamba, ipo katika mfumo wa vidonge na unga. Hutibu na kumaliza tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kwa muda mfupi tu.,SUPER HOLO hurudisha heshima ya ndoa, itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika 15-30. Itakupa hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3. Pia itaimarisha misuli iliyosinyaa na kulegea. Dawa hii hutumiwa kwa watu wa umrii wa miaka 20- 80

NZOGIWE ni dawaya maumbile.Hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo urefu wa nchi 4-8 na unene wa sentimita 2-4 za upenyo

NZOGOMA ni dawa asili ya miti shamba, huboresha mbegu za uzazi...huzibua mirija na kusafiisha ili kuweza kushika mimba au kutia mimba.

Pia tunayo dawa ya kupunguza tumbo, unene, maziwa makubwa, kuongeza hips, makalio na kutoa chunusi

TUNAPATIKANA MTONI MTONGANI. KANA HAUNA NAFASI YA KUFIKA UTALETEWA ULIPO. WASILIIANA NA DR. MBUSI.  PIGA SIMU NAMBA:   0718 431222

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 31 na 32 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA                    
ILIPOISHIA      
“Sawa mkuu”  
Daktari akaongoza njia, tukafika hadi kwenye chumba ambacho ndipo madkatari wote wanapotakiwa kufika kazini asubuhi wanasaini na pale wanapo toka wana saidi. Raisi akaanza kuligagua daftari hilo, nikaona akitingisha kichwa tu.
“Naombeni koti na mimi leo niwe daktari nikaaa humu kuangali jinsi wanavyo kuja, nyinyi nilindeni kwa nje”
“Sawa mkuu”
Raisi akapewa koti la kidaktari kisha sisi tukatoka nnje ya chumba hichi kuendelea kuimarisha ulinzi. Muda wa kufika ofisini kwa mfanyakazi wa serikali mwisho ni saa moja na nusu tena kwa wale wa mbali ila hadi inafika saa mbili asubuhi hakuna hata mmoja aliye fika, jambo lililo nifanya niwaze sijui ni kitu gani watakacho fanywa na raisi hawa madaktari.

ENDELEA
Tukaanza kuona makundi makundi ya madakatari wakija huku wakitembea kwa mwnedo wa taratibu wakipiga stori kama vile wanakwenda harusini. Hapakuwa NA Daktari aliye weza kustukia ni kitu gani ambacho kinaendelea kwa wakati huu. Hadi wanaingia ofisini humo, ndipo hapo wengine wakagundua kwamba vibarua vyao vipo hatiani kufutwa. Madaktari na manesi si chini ya thelathini wote wamekuja nje ya muda wa kufika ofisini kama mfanyakazi wa uma.
Kutokana na wingi wa wafanyakazi hao hatukucheza mbali na raisi, ambaye amewaitisha kikao cha dharura ndani ya ofisi hiyo hiyo japo wote wamesimama.

“Nasemea kuanzia sasa hivi ninavyo zungumza, kazi hamuna”
Sura za manesi na madaktari zikabadilika kila mmoja aliweza kuweka pozi lake, mwenye machozi kumlenga lenga, yalimlenga lenga. Mwenye machozi kumtoka yakamtoka.
“Nyinyi munakuja kazini kama hospitali hii ni ya baba zenu na mama zenu. Daktari mkuu hapa ni nani?”
Mzee mmoja mweusi na mfupi akanyoosha mkono wa kulia.
“Hii hospitali kila mwaka inapata ruzuku ya kiasi gani kutoka serikali kuu?”
“Bilioni tano mkuu”
“Bilioni tano hizo zinatumika katika kufanya nini?”
“Kupaka rangi majengo na…..naa…..naaaaa…..”
Daktari huyo akapatwa na kigugumizi kizito cha kujibu dhairi hawa wanaonekana ndio walaji wa pesa za serikali.
“Hembu huyu muwekeni ndani akajibu hili swala takukuru”
Mlinzi aliyekuja na raisi akamtoa daktari huyo na kumpeleka kwneye magari tulio kuja nayo. Raisi akatoa simu yake na kupiga namba anazo zijua yeye.

TANGA RAHA- Sehemu ya Ishirini na Tano ( 25 )

$
0
0
AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

Galfa hali ya hewa ikaanza kubadilika mbela ya madhabahu na upepo mkali ukatawala na radi vikaanza kutawalia kila pande ya madhabahu ila watu walio kuwepo wakabaki wakiwa wamesimama huku mikono yao wameinyoosha mbele kana kwamba wanapokea kitu kutoka juu.Mwanga mkali ukatoka kwenye sehemu ya madhabahu yao na gafla wakatokea watu wawili walio valia nguo nyeupa na mmoja akiwa ni mwanaume na mwingine akiwa ni Olvia Hitler na kunifanaya mwili mzima kunyong’onyea na kuishiwa nguvu kabisa

ENDELEA
    Olvia Hitler akasimama katikati ya mchungaji na muumini mwengine na akawawekea mikono kichwani mwao na kuanza kuzungumza maneno ambayo sikuwa ninayeelewa na kusababisha hali ya hewa kuzidi kutisha ndani ya kanisa lao la siri ambalo kusema kweli linatisha kupita maelezo.Upepo mkali mithili ya kimbunga ukaanza kuzunguka kwa kasi ndani ya kanisa huku kikiwa kama kinachungunza kitu fulani ndani ya chumba

“Eddy tuondoke ule upepo ni jini linaanalia usalama”
Tukaanza kutambaa chini mimi na Yudia na kabla hatujaufikia mlango tulio ingilia tukastukia watu wawili walio valia nguo nyeusi zilizo wafunika hadi vichwa vyao wakasimama mbele yetu.Yudia akasimama na kuwasukuma huku na yeye akiwa anazungumza manena ya ajabu kawa wafanyavyo watu waliomo ndani ya kanisa lao na kuwafanya watu hao kuangukia pembeni kisha na mimi nikanyanyuka na tukaanza kukimbia kuelekea kwenye mlango mwengine ambao ni tofauti n mlango tulio ingilia.Katika mlango tulio ingili tukakuta vipande vya miti vilivyo fungwa tambaa lenye mafuta ya taa vikiwaka huku vikiwa vimechomekwa kwenye  sehemu za ukuta wa sehemu hii na kuufaanya mwanga wake kuwa hafifu tofauti namwanga wa taa,Yudia akachomoa kimoja na kutangulia mbele huku akiniomba nimfwate

Tukaendelea kutembea kwa mwendo wa haraka huku kila wakati nikiwa nitazama nyuma kuangalia kama kuna watu wanao tufwata ila sikuona,Tukaendelea kwenda mbele urefu kidogo nikaanza kusikia kelele za watu wakilia na wasiwasi wangu ukaanza kunitawala
“Eddy usiogope hao ni miongoni mwa watu wanao sadikika kuwa duniani wamekufa ila wapo huku wamehifadhiwa na kila ifikapo mwisho wa wiki wawili huwa hutolewa sadaka ya kuteketeza”

Rais Magufuli Atoa Neno Kuhusu Kuhusu maandamano

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Pombe Magufuli amefunguka na kuzungumzia suala la maandamano na kusema atashughulika na watu ambao wataandamana ili wakawasilimulie wale watu ambao wamewatuma.

Rais Magufuli amesema hayo leo Machi 9, 2018  wakati akizindua tawi la benki ya CRDB Chato na kusema kuwa wapo watu ambao wanataka kuona amani ya nchi hii inavurugika jambo ambalo yeye hawezi kukubali kwa kuwa alihapa kulinda Katiba ya nchi.

"Wapo watu wameshindwa kufanya siasa za kweli wangependa kila siku tuwe barabarani tunaandamana, watu wao wanahamia huku wao wanataka wabaki wanaandamana kule 

"Nimeshasema ngoja waandamane wataniona, kama kuna baba zao wanawatuma basi watakwenda kuwasilimulia vizuri, niliapa kwa Katiba kwamba nchi hii lazima iwe ya amani na tunataka tujenge uchumi wa kweli ili Watanzania watajirike na hali ya Watanzania imeanza kwenda vizuri 

"Mwanzo ni mgumu lakini nataka niwaambie watanzania tupo kwenye wakati mzuri tuvumiliane ili tufike sehemu Tanzania iwe nchi ya asali" alisema Magufuli.

Rais Kenyatta na Odinga wakutana....waapa kufanya kazi pamoja

$
0
0
Kwa mara ya kwanza baada ya Uchaguzi Mkuu nchini Kenya uliofanyika October 2017, na kuleta mkanganyiko mkubwa wa kisiasa nchini humo, Rais Uhuru Kenyatta na Kiongozi wa Upinzani wa NASA Raila Odinga leo March 9, 2018 wamekutana rasmi na kuzungumza.

Viongozi hao wamekutana na kuzungumza kuhusu kuacha tofauti zao za kisiasa na kutanguliza maslahi ya wananchi wa nchi hiyo kwanza kwa kufanya kazi pamoja kurudisha amani.

“Maisha yetu ya baadaye hayawezi kupimwa kwa Uchaguzi Mkuu unaofuata bali utulifu wa nchi yetu na hali nzuri ya watu wetu, demokrasia ni mchakato ambao, hiari ya watu inasikilizwa lakini maslahi ya taifa lazima yatawale.” – Uhuru Kenyatta

Kwa upande wake Raila Odinga ameeleza kuwa “tukiendelea kuwa wabinafsi na waharibifu, hakuna kiwango chochote cha mageuzi ya kitaasisi ambacho kitaboresha maisha yetu.”

Inaelezwa kuwa wawili hao wamekubaliana kushirikiana katika agenda 9 mahususi, na ipo kamati iliyoundwa itakayo husisha wajumbe wa pande zote mbili ili kuanzisha programu ya kuwaunganisha tena wananchi ambao walitengwa na milengo ya kisiasa katika kipindi cha uchaguzi.

Rais Magufuli Aahidi kumpa Kazi Dr Kimei wa CRDB

$
0
0
Rais John Magufuli amesema licha ya kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa CRDB, Dk Charles Kimei anakaribia kustaafu ameahidi kumpatia nafasi katika Serikali ya Awamu ya Tano.

Rais Magufuli ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Machi 9, 2018 wakati akizindua tawi la benki hiyo wilayani Chato mkoani Geita.

“Kimei wewe ustaafu tu lakini nasema nafasi bado zipo. Muda wako unamalizika CRDB lakini Serikalini bado unaweza kufanya kazi ndani ya Serikali bado upo na ninakuahidi asilimia 100,” amesema Rais Magufuli.

Mwigulu Nchemba: Hakuna Tishio Lolote la Watu Kutekwa au Kuuawa

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwigulu Nchemba amefunguka na kusema Tanzania hakuna tishio lolote kuhusu watu kupotea au kuuawa kama inavyoelezwa na baadhi ya watu na kusema kuwa Wizara yake inapambana kuhakikisha watu na mali zao wako salama.

Waziri mwigulu Nchemba alisema hayo wakati akifanyiwa mahojiano na kudai kuwa miili ya watu ambayo imekuwa ikiokotwa baharini si miili ya Watanzania kwani kama ingekuwa miili ya Watanzania hivyo basi familia zao zingekuwa zinasikika kizipiga kelele kuhusu ndugu zao hao kupotea.

"Mimi kama Waziri wa Mambo ya Ndani nakuhakikishieni Watanzania kwamba Wizara inapambana kuhakikisha watu na mali zao wako salama na mpaka sasa hakuna tishio la namna hiyo kusema kwamba watu wanapotea hovyo hovyo au watu wanauawa hakuna kitu cha namna hiyo,

"Inatokea miili inaokotwa baharini bahari ambayo tunachangia na nchi nyingi sana na miili inaweza kusafiri kwa upepo kutoka sehemu nyingi sana lakini kuna watu wanasema watu wanauawa hovyo, haiwezekani watu wauawe hovyo halafu kukawa shwari tu familia zikawa zimetulia lazima familia zingepiga kelele" alisema Mwigulu Nchemba

Aidha Waziri Mwigulu Nchemba ametaka ajenda za watu zisigeuke kuwa siasa na kusema kuwa ajenda za siasa zifanywe kwenye siasa na si maisha ya watu pia Mwigulu Nchemba amedai kuwa katika matukio rasmi ambayo wao waliyapata ni kuhusu kutekwa kwa watoto Arusha.

"Utekwaji wa watoto ni jambo ambalo lilikuwa serious Watanzania wote waliona na wahalifu wakakamatwa ni bahati mbaya tu tulikuja kuwakamata na kuokoa mtoto mmoja yule lakini wengine wale walikuwa wameshawadhuru lakini tuliweza kuwakamata na kukamata ule mtandao ndiyo maana ile hali ilitulia na naendelea kuwataka Watanzania kuwa makini kwa sababu suala la usalama ni jambo ni endelevu" alisema Mwigulu Nchemba.

Mahakama yamuagiza AG kujibu kesi zinazohoji kukatazwa maandamano

$
0
0
Na Regina Mkonde
Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imemuagiza Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) kuleta majibu kuhusu mashauri mawili ya kikatiba yaliyofunguliwa mahakamani hapo na wanaharakati dhidi ya ofisi yake, ifikapo Machi 21 mwaka huu.

Mashauri hayo ni, shauri namba 4/2018 linalopinga sheria ya jeshi la polisi na ya vyama vya siasa zinazodaiwa kuzuia mikutano ya vyama vya siasa, na shauri namba 6/2018 linalopinga sheria ya uchaguzi inayowapa mamlaka Wakurugenzi wa Halmashauri nchini (maded) kuwa wasimamizi wa uchaguzi.

Hayo yamebainishwa leo mahakamani hapo na Mwanasheria upande wa walalamikaji, Wakili Jebra Kambole baada ya kuairishwa kutajwa kwa tarehe za kesi hizo kufuatia majaji wanaosikiliza kutokuwepo mahakani kwa sababu ya kuwa na dharula.

Vile vile, Wakili Kambole amesema mahakama imetaja tarehe 5 Aprili, 2018 kuwa siku ya kutajwa tarehe za kesi hizo.

“Mahakama imetoa amri mbili, kwanza imetaja  terehe 5 mwezi wa 4 haya mashauri yatakuja kutajwa tarehe, imetoa amri ya pili kwa mwanasheria mkuu wa serikali kwamba anapaswa kuleta majibu yake tarehe 21 mwezi wa 3, 2018 kwa hiyo hizo ni amri mbili zilizotolewa na mahakama siku ya leo. “

Amesema miongoni mwa walalamikaji katika shauri namba 4/2018 ni Baraka Mwago, wakati shauri namba 6/2018 mlalamikaji ni Bob Chacha Wangwe.

“Tulichokuja leo ni kuangalia namna gani mahakama itatoa amri ili watu mbalimbali waweze kutimiza wajibu wao, ni mashauri ya kikatiba yanapinga sheria mbalimbali ikiwemo sheria ya uchaguzi ambayo inafanya maded kuwa wasimamizi wa uchaguzi wakati inapaswa kuwa na tume huru ya uchaguzi, shauri namba nne inapinga sheria ya jeshi la polisi na sheria ya vyama vya siasa ambazo zinazuia mikutano ya vyama vya siasa na kuleta madharakwa wanachi. Tunapinga sheria hizo tunaona ni kandamizi zinakiuka katiba ikiwemo ibara ya 18 inayoruhusu uhuru wa kujieleza,” amesema na kuongeza.

“Inakiuka uhuru wa kufanya maamuzi juu ya maisha ya watanzania na maendeleo ya nchi yao, inakiuka haki ya kusikilizwa kwa watu ambao wakitaka kuandamana wanapata amri bila kusikilizwa, tunaangalia uhalali wa hizo sheria dhidi ya katiba ya nchi, kwa mujibu ibara ya 26 intoa jibu kwa mtu anayeona sheria yoyote iakiuka anawajibu wa kuleta shauri mahakamani, walalamikaji wametimiza wajibu wao kikatiba.”

Jeshi la Polisi Latoa ONYO Kali Kwa Waliopanga Kuandamana.......14 Watiwa mbaroni mauaji makada wa Chadema

$
0
0
KAMISHNA wa Operesheni wa Polisi (CP), Nsato Marijani amesema hadi sasa watuhumiwa waliokamatwa kudaiwa kuhusika na kifo cha Kada wa Chadema, Daniel John wamefikia wanne.

Pia amesema waliokamatwa katika tukio la kuuawa kwa kukatwa mapanga Diwani wa Kata ya Namwala Wilaya Kilombero, Geofrey Lwena wamefikia 10.

Amesema watuhumiwa wanaodaiwa kuandamana kinyume cha sheria na kusababisha kifo cha mwanafunzi wa Chuo cha taifa cha Usafirishaji (NIT), Akwilina Akwilini wamefikishwa mahakamani na uchunguzi unafanyika kwa aliyetenda.

CP Marijani ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam na kwamba upelelezi wa mauaji yote bado unaendelea.

"Kama tulishakamata watu wanne sisi tupo kwenye nafasi nzuri ya kusema nini kilikuwa sababu ya kifo hiki na nani waliokitenda, "amesema.

Amefafanua kuwa hawezi kuzungumzia zaidi kwani upelelezi unaendelea na kuwataka wananchi kuacha kusambaza taarifa ambazo hawana uhakika nazo.

Akizungumzia kifo cha Diwani Lwena, amesema wanataarifa zaidi za chanzo cha tukio hilo.

"Kadri upelelezi unavyoendelea tutajua wahusika wakina nani na tutawafikisha mahakamani,"amesema.Amesema vifo hivyo havihusiki na matukio ya kisiasa.

Akizungumzia maandamano, CP Marijani amesema jeshi la Polisi halitakubali kufanyika maandamano kwani ni kinyume cha sheria.

"Lolote linalofanyika katika nchi hii sisi kama jeshi la Polisi tunawaasa wananchi walifanye kwa mujibu wa sheria, suala la kufanya maandamano ukiwa na nia ya kuiondoa serikali ni uhaini, "amesema.

Amewataka wazazi na walezi wawaonye vijana wao kuwa vitendo wanavyokusudia kufanya ni uhaini na ni kinyume cha sheria.

"Ni dhahiri kwamba jeshi la Polisi haliwezi likakubali jambo hili litokee, tutafanya kila ambalo lipo kwenye uwezo wetu, kwa kadri tunavyoruhusiwa na sheria kuhakikisha kwamba jambo hili halifanyiki, "amesema na kuongeza;

"Sasa tusije baadae tukalaumiana, tumelisema hili wazi tunaamini kabisa watanzania waliokuwa wengi ni watu wazuri na wema wachache wasiotaka kufuata sheria na wanataka kuchezea usalama wa nchi hii basi sheria itachukua mkondo wake, "

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Rais Magufuli: Hii Vita ni Kubwa Sana, Watanzania Tuungane Pamoja

$
0
0
Rais Dkt. John Pombe Magufuli amesema suala la maendeleo linapigwa vita sana hivyo amewataka watanzania waunge mkono hatua mbalimbali zinazochukuliwa na serikali ili kuweza kuimarisha uchumi na utekelezaji wa miradi mikubwa ya maendeleo.

Dkt. Magufuli ametoa kauli hiyo leo (Machi 09, 2018) wakati alipokuwa anafanya ufunguzi wa benki ya CRDB tawi la Chato mkoani Geita.

"Niwaombe watanzania tutangulize uzalendo kwanza, mahali popote tulipo tujue hatuna baba wala mama hii ndio Tanzania yetu tukiichafua tumechafuka wote na maneno muda mwingine huwa yanaumba. Nchi yetu inakwenda vizuri sana na mtu yeyote ukifanya vizuri watu hawakupendi. Uzuri una gharama", amesema Dkt. Magufuli.

Pamoja na hayo, Dkt. Magufuli ameendelea kwa kusema "tunapoweza kujenga reli ya kisasa (Standard Gauge) kwa Trioni 7.6 hela za ndani usifikili watu wanafurahi, tunapoweza kuamua kujenga uzalishaji umeme katika maporomoko ya mto rufiji (Stieglers Gorge) tunapoweza kununua ndege 6 kitu ambacho tulikishindwa ndani ya miaka 50 usifikili wengine wanafurahi.

"Maendeleo yanachangamoto na vita kubwa ni lazima watanzania mjifunze na kuangalia mbele. Tumezungumza Tanzania ya viwanda ila zipo nchi zilizolalamika eti ni kwanini sisi tuwe na viwanda vya nguo kwa maana wanataka waendelee kutupa mitumba yao. 

Kwa upande mwingine, Rais Dkt.John Magufuli kesho (Machi 10, 2018) anatarajia kufanya ziara ya siku moja mkoani Shinyanga, kukagua na kuzindua baadhi ya miradi ya maendeleo ikiwemo barabara inayounganisha Tanzania na Rwanda inayoanzia katika eneo la bandari kavu ya Isaka wilayani Kahama hadi Rusahunga mkoani Kagera.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosii ya March 10

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images