AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA
“Wewe piga ila sipo tayari kufanya unachotaka kufanya”
“Mamaaa”
Yudia akapiga kelele na kunifanya nimzibe mdomo huku nikiwa ninamshangaa.Akaifungua zipu ya suruali yangu na kabla hajauingiza mkono kwenye suruali yangu tukasikia sauti ya mama yake ikimuita huku akija sehemu ya chumba hichi tulichopo na kunifanya nianze kutetemeka
ENDELEA
Wazo la haraka likanijia kichwani kwangu na nikalitekeleza kwa haraka ambalo nikaanguka chini na kunza kurusha rusha miguu kama mtu aliyepandwa na mapepo huku nikitoa makelele ya kunguruma na mikono yangu mara kwa mara nikiipeleka kwenye zipu yangu na kuifunga na kumfanya Yudia kusimama mlanoni kwa woga akimsubiria mama yake kuingia ndani ya chumba cha kusomea.Mama Mchungaji akaingi na baada ya kuniona nipo kwenye hali niliyo nayo ambayo kwangu ninaigiza ili kuua soo la kufumaniwa na mtoto wa mchumaji.
“Kalete biblia yangu ipo sebleni ya juu”
Yudia akatoka ndani ya chumba huku akinisogelea na kuniwekea mkono kichwa ni na akaanza kuniombea kimya kimya wala sikujua kama anaomba,Nikajikuta nikianza kutulia taratibu huku macho yangu yakiwa yametua kifuani mwa mama mchungaji kwani ukubwa wa maziwa yake yenye rangi nzuri ya kuvutia yakanifanya mawazo yangu kuanza kufikiria vitu vya ajabua ajabu.Yudia akafungua mlango na kuja hadi sehemu tuliyopo
“Hiyo biblia ipo wapi?”
“Sijaiona”
“Nimeiweka kwenye meza ya computer fanta haraka hali ya mwenzanu inakuwa mbaya”
“Sasa mama si umuamshe baba?”
“Baba yako yupo kwenye maombi binafsi hembu fanya haraka kailete biblia hembu fanya haraka”
Yudia akaondoka na kumuacha mama yake akiendelea kukemea mapepo ambayo sikuwa nayo japo nimekubwa na vituko visvyo kuwa na kichwa wala miguu ila ninajielewa mimi mwenyewe,Nikaona nisimpotezee m mama wa watu muda nikasimama na kukaa kitako na kujifanya mapepo yamenitoka
“Unajisikiaje Eddy?”
“Salama tuu”
“Ohhhh thak’s Loard”(Ohhhh asante bwana)
Mama mchungaji alizungumza huku akijifunga tenge lake vizuri na mimi nikanyanyuka na kukaa kwenye kiti
“Tukuletee kitu cha kula?”
“Haoana ninajisikia vizuri tuu”
“Mama nimeiona”
Yudia alizungumza huku akiingia ndani ya chumba tulichopo na akajikuta akiwa ameishika biblia huku akitushangaa kwa maana alihisi atanikuta nikiwa ninarusha rusha miguu kama mara ya kwanza
“Ameshapona?”
“Ndio amesha pona lete hiyo biblia nimpe mistari ya kusoma ili akajisome chumbani kweke”
Yudia akampa mama yake biblia na akaanza kunisomea mistaria ambayo nitwakenda kusoma chumbani kwangu.Nikaikariri na nikaagana nao na kuondoka ndani ya chumba na moja kwa moja nikaingia katika chumba ambacho Joseph alinionyesha.Nikapanda kitandani huku nikijichekea kimoyo moyo kwa kitendo nilicho kifanya
“Hii ya leo kali kumbe na mimi ninaweza kuigiza inanibidi niingie bongo movie”
Nilikisemea kimoyo moyo huku nikilirudia tendo nililokuwa nimelifanya na kujikuta nikicheka kwa sauti ya chini.Nikasimama na kuvua nguo zangu na kuingia bafuni na kufungulia maji ya bomba la mvua na kuanza kuoga huku nikipiga mluzi usio eleweka ni wa nyimbo gani.Nikastuka baada ya kuusikia mlango wa kuingilia chumbani kwangu ukifumguliwa kutonana na mapovu niliyokuwa nayo usoni nikanawa uso wangu haraka haraka kwa kutumia maji masafi na kujifunga taulo na kuchungulia na kuukuta mlango ukiwa umefungwa kama nilivyo ufunga
“Mmm labda sijausikia vizuri itakuwa ni hii miluzi yangu ya kijinga”
Niliijifariji na kutudi tena bafuni na safari hii nikaoga haraka haraka na kutoka na kupanda kitandani na nikakumbuka mistari aliyo ambiwa na mama mchungaji na uzuri zaidi biblia ipo sehemu ya wazi ambayo nikaichukua na kuifungua na kujikuta nikistuka baada ya kuto kuikuta na anadihi hata moja.Nikairudisha mezani huku mapigo ya moyo yakianza kuniienda mbio huku nikianza kupata na wasiwasi
“Isije kuwa Olvia amekuja huku kwa mchungaji?”
Nilijiuliza maswali ambayo hayana majibu ya uhakika,nikachukua shuka nikajifunika gubigubi kuanzia miguuni hadi kichwani kwa lengo la kutokuona kitu cha aina yoyote kitakacho endelea ndani ya chumba nilichopo.Usingizi ulianza kunichukua taratibu na gafla chumba nilicho lala kikaanza kutwaliwa na makelele ya watu wakilia huku wengine wakicheka,nikanyanyuka huku nikiwa nimeyaziba masikio yangu nisiendelee kuyasikia makelel yanayoendelea.Nikaanza kupiga hatua za kwenda mlangoni ila nikastukia nikamuona mdogo wangu ambeye alifariki tukiwa wadogo akisimama mlangoni huku macho yeke yakiwa yanatokwa na damu huku mikono yeke akiwa ameinyooshea kwangu