Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Billnass Ampokonya Young Dee ROSA REE...Tazama VIDEO Walichofanya Live

$
0
0
Billnass Ampokonya Young Dee ROSA REE...Tazama VIDEO Walichofanya Live

Tazama VIDEO Hapa Chini:

Makonda aagiza mwanafunzi aliyepotea ashughulikiwe

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amelitaka jeshi la polisi kuendelea kufanya kazi bila kutetereshwa na mtu yeyote na amemuagiza Kamanda Mambosasa na timu yake kuwashughulikia watu wanaotumia lugha za kashfa dhidi ya viongozi wa nchi ambao ni nembo ya taifa.

Pia amewaomba waandishi wa habari kuangalia taarifa wanazozisambaza kwa umma kuhakikisha kuwa ni taarifa ambazo zimethibitishwa na mamlaka husika kwani taarifa nyingi zinazosambazwa zimekuwa zikileta taharuki katika umma.

Hayo ameyasema kufuatia habari zilizosambaa hivi karibuni kuhusu Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi nchini Tanzania ambaye ni Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es salaam, Abdul Nondo ambaye alipotea siku chache zilizopita na kupatikana akiwa Mafinga.

Amesema kuwa kitendo cha waandishi wa habari kuandika habari ambazo hazijathibitishwa na mamlaka husika huchafua mkoa wa Dar Es Salaam na hivyo ameagiza kijana huyo ashughulikiwe.

”Juzi nimesikia kuna mmoja amesema ametekwa, mi nafikiri wakimalizana nae kule Iringa watuletee huku Dar es salaam, asituchafulie mkoa wetu” amesema Makonda.

Aidha ameomba Mamlaka ya Mawasiliano TCRA, kushughulikia makosa ya kimtandao ili kuhakikisha nchi yetu inabaki katika amani na utulivu,.

Mmiliki wa Mabasi ya Super Sami Atoweka Siku 14.....Gari Lake Lakutwa Mbungani Limechomwa Moto

$
0
0
Mmiliki wa mabasi ya Super Sami, Samson Josiah, ametoweka kwa zaidi ya wiki moja sasa na gari lake aina ya Toyota Landcruizer kukutwa likiwa limechomwa moto katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoani Mara.

Gari hilo lililokuwa likitumiwa na mfanyabishara huyo ambaye ni mkazi wa Mwanza, lilikutwa katika Hifadhi ya Taifa ya Serengeti mkoani Mara jana likiwa limeteketea kwa moto.

Ofisa Habari wa Chama cha Wamiliki wa Mabasi (Taboa), Mustapher Mwalongo, amesema  kuwa mfanyabishara huyo licha ya gari lake kukutwa limeteketea kwa moto, hawakukuta mabaki ya mwili wake.

"Gari lake limeteketea kweli lakini hatujabaini kama na yeye alikuwa kwenye gari lile kwa sababu waliofika eneo la tukio hawajakuta mwili au mabaki ya aina yoyote," alisema Mwalongo.

Alisema baada ya mmiliki huyo wa mabasi kutoweka tangu Machi mosi, kamati iliundwa ya kufuatilia sababu za kutoweka kwake na wapi alipo ambayo inashirikiana na familia.

"Kamati ilipopata taarifa kuwa kuna gari limeteketea kule Serengeti, walishirikiana na Jeshi la Polisi kwenda hadi eneo la tukio na kubaini kweli ni lake lakini ndani hawajabaini kama alikuwemo mle wakati linachomwa," alisema Mwalongo.

Alisema Jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi huku kamati hiyo ikiendelea na jitihada mbalimbali za kumsaka na kwamba hakuna uthibitisho wa aina yoyote ya kuwa amefariki dunia akiwa ndani ya gari lililoungua.

"Hakuna taarifa rasmi za mfanyabishara huyo kufa licha ya baadhi ya mitandao ya kijamii kuandika kuwa amefariki dunia. Hakuna mwili uliokutwa katika eneo lile," alisema.

Alisema wawakilishi wa Taboa mkoani Mwanza wanafuatilia kwa karibu na kuwapa kila taarifa wanayoipata kuhusiana na tukio hilo.

Pia alisema hadi jana jioni kamati hiyo kwa kushiriana na askari wa wanyamapori walikuwa wanaendelea kumsaka mfanyabishara huyo katika hifadhi hiyo.

Kuhusu kutoweka kwake, Mwalongo alisema mara ya mwisho walikutana kwenye kikao cha kamati ndogo ya Taboa mkoani Mwanza Februari 26, mwaka huu.

Alisema kuanzia Machi mosi zilianza kuzuka taarifa za kutopatikana kupitia simu zake za mkononi hadi nyumbani kwake.

Mabasi ya Kampuni ya Super Sami yanafanya safari zake kati ya Mwanza na mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma, Iringa na Kagera.

Taarifa ya Tanesco kuhusu kukatika kwa umeme kwenye gridi ya Taifa

$
0
0
Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limetoa taarifa kwa umma kuhusu kukatika kwa umeme usiku wa kuamkia Jumamosi ya Machi 10 katika mikoa iliyounganishwa kwenye gridi ya Taifa.

Taararifa ya Tanesco imeeleza kuwa majira ya saa 8:49 usiku kumetokea hitilafu katika mfumo wa gridi ya Taifa iliyopelekea kukosekana kwa huduma ya umeme katika maeneo na mikoa yote iliyoungwa kwenye gridi ya Taifa.

Baada ya hitilafu hiyo kutokea, mafundi na wataalamu wa shirika hilo walichukua hatua za haraka na bado wako kazini kuhakikisha kuwa huduma ya umeme inarejea mapema kadri iwezekanavyo.

Uongozi wa shirika hilo umeomba radhi kwa usumbufu uliojitokeza lakini ukitoa tahadhari kwa wananchi kuwa wasishike wala kukanyaga ulioanguka au uliokatika ili kuepusha madhara zaidi.

Takukuru yamfikisha mahakamani meneja Machinga Complex

$
0
0
Taasisi ya Kuzuia  na Kupambana na Rushwa (Takukuru) imemfikisha katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala, meneja wa soko la wafanyabiashara wadogo la Machinga Complex lililoko jijini Dar es Salaam, Nyamsukura Masondore, kwa tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka.

Akimsomea hati ya mashtaka inayomkabili mshtakiwa huyo jana  Ijumaa Machi 9, 2018, kwa Hakimu Mkazi Adelf Sachore, Mwendesha Mashtaka wa Takukuru, Sophia Gura alidai mshtakiwa huyo alitenda kosa hilo tarehe tofauti kati ya Septemba 29 na Oktoba 7, 2014 akiwa mwajiriwa wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kama meneja wa jengo la biashara la Machinga Complex.

Sophia alidai kuwa Masondore akiwa na jukumu la kuongoza shughuli za kila siku za jengo hilo, kwa makusudi alitumia vibaya madaraka yake kwa kutoa eneo ambalo halijaidhinishwa kwenye jengo hilo kwa Umoja wa Wauza Mitumba.

Imedaiwa kufanya kwake hivyo ni kinyume na kanuni namba 12(a) na (b) za Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam( Bodi ya Huduma ya Jengo hilo) na kwamba  kutokana na kitendo hicho mshtakiwa huyo alijipatia faida yeye pamoja na wengine.

Baada ya kusomewa shtaka hilo mshtakiwa huyo alikana na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi wake bado haujakamilika.

Hata hivyo, wakili anayemtetea, Jamhuri Johnson ameiomba mahakama impatie dhamana mteja wake huyo na upande wa mashtaka haukuwa na pingamizi.

Hakimu Sachore alitoa masharti ya dhamana akimtaka Masondore kuwa na wadhamini wawili wenye barua na vitambulisho kutoka taasisi zinazotambulika kisheria na  pia watasaini ahadi ya Sh 5 milioni. Na kwamba barua hizo zitahakikiwa.

Kesi imeahirishwa  hadi Machi 20, 2018 kwa ajili ya kutajwa ili kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika ama la.

Afisa TRA apandishwa kizimbani

$
0
0

Ofisa Msaidizi wa Kodi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Joyce Amon amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala akikabiliwa na shtaka la kushawishi rushwa.

Wakili wa Serikali, Sophia Nyanda alisema jana  Ijumaa Machi 9, 2018  mbele ya Hakimu Mkazi  Adelf Sachore kuwa  Desemba 12, 2017  katika eneo la Gerezani Kariakoo Wilaya ya Ilala mshtakiwa huyo akiwa mwajiriwa wa TRA kama Ofisa Msaidizi wa Kodi alishawishi rushwa ya Sh800,000 kutoka kwa Antelo Sanga ili asiweze kumwandikia cheti cha faini cha  Kodi  ya Ongezeko la Thamani  (VAT).

Katika shtaka la pili, mwanafunzi  Lilian  Wilson (23) naye anakabiliwa na shtaka la kusaidia kutenda kosa hilo.

Wakili Nyanda alidai Desemba 13,2017 katika Hoteli ya Tansome mshtakiwa huyo Lilian alimsaidia  Joyce ambaye ni Ofisa Msaidizi wa Kodi wa TRA  kujipatia   Sh400,000 kutoka kwa Antelo Sanga  ili asiweze  kumpatia cheti cha faini cha VAT.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo washtakiwa walikana na upande wa mashtaka ulidai kuwa upelelezi bado haujakamilika.

Hakimu Sachore  alimtaka kila mshtakiwa kuwa na wadhamini wawili wenye barua kutoka katika taasisi zinazotambulika kisheria  ambao watasaini ahadi ya Sh5 milioni kwa kila mmoja. Na kwamba barua hizo zitahakikiwa.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Machi 20, 2018 kwa ajili ya kutajwa ili kuangalia kama upelelezi utakuwa umekamilika au la.

Jipatie Tiba ya Asili ya Ngiri, Vidonda vya Tumbo,Kisukari na Nguvu za Kiume

$
0
0
Super nzoka IKEMEKO TRDITONAL clinic Ni dawa ya Asili ya vidonge iliyotengenezwa kwa techknojia ya kisasa na ubora wa hali ya juu 

Huongeza nguvu za kiume maradufu hata kwa wale wasiojiweza kabisa kufanya tendo la ndoa na wapo abao hata wakifanya hushindwa kutoa maji maji maji ambayo ndani yake kuna mbegu za kiume zinazotakitakiwa kurutubisha yai

Dawa hii huboresha na tunatibu nakumaliza matatizo haya kwa muda mfupi tu na haina madhara kwa mtumiaji yeyote hata wa umri wa miaka 80 na kuendelea.... inaongeza hamu, urijali kwa wanaoshindwa kuendelea na tendo la ndoa.

Huanza kufanya kazi baada ya dakika 60 tu na kufanya uchelewe kufika kileleni dakika 20 kwa tendo la kwanza itakuwa unauhakika wa kurudia tendo la ndoa zaidi ya Mara tatu bila kuhisi kuchoka 

SILYA; inakuza uume uliosinyaa kurefusha umbile dogo urefu inchi (6-9)na unene wa cm 4 za upenyo kwa wenye kasoro za kimaumbile na walioathiriwa na kupiga punyeto pamoja na matatizo ya kiafya

Tiba hii ni ya kudumu.Pia tunatibu ngiri ya kupanda na kushuka,tumbo kuuguruma chini ya kitovu ,kaswende kisukari ,maumivu ya mgongo, kiuno, kutopata choo vizuri na uvimbe kupitia njia ya mkojo, presha, vidonda vya tumbo

Wasiliana Nasi kwa namba;  0716343218 TUNAPATIKANA BUGURUNI SOKONI STENDI ya musanga

Tiba Asili ya Kuondoa Chunusi, Kupunguza Tumbo, Maziwa Makubwa na Nguvu za Kiume

$
0
0
Asilimia 90 ya wanaume hushindwa kufanya tendo la ndoa kikamilifu kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za kiafya  kama vile kisukari, punyeto ambayo huathiri mfumo mzima wa wa misuli inayozalisha vichocheo ashiki , kutopata choo vizuri hali ambayo huchakiwa na kula chakula kisicho na asili,tumbo kuunguruma, kujaa gesi,kiuno kuuma, mgongo na miguu kufa ganzi

SUPER HOLO; Ni dawa itokanayo na miti shamba, ipo katika mfumo wa vidonge na unga. Hutibu na kumaliza tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kwa muda mfupi tu.,SUPER HOLO hurudisha heshima ya ndoa, itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika 15-30. Itakupa hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3. Pia itaimarisha misuli iliyosinyaa na kulegea. Dawa hii hutumiwa kwa watu wa umrii wa miaka 20- 80

NZOGIWE ni dawaya maumbile.Hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo urefu wa nchi 4-8 na unene wa sentimita 2-4 za upenyo

NZOGOMA ni dawa asili ya miti shamba, huboresha mbegu za uzazi...huzibua mirija na kusafiisha ili kuweza kushika mimba au kutia mimba.

Pia tunayo dawa ya kupunguza tumbo, unene, maziwa makubwa, kuongeza hips, makalio na kutoa chunusi

TUNAPATIKANA MTONI MTONGANI. KANA HAUNA NAFASI YA KUFIKA UTALETEWA ULIPO. WASILIIANA NA DR. MBUSI.  PIGA SIMU NAMBA:   0718 431222

Makonda ONYO Atoa Onyo Waliopanga Kuandamana

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amefunguka na kusema watu wanaojifanya kutaka kuandamana wataweza kufanya hivyo kipindi ambacho yeye hatakuwa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam au hakiwa ameondoka ila vinginevyo hawawezi kuthubutu kuandamana.

Makonda amesema hayo akiwa anahotubia kwenye moja ya mkutano uliofanyika Dar es Salaam na kusema kuwa watu wengine ambao wanapiga sana kelele kuhusu maandamano hayo na kutaka kuvuruga amani ya nchi ndiyo wanapata fedha nyingi kutoka wa wafadhili wao ambao hawataki Mkoa wa Dar es Salaam ubaki salama.

"Kuna kakundi hapa kanahangaika kweli usiku na mchana wengine wanahangaika kutumia mitandao ya kijamii kutukana viongozi, kuhamasisha sijui wanaita nini sijui maandamano nawapa pole sana, watafanya labda mimi nikiondoka nikiwa siyo Mkuu wa Mkoa .....kwenye huu Mkoa hiyo mipango mipango yao watafanya labda mimi nikiwa sipo lakini amani ya mkoa wa Dar es Salaam ni muhimu sana" alisemana kuongeza;

"Amani ni muhimu sana kuliko propaganda za kisiasa na niwaambieni tu wengine wakipiga kelele na kutokea kwenye 'front page' kwenye magazeti ndiyo wanapata mshahara zaidi, wanapata donor kutoka kwenye baadhi ya mataifa yasiyotakia amani taifa letu kwa hiyo lazima tujue tunaye adui tunayeishi naye kama Mtanzania lakini amebeba majukumu ya mataifa yasiyoitakia amani taifa letu" alisisitiza Makonda

Rais Magufuli Azungumzia Ushukuru kwa Wafanyabiashara Wadogo

$
0
0
Rais John Magufuli amesema ushuru ni ugonjwa ambao umeendelea kuwa kero kwa wafanyabiashara ndogondogo nchini.

"Ushuru ni ugonjwa , kila sehemu ushuru, ushuru , wabunge wenu wameshapitisha sheria. Mtu akiwa na chini ya tani moja ya mzigo asitozwe ushuru. Kwenye minada kulikuwa hata na ushuru wa kwato za ng'ombe, hivi unaweza kulizuia ling'ombe lisiwe na kwato?, “ amehoji Rais Magufuli.

Ametoa kauli hiyo leo Machi 10, 2018 wakati wa uzinduzi wa barabara ya kilometa 45 kutoka Uyovu hadi Bwanga wilayani Bukombe, mkoani Geita iliyojengwa kwa kiwango cha lami.

Barabara hiyo ilikamilika ujenzi wake Oktoba, 2017 na imejengwa kwa fedha za ndani kwa ajili ya asilimia 100.

Huku akizungumza mara kwa mara Kisukumu na kuwafanya wananchi waliohudhuria uzinduzi huo wa barabara kuangua kicheko, Magufuli pia alikemea kundi la watu aliodai kuwa hawapendezwi na kasi ya mafanikio katika sekta mbalimbali.

"Kuna watu hawapendi kuona amani hii tuliyonayo. Dhana halisi ya kutunza amani, amani ni kitu muhimu, hata mitume walihubiri amani, Yesu aliwaambia nawaachieni amani, kwa hiyo nawaambia amani tuliyonayo imejengwa na Mwalimu (Julius Nyerere), amekuja Mwinyi (Ali Hassan) na akaja KIkwete (Jakaya) pia ameitunza amani,” amesema.

"Tuwazuie dhahabu, tutengeneze reli kutoka Dar ,Dodoma, mpaka Lusumo na iwe ya umeme, nani anafurahi? Nani afurahi kuona barabara za lami zikijengwa?.”

Raiis Magufuli: "Sitobadilika Hata Kidogo"...... Aahidi kumega Ardhi ya hifadhi kuwapa wananchi

$
0
0
Rais Magufuli ameendelea kusisitiza kuwa hatobadilika na ataendelea kuwa yule yule katika kuwatumikia wananchi.

Pia amesema serikali itamega maeneo ya ardhi ya hifadhi na kuwapa wananchi ili yatumike katika shughuli za maendeleo.

Ametoa msimamo huo leo alipokuwa akifungua matumizi ya barabara ya Uyovu- Bwanga km 45 katika eneo la uyovu runzewe wilayani  Bukombe mkoani Geita.

“Sitobadilika kamwe mimi ni yule yule nitaendelea kuwatumikia watanzania wote,’’ amesema Magufuli

Kuhusu ardhi amesema hatua ya kumega ardhi ya hifadhi ni kufuatia kuwepo kwa ongezeko la idadi ya watanzania tangu  nchi kupata uhuru.

“Ni ukweli usiopingika ni lazima maeneo ya hifadhi yamegwe na kupewa wananchi kwa ajili ya shughuli za maendeleo hii ni kutokana na kwamba idadi ya watanzania imeongeza maradufu tangu nchi ipate  uhuru,’’ amesema Magufuli

Amewata wananchi kuwa na subra na kwamba serikali ipo katika mchakato wa kutoa maeneo hayo.

Rais amesema kutokana na ongezeko la watu maeneo ya kulima na ufugaji yamepungua kwa kiasi kikubwa.

Akitolea mfano amesema kwa sasa matumizi ya ardhi kwa wilaya ya Bukombe ni asilimia 40 na asilimia 60 ni hifadhi.

“Hakuna sababu ya kuandamana wala kupigana kugombea ardhi, serikali itatoa ardhi,’’ alisisitiza.

Barabara hiyo ni kiunganishi cha mikoa ya Geita, Shinyanga, Kigoma, Kagera pamoja na nchi ya  Rwanda

TANGA RAHA- Sehemu ya Ishirini na Sita ( 26 )

$
0
0
AGE………………18+
WRITER…………EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

“Anaitwa nani?”
“Anaitwa RAHMA anasoma kidato cha nne”
Nikajikuta nimekaa kimya nikimtazama mkuu wa shule huku nikijiuliza kama akili zake zinafanya kazi sawa sawa au ndio uzee unamchanganya

ENDELEA
Nikakaa kimya huku nikimtazama mkuu wa shule machoni kwani sikujua ni nini nimuambie
“Eddy ukihitaji hata pesa mimi nitakupatia ili tu nimpate Rahma”
“Ila mkuu mbona msichana mwenyewe simuoni hapa shule”
“Amesafiri ila akirudi tu nataka niweke mambo sawa”
“Usijali mkuu wangu”

Nikajikuta nikinyanyuka kwenye kiti nilicho kaa na kumuaga mkuu wa shule na kumuahidi nitalifanyia kazi na nikarudi ofisini kwa waalimu wengine na kuwakuta kila mmoja akiendelea na shuhuli yake kutokana sikuja kikazi nikabaki nikiwa ninajisomea baadhi ya vitabu vinanavyohusiana na masomo yangu ninayo yafundisha.Simu yangu ikaingia ujumbe mfupi wa meseji na nikakuta ni namba ya Rahma
“BABY UWAHI KURUDI NIPO NYUMBANI KWAKO NA HALDA”
Mapigo ya moyo yakaanza kunienda mbio baada ya kuona saa ya kwenye simu yangu inaonyesha zimabaki dakika kumi kutimu saa sita kamili kabla haujafika muda tulio ahidiana na mchungaji juu ya kwenda kufanya mamombi ambayo kwa wakati huu kwangu sikuyaona na umuhimu wa aina yoyote kwani mchungaji mwenyewe anaushirikiano na Olvia Hitler.Nikanyanyuka kwa haraka na kabla sijaufikia mlango wa kutokea ofisini simu yangu ikaita na kuikuta ni namba ya mchungaji,nikabaki nikiitazama pasipo kuipokea na kumfanya madam Recho kuzungumza

“Jamani si mzime misimu yenu inatupigia kelele”
Niakageuka na kumtazama madam Recho na sikuseme kitu cha aina yoyote zaidi ya kuminya kitufe cha kupokelea simu na kuiweka sikioni na kuisikia sauti ya mchungaji
“Mpendwa tumefika nyumbani kwako tupo hapa getini tunaomba utufungulie mlango kwa maana tunapiga honi nahisi uisikii kutokana na mziki ulio ufungulia kwa sauti ya juu”
“Ahh...Sawa mchungaji nakuja”
Nikakata simu na kubaki nikiwa nimetizama chini huku nikishush pumzi na sikujua nifanye nini kuhusiana na swala la kwenda nyumbani kwa kwangu kwani hali ya hewa imesha haribika.

“Eddy unapakwenda?”
Mkuu wa shule aliniuliza na nikamjibu kwa kutingisha kwichwa nikiashiria kuwa sina pa kwenda
“Basi twende sehemu moja kama huto jali”
“Sawa mkuu”
Tukatoka ofisini na kuingia kwenye gari ya mkuu wa shule na sikujua ni wapi tunakwenda na ndani ya gari sikuzungumza kutu cha aina yoyote hadi tukafika kwenye moja ya mtaa ambao sikuujua jina lake na sote tukashuka kweye gari na mkuu wa shule akaminya kengele ya getini kwenye nyumba nzuri na baada ya muda geti likafunguliwa na akatoka msichana mdogo anaye onekana ni mfanyakazi wa ndani na baada ya kumuona mkuu wa shule akaanza kumchangamkia huku wakitaniaana kwa baadhi ya maneno kisha akatukaribisha ndani na moja kwa moja tukapitiliza hadi sebleni na tukakaa kwenye sofa na msichana wa kazi akasimama na kuiwasha tv iliyopo ukutani na kuaanza kuadilisha badilisha chaneli zilizopo kweye king’amuzi wanacho kitumia

“Babu siku hizi mambo yako sio mabaya naona dada akakupendezesa ana”
“Kawaida babu yangu”
“Mmmm kweli ni kawaida kwani hiyo inye uliyo ifungashia utaweza kusema kuwa wewe ndio mwenye nyumba”
“Babu jamani hujaacha vituko vyako?”
“Ndio ukweli na siku hizi unanga’aa sana”
“Asante”
“Haya huyu mwenzako yupo wapi?”
“Dada amekwenda hospitalini mara moja ila muda si mrefu atarejea”
“Ahaa amakwenda hospitali gani?”
“Buriani”
“Eddy hapa ni nyumbani kwa  madam Rukia”
“Ahaaa asante”
Mfanyakazi wa ndani akaondoka na kwenda jikoni na kutuacha tukia tunatazama Tv baada ya muda kidogo mkuu wa shule akanyanyuka na kuniambia anakwenda mara moja jikoni kuzungumza na mfanya kazi wa ndani.Nikabaki nikitazama Tv galfa nikasikia simu yangu ikiita na nikaitoamfokoni na kuikuta ni namba ya mchungaji,Sikutaka kuipokea nikaiweka simu pembeni huku nikitafakari ni kitu gani nifanye.

Tiba Bora ya Nguvu za Kiume, Kisukari, Ngiri, Miguu Kuvimba

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume yanawaathiri watu wengi kisaikolojia hasa baada ya kujiona tofauti sana na wengine. Kawaida mwanaume anatakiwa kuwa na uume kuanzia nchi 6- 8, vinginevyo mtu huwa na matatizo. Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hilo. 

Baadhi ni upungufu wa vichocheo hivi; Homoni za getrogen ambazo mwanaume anapobalehe, vichochea hivi huchochea ukuaji wa uume.

Ngiri; Hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na hufanya tumbo kuunguruma na kujaa gesi. Sababu zingine ni korodani moja kuvimba, kupopata choo vizuri.

Sababu hizi na zingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba na mara kwa mara husababisha kukosa tendo ya kurudia tendo na baadae kushindwa kabisa

SILYA: Ni dawa inayozalisha homoni zxa Gestrogen na kufanya uume kukua na kuongezeka hadi nchi 6-8
 
WET POWER: Ni dawa bora ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba na matunda ambayo huongeza nguvu za kiume kuanzia miaka 15-95 na hukomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi, ina imariisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa na itakufanya uwe na hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara mbili bila hamu kuisha na pia itakuchelewesha kufika kileleni

Pia tunatibu kisukari, presha, ngiri, miguu kuvimba na kuwaka moto

Wasiliana na Sheikh Khatib akutatulie matatizo yako. Namba zake; 0785 234 837  au 0656 551 093  au 0746473974

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

AISIIIII……….U KILL ME ( Sehemu ya 33 na 34 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA 

Kutokana sikuwa nimekaa sehemu yoyote nikageuza na kutoa chumba huku nikiufunga mlango wa chumba vizuri. Nikaanza kutembea kwenye kordo hii huku nikiwa makini kutazama nyuma na mbele. Mlango wa chumbani cha mbele ukafunguliwa, ikanibidi kupunguza mwendo  wa kutembea, macho yakanitoka baada ya kumuona K2 na Lukas wamesimama mlangoni hapo huku wakipigana mabusu ya mdomoni, huku Lukas akiwa amejifunga taulo kiunoni na K2 akiwa amevalia suti yeusi, ila vifungo vya shati lake vikiwa havikajaa vizuri, kwa bahati mbaya, K2 akanitazama, kitu kilicho mstua sana hata Lukas naye alivyo niona akakimbilia ndani.
  
ENDELEA  
Nikamtazama K2 kwa macho makali yaliyo jaa hasira. Sikutaka kumsemesha chochote zaidi ya kumpita na kuanza kushuka kwenye ngazi kwa kasi.
“Dany, Dany”
Niliisikia sauti ya K2 ikiniita kwa nyuma yangu, sikuona haja ya mimi kuweza kusimama, zaidi ya kuendelea kushuka kwneye ngazi.
“Dany nakuamrisha kama bosi wako, simama”
Kauli ya K2 ikanifanya nigeuke taratibu na kumtazama kwa macho yaliyo jaa dharau, nikamtazama jinsi anavyo hema kwa kuchoka kwa kukunikimbiza, kwenye ngazi hizi.
“Ndio bosi”
“Dany umefikaje fikaje huku?”
“Hicho ndicho kilicho kufanya unisimamishe?”
“Ahaa… kwa maana wewe unaumwa?”
“Kwa hiyo?”
“Sio vizuri kutembea tembea”
“Ehee”
“Ndio”
“Ok”
Nikaanza kushuka tena kwenye ngazi na kumfanya K2 kuniwahi na kunishika mkono wangu wa kulia, nikageuka kwa haraka huku mkono wake nikiwa nimeachanisha kwa nguvu na mkono wangu.
“Hembu nisikilize wewe malaya usiye jitambua. Cheo chako unakitumia katika kutembea na vijana si ndio?”
Nilimfokea K2 hadi akarudi nyuma huku  akiwa amenitumbulia macho ya woga sana.
“Upumbavu wako wote ulio kuwa unaufanya, na hichi nilicho kiona leo nimeutambua. Sasa mwisho uwe leo sihitaji mauhusiano na wewe tena. Umenielewa?”

Nilizungumza kwa sauti nzito huku tinda za sura yangu zikiwa zimejikunja kisawa sawa. K2 hakuzungumza kitu cha aina yoyote zaidi ya kukaa kimya, woga ukiwa umemjaa. Nikaanza kushuka kwneye ngazi huku nikiwa nimejawa na hasira kali, K2 hakuthubutu hata kunyanyua mguu wake na kunigfwata, nikafika mapokezi na kumkuta msichana ambaye ni muhudumu wa hii hoteli.
“Nahitaji maji makubwa na mzinga wa Vodka”
“Sawa”
Dada huyo akafungua friji kubwa lililopo nyuma yake na kunikabidhi chupa kubwa ya maji, kisha akanipatia na mzinga huo wa Vodka.
“Naweza Kulipa kwa creadit card?”
“Ndio”
Nikatoa waleti yangu, na kuchomoa kadi ya malipo, akaipisha kwneye mashine moja ya kulipa kisha akanirudishia kadi yangu, taratibu nikaanza kazi ya kuzipandisha ngazi hizo nikielekea gorofani. Sikumkuta K2 katika sehemu ambayo nilimuacha. Moja kwa moja nikaelekea katika chumba nilicho muacha Babyanka, nikafungua mlango wa chumba hichi na kuufunga kwa ndani.
“Hei nimerudi”

 

ACT-Wazalendo Wameongea na Waandishi wa Habari Leo....Nini Wamekisema?, Bofya Hapa

$
0
0
Ngome ya vijana ya Chama cha ACT Wazalendo imewataka mawaziri wenye dhamana ya kusimamia viwanda, ajira na fedha kukaa pamoja kutafakari tatizo la ajira kwa vijana na kuweka mazingira bora ya ufanyaji wa biashara ndogondogo.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Jumamosi Machi 10, 2018, Katibu wa Sera na Tafiti wa Ngome ya vijana wa chama hicho,  Kitentya Luth amesema uamuzi huo umefikiwa baada ya kushuhudia wimbi la waajiri sekta binafsi na Serikali kupunguza wafanyakazi.

"Hata sekta ya elimu na viwanda ambazo awali zilikuwa zinatoa ajira nyingi nazo hali ni mbaya. Walimu hawajapata ajira kwa zaidi ya miaka mitatu, jambo hilo linasababisha mkwamo katika elimu lakini pia vijana hao wanashindwa kujikwamua kimaisha," amesema Luth.

Tweet ya Kikwete yazua gumzo mtandaoni

$
0
0
Ujumbe wa Rais mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete katikati ya wiki hii uliteka mtandao wa kijamii wa Twitter na kusambaa kwenye Whatsapp, akionesha sehemu ya maisha yake baada ya urais.

Dkt. Kikwete ambaye alihamia Msoga mkoani Pwani kwa ajili ya mapumziko baada ya kutoka Ikulu, aliwepa picha kadhaa akiwa anakula chakula kwenye sahani na bakuli moja na wazee ambao walihudhuria msiba wa baba yake mdogo, Said Lumaliza katika kijiji cha Msigi.

“Tukila chakula na ndugu zangu msibani kwa baba yangu mdogo marehemu Said Lumaliza(1917-2018) katika kijiji cha Msigi karibu na Msoga. Hii ndiyo fahari ya maisha ya kustaafu.!” alitweet mara mbili kwa Kiswahili na Kiingereza, Machi 8.

Watumiaji wa mtandao huo ambao wengine walitoka nje ya nchi walisifu maisha ya kujishusha ya rais huyo mstaafu na kueleza kuwa ni viongozi wachache waliokuwa na cheo kama chake ambao wanaweza kurejea kwenye maisha ya aina hiyo.

“Kuna Maisha baada ya kustaafu. Itafika muda ulinzi kamili itakua ni yale uliyo wafanyia watu na ndicho nilicho jifunza hapo,” aliandika Samuel Isaya.

“Wewe ni rais wa mfano kwa Afrika pamoja na kuwa na mapungufu yako kama binadamu. Hongera sana mhe Mungu akutangulie ktk muda wote wa Maisha yako,” Zakayo Sarwatt.

“It’s very rare to see a former African president from any African country spending time with low class citizens,” aliandika Hermescash. Kwa tafsiri isiyo rasmi, “Ni mara chache sana utaona marais wa zamani Afrika kutoka nchi yoyote wakitumia muda wao na watu wa hali ya chini.”

Godbless Lema: Uhusiano Usioridhisha kati ya wabunge na viongozi wa Serikali unakwamisha shughuli za maendeleo.

$
0
0
Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema amesema uhusiano usioridhisha kati ya wabunge na viongozi wa Serikali unakwamisha shughuli za maendeleo.

Mbunge huyo ameshauri itafutwe suluhu ili kurejesha mahusiano mazuri baina ya makundi hayo.

Akizungumza leo Machi 10, 2018 katika  kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa wa Arusha, Lema amesema kama hakuna mahusiano mazuri kwa viongozi si rahisi kuwapatia wananchi maendeleo.

"Hili ni suala la utawala bora, leo hii kuna watendaji wa Serikali wanaogopa hata kupiga picha na wabunge, hasa wa upinzani. Jambo hili linapaswa kuondolewa kwani lina athari katika jamii,” amesema Lema.

Amesema wabunge wana nafasi ya kuchochea maendeleo ya wananchi na kuondoa kero zao, kwamba kuna wakati kiongozi wa serikali kutokana na sababu za kiitifaki hawezi kupeleka hoja moja kwa moja kwa viongozi wa juu lakini mbunge anaweza.

"Tufanye kazi pamoja, leo hii tunapitisha bajeti ya mkoa lakini kama hatuna mahusiano mazuri baina yetu, sisi kama viongozi sidhani kama tutafanikiwa,” amesema.

Akijibu hoja hiyo ya Lema Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Idd Kimanta amesema anaamini viongozi wa Serikali wanajua wajibu wao wa kufanya kazi na wadau mbalimbali.

"Utawala bora ni pamoja na kufanyakazi pamoja na nina imani hili linafanyika lakini kama kuna watu wanatengwa hilo ni jambo la watu binafsi,” amesema.

Hata hivyo, Kimanta ametaka viongozi kufanya kazi ya kutatua kero za wananchi na kuachana na mambo ya siasa kwani chaguzi tayari zimepita sasa ni wakati wa kufanyakazi.

Tafsiri sahihi ya kosa la uhaini na adhabu yake Kwa Mujibu wa Katiba ya Tanzania

$
0
0
Uhaini  ni  kosa  la  jinai, kwa tafsiri nyepesi ina maana kwamba ni kosa kubwa ambalo mtu analifanya dhidi ya nchi yake na mtu anyefanya kosa hili anajulikana kama msaliti, mfano wa watu wasaliti wanaojulikana duniani ni Yuda ambaye kidini alimsaliti Yesu, mwingine ni Benedict Anold huyu jamaa aliisaliti nchi yake ya Marekani dhidi ya Mbritishi, wengine ni Vidkun Quisling, na Marshall Pe’tain.

Kisheria ukubwa wa kosa hupimwa kwa adhabu yake, kosa likiwa kubwa mtuhumiwa hutumikia adhabu kubwa vivyo hivyo kosa likiwa dogo mtuhumiwa huadhibiwa kiasi.

Kwa mujibu wa sheria ya Tanzania, mtu akifanya yafuatayo huhesabiwa kama amefanya kosa la jinai la uhaini hivyo huadhibiwa kulingana na ukubwa wa kosa hilo.

Kifungu cha 39 ( 1 ) cha kanuni za adhabu kinasema kuwa mtu yeyote ambaye yumo ndani ya Jamhuri  ya Muungano au popote, kujaribu kumuua Rais, kuanzisha vita dhidi ya Jamhuri ya Muungano,  kusababisha, kuwezesha, kuchochea, kushawishi, kushauri kuhusu  kifo, kumlemaza, kumzuia, kufungwa kwa Rais, kumwondolea Rais heshima na jina la mkuu wa nchi, amiri jeshi mkuu, au kiongozi wa serikali, kupindua serikiali iliyo madarakani, kutishia serikali, bunge au mahakama kwa makosa haya na yale yaliyotajwa hapo juu mtu wa namna hiyo atakuwa  ametenda kosa la jinai ambalo ni kosa la uhaini

Aidha ifahamike kuwa kwa mtu yeyote atakayekutwa na hatia ya kutenda kosa la uhaini adhabu yake ni kifo na sheria hiyo ya kifo imeelezwa katika kifungu cha sheria namba 39 na 40 cha kanuni za adhabu.

Hivyo watanzania kwa umoja wetu tunapaswa kuzijua sheria za nchi yetu ili kuweza kujiepusha kutenda makosa ya uhaini  dhidi ya nchi yetu.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images