Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Treni ya abiria yapinduka na kuanguka

$
0
0
Treni ya abiria ya Shirika la Reli Tanzania iliyokuwa ikitokea mkoani Dodoma kwenda Kigoma imepata ajali katika eneo la Kijiji cha Mpeta wilayani Uvinza.

Ajali hiyo imesababishwa na kichwa cha treni kuacha njia na kusababisha mabehewa mawili kuanguka katika dimbwi dogo la maji.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kigoma Martin Othieno amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo. Mpaka sasa hakuna taarifa ya vifo wala idadi ya majeruhi.

Behewa kadhaa bado zimesalia kwenye njia yake baada ya ajali.

Habari Ziliizopo Katika Magazetii yya Leo Alhamisi ya Marchh 1

TCRA yazifungia nyimbo 15 za Wasanii.....Zimo Mbili za Diamond

$
0
0
Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) imepokea list ya nyimbo 15 zisizokuwa na maadili kutoka kwa Baraza la Sanaa Taifa (BASATA).

Nyimbo hizo ziliachiwa na wasanii katika vyombo vya habari pamoja na mitandao ya kijamii bila kupitishwa katika mamlaka husika kwaajili ya kuzikagua na baadaye kuiachia zipigwe.

TCRA imesema nyimbo hizo zina maudhui kinyume na maadili na Huduma za Utangazaji (Maudhui) 2005, hivyo mamlaka hiyo imeviagiza vyombo vya habari kusitisha kuzicheza ngoma hizo.

Japan Yaipatia Tanzania Msaada Wa Sh. Bilioni 77.3 Kujenga New Bagamoyo Road Dar Es Salaam

$
0
0
Serikali ya Japan kupitia Shirika lake la Maendeleo (JICA), imeipatia Tanzania ruzuku ya Yen bilioni 3.78 sawa na Shilingi bilioni 77.3 kwa ajili ya upanuzi wa barabara ya New Bagamoyo, kuanzia Morocco hadi Mwenge, Jijini Dar es Salaam.

Makubaliano ya msaada huo yametiwa saini Februari 28, 2018, Jijini Dar es Salaam na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Mipango Bw. Doto James, kwa niaba ya Serikali, na Balozi wa Japan nchini Tanzania Masaharu Yoshida na kushuhudiwa na Mwakilishi Mkazi Mkuu wa Shirika la Maendeleo la Japani (JICA), Toshio Nagase na Mtendaji Mkuu wa  Wakala wa Barabara nchini-Tanroads, Mhandisi Patrick Mfugale.

Mradi wa barabara hiyo yenye urefu wa kilometa 4.3 utahusisha barabara yenye njia nne pamoja na kuanza kwa awamu ya nne ya ujenzi wa barabara itakayotumiwa na mabasi ya mwendo wa haraka (BRT phase IV).

Akizungumza baada ya kutiwa saini wa makubaliano hayo, Bw. Doto James amesema kuwa barabara hiyo ikikamilika itasaidia  kutatua changamoto ya msongamano wa magari yanayotoka na kuingia katikati ya Jiji la Dar es Salaam.

“Upanuzi wa Barabara ya New Bagamoyo si tu kwamba utaondoa msongamano wa magari, bali pia ni kiungo muhimu cha Bandari ya Bagamoyo ambayo itarahisisha usafirishaji wa abiria, mizigo na huduma kutoka Jiji la Dar es Salaam, mkoa wa Pwani na mikoa mingine nchini” Alisema Bw. Doto James.

Ameishukuru Japan kwa msaada mwingine uliotolewa mwezi Septemba, 2017 wa kiasi cha fedha za Japan (Yen) milioni 69 sawa na shilingi bilioni 1.4 ambazo zimetumika kwa ajili ya kufanya upembuzi yakinifu wa barabara hiyo itakayoanza kujengwa

Bw. James ameeleza kuwa  awamu ya kwanza, Japan ilitoa kiasi cha shilingi bilioni 99.5. kujenga barabara ya njia nne katika kipande cha kilometa 12.9 kutoka makutano ya barabara ya Tegeta na makutano ya barabara ya Mwenge pamoja na kukamilisha ujenzi wa madaraja ya Mlalakuwa, Lugalo na Tegeta.

“Si mara ya kwanza kwa Japan kuisaidia Tanzania, wanajenga barabara za juu katika makutano ya Tazara, ujenzi wa barabara kwa kiwango cha lami kutoka Dodoma hadi Babati mkoani Manyara (km 188.15), Tunduru-Mangaka – Mtambaswala (km 202) na barabara ya Iringa hadi Dodoma (259.9)” alisisitiza Bw. Doto James.

Balozi wa Japan, Mhe. Masaharu Yoshida ameeleza kuwa kutolewa kwa msada huo ili kuwezesha awamu ya pili ya ujenzi wa barabara kuanza kutayafanya matokeo ya kujenga barabara hiyo kuanza kuonekana dhahiri ikiwemo kupunguza msongamano wa magari kwa kiasi kikubwa ili kuokoa fedha nyingi zinazotokana na changamoto za msongamano huo.

“Ili kukamilisha usanifu wa kina wa mradi huu, nilisaini mkataba wa usanifu wa kina wa mradi wa upanuzi wa barabara ya new Bagamoyo  (Awamu ya Pili) miezi mitano iliyopita, hatimaye sasa ninasaini mkataba wa sehemu kuu ambayo ni ujenzi wenyewe” Alisema Balozi Yoshida.

Balozi huyo wa Japan hapa nchini, amesema mradi huo utasaidia kuboresha ukuaji wa uchumi na kupunguza umasikini nchini na kwamba msaada huo ni mwendelezo wa kudumisha uhusiano mzuri uliopo kati ya Japan na Tanzania.

Utafiti uliofanyika hivi karibuni unaonesha kuwa Barabara ya Bagamoyo ndiyo yenye msongamano mkubwa wa magari  yanayokadiriwa 52,000 yanayopita kila siku katika barabara hiyo.

Lundenga Aitema Miss Tanzaniia

$
0
0
Mkurugenzi wa Kampuni inayoandaa mashindano ya Miss Tanzania ya Lino International Agency LTD Hashim Lundenga ametangaza rasmi kuacha shughuli za kuendesha mashindano hayo kuanzia Februari 13 mwaka huu.

Hivyo kuanzia sasa mashindano ya Miss Tanzania nchini yataendeshwa na The Look Company Limited, chini ya Mkurugenzi Basilla Mwanukuzi aliyewahi kuwa Miss Tanzania mwaka 1998.

Akizungumza jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi wa kampuni hiyo, Hashim Lundenga amesema uamuzi huo umetokana na malengo yao ya kutaka mashindino hayo kusimamiwa na damu changa kwa lengo la kuleta chachu katika tasnia ya urembo nchini.

“Tumefikia uamuzi huu baada ya kuona kampuni yetu tayari imejijengea sifa na heshima nchini.Hata hivyo tunaamini The Look Company Limited chini ya Mkurugenzi Mwanukuzi watasimamia taratibu, kanuni, sheria na miiko ya uongozi na hatimaye kumpeleka mrembo katika mashindano ya dunia kama ilivyo kawaida,”amesema. 

Amewataka waandaaji wapya wa mashindano ya urembo wasisite kuomba ushauri au mawazo ya kujenga kutoka kwao pale watakapohitaji.

Lundenga ambaye ni maarufu kama Uncle Hashim amewashukuru Baraza za sanaa la Taifa (BASATA), na Wizara ya Habari, Utamaduni,Sanaa na Michezo kwa ushirikiano mkubwa kwa muda wote tangu kuanza kwa mashindano hayo mwaka 1994.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kampuni ya Look Limited, Mwanukuzi amesema wamejiwekea mikakati kuendeleza fani ya ulimbwende pale ambapo kampuni ya Lino imeishia. Amesema kuwa pale penye changamoto katika kuandaa masuala ya warembo watakuwa karibu na Kampuni ya Lino pamoja na BASATA ili kufanikisha na kuleta tija katika Taifa.

Rais Shein Apangua Baraza la Mawaziri

$
0
0
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Dkt. Ali Mohamed Shein amafanya mabadiliko madogo katika Baraza la Mapinduzi kwa kuongeza Wizara moja zaidi, na kuwabadilishia Wizara baadhi ya Mawaziri.
 
Kufuatia mabadiliko hayo, shughuli za Vijana zimehamishiwa katika Wizara mpya ya Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo; shughli za Mazingira zimehamishiwa katika Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais; na shughli za Wakala wa Serikali wa Uchapaji zimehamishiwa Wizara mpya ya Habari, Utalii na Mambo ya Kale.
 
Aidha, amewateua Naibu Mawaziri wapya wawili na kumbadilisha Wizara Naibu Waziri mmoja. Kufuatia mabadiliko hayo, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar hivi sasa itakuwa na Wizara 14 zenye Mawaziri na Naibu Mawaziri kama ifuatavyo:
  1. OFISI YA RAIS NA MWENYEKITI WA BARAZA LA MAPINDUZI
  2. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi- Mheshimiwa Issa Haji Ussi Gavu
  3. OFISI YA RAIS, KATIBA SHERIA, UTUMISHI WA UMMA NAUTAWALA BORA
  4. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais – Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora – Mheshimiwa Haroun Ali Suleiman
  5. Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Katiba, Sheria, Utumishi wa Umma na Utawala Bora – Mheshimiwa Khamis Juma Mwalim
  6. OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA SERIKALI ZA MITAA NA IDARA MAALUM ZA SMZ
  7. Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ – Mheshimiwa Haji Omar Kheri
  8. Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ – Mheshimiwa Shamata Shaame Khamis
  9. OFISI YA MAKAMU WA PILI WA RAIS
  10. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais – Mheshimiwa Mohamed Aboud Mohamed
  11. Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais – Mheshimiwa Mihayo Juma Nhunga
  12. WIZARA YA AFYA
  13. Waziri wa Afya- Mheshimiwa Hamad Rashid Mohamed
  14. Naibu Waziri wa Afya – Mheshimiwa Harusi Said Suleiman
  15. WIZARA YA ARDHI, NYUMBA, MAJI NA NISHATI
  16. Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati – Mheshimiwa Salama Aboud Talib
  17. Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba, Maji na Nishati – Mheshimiwa Juma Makungu Juma
  18. WIZARA YA BIASHARA NA VIWANDA
  19. Waziri wa Biashara na Viwanda – Mheshimiwa Balozi Amina Salim Ali
  20. Naibu Waziri wa Biashara na Viwanda – Mheshimiwa Hassan Khamis Hafidh
  21. WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA AMALI
  22. Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali – Mheshimiwa Riziki Pembe Juma
  23. Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amal Mheshimiwa Mmanga Mjengo Mjawiri
  24. WIZARA YA FEDHA NA MIPANGO
  25. Waziri wa Fedha na Mipango – Mheshimiwa Dkt. Khalid Salum Mohamed
  26. WIZARA YA HABARI, UTALII NA MAMBO YA KALE
  27. Waziri wa Habari, Utalii na Mambo ya Kale – Mheshimiwa Mahmoud Thabit Kombo
  28. Naibu Waziri wa Habari, Utalii na Mambo ya Kale – Mheshimiwa Choum Kombo Khamis
  29. WIZARA YA KAZI, UWEZESHAJI, WAZEE, WANAWAKE NA WATOTO
  30. Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto – Mheshimiwa Maudline Cyrus Castico
  31. Naibu Waziri wa Kazi, Uwezeshaji, Wazee, Wanawake na Watoto – Mheshimiwa Shadia Mohamed Suleiman
  32. WIZARA YA KILIMO, MALIASILI, MIFUGO NA UVUVI
  33. Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi – Mheshimiwa Rashid Ali Juma
  34. Naibu Waziri wa Kilimo, Maliasili, Mifugo na Uvuvi – Mheshimiwa Dkt. Makame Ali Ussi
  35. WIZARA YA UJENZI, MAWASILIANO NA USAFIRISHAJI
  36. Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji – Mheshimiwa Dkt. Sira Ubwa Mamboya
  37. Naibu Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji – Mheshimiwa Mohamed Ahmada Salum
  38. WIZARA YA VIJANA, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO
  39. Waziri wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo – Mheshimiwa Balozi Ali Abeid Karume
  40. Naibu Waziri wa Vijana, Utamaduni, Sanaa na Michezo – Mheshimiwa Lulu Msham Abdulla
Aidha, Mheshimiwa Said Soud Said na Mheshimiwa Juma Ali Khatib wanaendelea kuwa Wajumbe wa Baraza la Mapinduzi na Mawaziri Wasiokuwa na Wizara Maalum.

NEC Yatumiia Hoja 6 Kumzima Mbowe

$
0
0
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesisitiza kuwa itaendelea kuzingatia Sheria, Kanuni, Maadili na taratibu mbalimbali katika kuendesha chaguzi nchini.

Kauli hiyo imetolewa jana jijini Dar es salaam na Mkurugenzi wa Uchaguzi (NEC), Kailima Ramadhani  wakati akijibu shutuma zilizotolewa na Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Mhe. Freeman Mbowe juzi, kupitia vyombo vya habari na mitandao ya kijamii NEC haikutoa ushirikiano kwa Chama hicho na kwamba ilikiuka Sheria na taratibu za Uchaguzi katika kuendesha Uchaguzi Mdogo uliofanyika Februari 17, 2018.

“ Ni kwamba shutuma na malalamiko yaliyotolewa na Mhe, Mbowe yametusikitisha kwa sababu mbali na kumjibu kwa barua, tuliongea naye kwa njia ya simu. Haya  madai kwamba Tume haikuyajibu malalamiko yao sio kweli, ni upotoshaji wa hali ya juu ambao haupaswi kufanywa na kiongozi kama yeye” Alisisitiza Kailima.

Alisema Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) haijibu malalamiko kwa kuzingatia  matakwa ya mtu bali inajibu hoja kwa mujibu matakwa ya Katiba, Sheria, Kanuni na Maadili ya uchaguzi pamoja na maelekezo yote ambayo yapo kwa mujibu wa sheria.

Alieleza kuwa Kanuni, sheria, maelekezo na maadili ya Uchaguzi yameweka utararatibu wa kushughulikia malalamiko na changamoto mbalimbali zinazojitokeza wakati wa uchaguzi ,uteuzi, na wakati wa kipindi cha kampeni ambapo malalamiko yote hushughulikiwa  na Kamati za Maadili zilizo katika maeneo husika ya uchaguzi kuanzia ngazi ya Kata, Jimbo na Rufaa.

“Kwa masikitiko CHADEMA walitekeleza hatua moja tu katika vipengele hivyo wakati wa uchaguzi, kipengele walichotekeleza ni pale baadhi ya wagombea wao walipoenguliwa kugombea, walifuata utaratibu kwa kuwasilisha rufaa Tume ya uchaguzi na Tume ilipitia na ikawarudisha wagombea wao kwenda kugombea” Alisisitiza Kailima.

Alibainisha kuwa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kilitaka wakati wa kampeni Tume ifanye maamuzi kinyume cha maadili waliyoyasaini akisisitiza kuwa kamati za maadili ngazi ya jimbo ambazo Mwenyekiti wake ni Msimamizi wa Uchaguzi na wajumbe wake ni kutoka vyama vyote vilivyosimamaisha wagombea ndio wanaofanya uamuzi.

Aidha, alisema CHADEMA  waliwasilisha malalamiko kwa Tume badala ya kuwasilisha malalamiko kwenye kamati hizo za maadili zinazosimamia malalamiko yote. 

“ Sio sahihi kusema Tume hatukujibu malalamiko yao. Mfano tarehe 15 Chadema waliwasilsiha barua mbili Tume ya Uchaguzi, waliwasilisha barua moja asubuhi na saa 1.30 jioni waliwasilisha barua nyingine, jumla barua hizo zikiwa na hoja tano na Tume ikawaandikia barua zenye ufafanuzi wa hoja hizo”

Akitoa ufafanuzi kuhusu hoja zilizowasilishwa na CHADEMA alisema kuwa Chama hicho kilitaka Mawakala wao mbadala ambao ni asilimia 15 waapishwe hatua iliyoifanya NEC iwajibu kwamba hakuna kifungu cha Sheria kinachotoa fursa kwa chama chochote cha siasa kuapishiwa mawakala mbadala asilimia 15.

“ Ukisoma Kifungu cha 57 (3) cha Sheria ya Taifa ya Uchaguzi  kinafafanua vizuri namna ya mawakala wanavyotakiwa kuwepo na kuapishwa lakini pia hata kama kifungu hicho kingekuwa kinatoa fursa hiyo, Chadema walileta malalamiko yao  tarehe 15 Februari 2018 wakati muda wa uteuzi wa mawakala ulikuwa tarehe 10 Februari 2018, hivyo hakukuwa na muda wa kuwaapisha mawakala wengine kwa mujibu wa sheria kwa kuwa hawakuwemo kwenye orodha” Alisisitiza.

Hoja nyingine iliyowasilishwa na CHADEMA ni ya Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Kinondoni alikataa kuwapa mawakala barua na fomu za viapo.  

“Kuhusu hoja hii tulifanya hesabu tukaona kwamba msimamizi alitakiwa kusaini barua 22,000 na fomu za viapo 14,000. Tukasema kwamba kutakuwa na utaratibu wa mawakala kupewa fomu na viapo vyao kupitia kwa wawakilishi wao na walipewa kwa njia hiyo,  Hili tuliwajibu hivyo katika barua yetu” Alibainisha Kailima.

Kuhusu Mawakala wa CHADEMA kuambiwa kwenda na vitambulisho kwenye vituo vya kupigia kura NEC iliwajibu kwamba wakala chama cha siasa ni mpiga kura kama walivyo wapiga kura wengine.

 Aidha, Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa kuzingatia sheria ya uchaguzi kifungu namba 61 na namba  62 cha sheria za Serikali za Mitaa ilitoa ridhaa kwa wapiga kura kutumia vitambulisho mbadala ili nao waweze kupiga kura ndio maana wakaelekezwa kwenda navyo.

Hoja nyingine ni kwamba msimamizi wa uchaguzi jimbo la Kinondoni, hajatoa maelekezo ni wapi pa kuhesabia kura ambapo walijibiwa kwamba Tume ina barua kutoka kwa msimamizi wa uchaguzi akiwajulisha vyama vya siasa kwamba sehemu ya kujumlishia kura itakuwa ni sehemu ya Biafra.

“Kanuni inasema wangejulishwa eneo hilo la kujumlishia baada ya kura kupokelewa, lakini msimamizi wa uchaguzi aliwajulisha mapema eneo la kujumlishia kura” Alisema.

Hoja nyingine iliyotolewa inahusu Wasimamizi wa vituo hawakuteuliwa kwa utaratibu. Majibu ya hoja hii ni kwamba sheria ya uchaguzi imeweka utaratiibu wa namna wasimamizi hao wanavyopatikana. Lakini kanuni za uchaguzi wa Rais namba 15 na kanuni 11 za Serikali za Mitaa zinaeleza namna msimamizi wa kituo anavyopatikana.

Kanuni hiyo inasisitiza kuwa msimamizi wa uchaguzi atatoa tangazo, Kwa jimbo la Kinondoni msimizi alitoa tangazo, watu waliomba, walifanya usahili na kabla ya uteuzi mkurugenzi wa uchaguzi alitoa matangazo ya majina katika mbao zote za kata 10 za jimbo la Kinondoni.

Aidha, alisema kuwa Msimamizi wa uchaguzi aliwaandikia barua vyama vyote kama vina pingamizi vijitokeze. Kama kulikuwa na tatizo vyama vilikuwa na fursa ya kuweka pingamizi, lakini hawakufanya hivyo na Tume iliwajibu hivyo. Wanaposema Tume haikuwajibu sio kweli  labda  waseme walijibiwa nje ya matakwa yao  na sio kwa mujibu wa sheria.

Kuhusu hoja ya wizi wa kura ameeleza kuwa katika kituo cha kupigia kura kuna Msimamizi wa kituo, Msimamizi msaidizi na Wakala wa chama cha siasa na kuna waandishi wa habari hivyo hakukua na fursa ya jambo hilo kutokea.

Alisema utaratibu wa upigaji wa Kura ulikuwa wazi na kusisitiza kuwa kuna utaratibu wa kisheria wa kuwasilisha malalamiko kama mtu haridhiki kabla wakati na baada ya kupiga kura, wakati wa kuhesabu na baada ya kuhesabu kura.

Mkurugenzi Kailima alieleza kuwa mtu au chama kisipofuata uratibu huo, lazima kitailalamikia Tume na Mgombea akikataa kufuata utaratibu huo hata akija Tume kulalamika,ataelekezwa na Tume atumie wakala wake kujaza fomu zote namba 14 na 16 zinazohusika kisheria kuwasilisha malalamiko.

“Tunamsihi Mbowe na chama chake, wasome sheria za uchaguzi na kuzielewa. Tume iko tayari kumpa elimu ya mpiga kura kuzifahamu sheria hizi kwa mapana yake, Pia tunamwomba Mhe. Mbowe kama hakuridhika na taratibu za uchaguzi, ana fursa ndani ya siku 30 za kuwasilisha malalamiko yake Mahakamani ambacho ndicho chombo pekee cha kutoa haki’” Alisisitiza 

Amekitaka Chama hicho kwenda Mahakamani kwa kutumia ushahidi ambao Mawakala wake walijaza kwenye fomu namba 14 na 16 kwa sababu Tume ya Uchaguzi haina tena fursa ya kupokea malalamiko kisheria baada ya uchaguzi kupita.

Mkuu wa Majeshi: Kuna Viashiria vinavyotishia Usalama wa Nchi, Hatua zinachukuliwa kudhibiti hali hiyo

$
0
0
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama (JWTZ), Jenerali Venance Mabeyo amewataka Watanzania kujiepusha na vitendo vinavyoweza kutishia usalama wa nchi na kuharibu tunu ya amani iliyopo.

Ameeleza kuwa hivi sasa vipo viashiria vinavyotishia usalama wa nchi, na kwamba hatua zinachukuliwa ili kudhibiti hali hiyo.

Jenerali Mabeyo amewaomba Watanzania kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Rais John Magufuli dhidi ya wizi, ufisadi na matumizi mabaya ya ofisi za umma, kwa kuwataja hadharani watu wanaojihusisha na vitendo hivyo.

Ametoa kauli hiyo jana wakati akifunga Maadhimisho ya Tamasha la Mashujaa wa Vita ya Majimaji katika Viwanja vya Makumbusho ya Mashujaa wa Vita ya Majimaji mjini Songea.

Mabeyo amesema vita dhidi ya wizi na ufisadi, iliyoanzishwa na Rais Magufuli, si ya mtu mmoja, bali kila Mtanzania anapaswa kushiriki, kwani mali zinazoibwa na baadhi ya Watanzania, zinapaswa kuwanufaisha watu wote.

Mabeyo alisema badala ya kushughulika na uvunjifu wa amani, ipo haja ya Watanzania kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Serikali ya Awamu ya Tano, ambayo imedhamiria kuwatumikia wananchi kwa kuboresha huduma za kijamii ili kutoa fursa kwa wananchi kutumia muda wao kufanya kazi za kujiletea maendeleo.

Ametaja baadhi ya mambo yanayotishia usalama wa nchi kuwa ni matumizi mabaya ya utandawazi ambayo mbali na ya kuharibu utamaduni wa nchi, baadhi ya watu wanaitumia vibaya kwa kuhamasisha wananchi kufanya na kushiriki katika matukio ambayo yanaashiria uvunjifu wa amani na utulivu uliopo nchini kwa muda mrefu.

Jenerali Mabeyo alitaka shule za msingi, sekondari na vyuo nchini, kufundisha wanafunzi umuhimu wa kulinda, kutunza amani na wananchi kuishi kwa kupendana, badala ya kutumia muda wao kutafuta sababu za kutengana, jambo ambalo halina tija kwa taifa.

Wakati huo huo, Jenerali Mabeyo aliitaka Wizara ya Maliasili na Utalii kuboresha Makumbusho ya Mashujaa wa Vita ya Majimaji ili yatumike kwa ajili ya utalii na kuliingizia taifa fedha nyingi.

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Chiristina Mndeme alisema Serikali ya Mkoa wa Ruvuma, itaongeza nguvu katika kulinda mipaka yake ili wananchi wa mkoa huo waweze kuendelea na kazi za uzalishaji mali. 

Sh1.9bilioni zatolewa kubotesha vituo vya afya

$
0
0
Serikali  imepeleka Sh1.92bilioni  katika Halmashauri ya mji wa Nanyamba wilayani Mtwara kwa ajili ya ujenzi na uboreshaji wa vituo vya afya.

Hayo yameelezwa jana Jumatano Februari 28, 2018 na Waziri Mkuiu, Kassim Majaliwa ameeleza hayo wakati akizungumza na wakazi wa halmashauri hiyo, akiwa katika ziara mkoani Mtwara.

Amesema fedha hizo zilitolewa na Serikali ili kuimarisha upatikanaji wa huduma za afya kwa wananchi, kwamba Sh1.2bilioni zimetolewa kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha afya Kata ya Njengwa, ambapo aliwasisitiza watendaji kutobadilisha matumizi.

Amebainisha kuwa ujenzi huo utahusisha chumba cha upasuaji, maabara, chumba cha kujifungulia, jengo la mama na mtoto na wodi ya wanawake na wanaume, eneo la kuchomea taka na chumba cha kuhifhadhia maiti.

“Serikali imeamua kuimarisha sekta ya afya kwa kujenga na kuboresha vituo vya afya ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma za afya karibu na makazi yao,” amesema.

Aidha, Majaliwa amewataka wananchi hao kuendelea kuiunga mkono Serikali ambayo imedhamiria kuwatumikia ili waweze kupata maendeleo.

Amesema Serikali inatarajia kuipitia upya sheria ya elimu pamoja na sheria ya mtoto ili kuweka masharti ya kumlinda mtoto wa kike hususani kudhibiti mimba kwa wanafunzi.

Awali, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Gelasius Byakanwa amesema Serikali itawachukulia hatua watu wote watakaobainika kuwapa watoto wa kike dawa za uzazi wa mpango ili kuwazuia wasipate mimba.

Amesema wanafunzi wa kike katika halmashauri hiyo wamebainika kuwa wanatumia dawa za kuzuia mimba wakiwa shuleni, hivyo kuwaruhusu kushiriki katika matendo yasiyokuwa ya kimasomo.

Amebainisha kuwa Serikali itafanya msako wa kuwatafuta wote wanaotumia dawa hizo pamoja na wanaowapa na watakaobainika hatua kali zitachukuliwa dhidi yao kwa sababu jambo ni hatari kwa maendeleo ya wanafunzi hao.

Idadi ya Watanzania Sasa ni Milioni 54.2.....Mwaka 2030 Wataongezeka na Kufikia Milioni 77.5

$
0
0
WAZIRI wa Fedha na Mipango,Dk. Philip Mpango amepiga marufuku kwa shirika lolote kufanya makadirio ya idadi ya watu wa Tanzania na kuchapisha matokeo hayo bila kushirikisha Ofisi ya Taifa ya Takwimu na atakayebainika kufanya hivyo watamchukulia hatua kali za kisheria.

Dk.Mpango amesema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati anazindua taarifa ya makisio ya idadi ya watu Tanzania ambapo alisema kwa makadirio yaliyotokana na Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012.

Viwango vya uzazi na vifo kwa takwimu za mwaka 2016, idadi ya watu Tanzania sasa ni milioni 54.2 ambapo Tanzania Bara ni watu milioni 52.6  na Tanzania Bara watu milioni 1.6 kwa mwaka 2018.

Dk.Mpango aliisema idadi hiyo inakadiriwa kufikia watu milioni 59.4 mwaka 2021 na ifikapo mwaka 2030 idadi ya watu itafikia milioni 77.5.

Pia Dk.Mpango aliwakumbusha wadau wote wa ndani na nje ya nchi kuwa takwimu za idadi ya watu kwa nchi ya Tanzania ni hizo ambazo amezitangaza jana na si vinginevyo.

Alifafanua kwa kuzingatia matokeo ya Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 inakadiriwa kuwa kila mwaka kuna ongezeko la wastani watu wapatao milioni 1.6 hapa nchini.

Dk.Mpango alisema ongezeko hill linatokana na idadi kubwa vya vizazi vipatavyo milioni 2.0 ikilinganishwa na idadi ndogo ya vifo ambavyo ni takribani 400,000 kwa mwaka.

“Utafiti wa mama na mtoto wa mwaka 2015/16 unaonesha kwamba mwanamke wa kitanzania atazaa watoto watano katika maisha yake yote ya uzazi .

” Hata hivyo kiwango cha uzazi kilipungua kutoka wastani wa watoto 7 mwaka 1978 had I wastani wa watoto watano mwaka 2016.Baadhi ya sababu za juu cha uzazi ni kiwango kikubwa cha vifo vya watoto,familia kupendelea kuwa na watoto wengi,umasikini,mila,imani za kidini na matumizi madogo ya uzazi wa Mpango,”alisema.

Aliongeza matokeo yake ni kuwa na idadi ya watu hapa nchini imeendelea kuongezeka na kuifanya Tanzania kuwa nchi ya sita katika Bara la Afrika kwa kuwa na idadi kubwa ya watu baada ya Nigeria, Ethiopia, DRC na Misri.

Alisema kwa mtazamo wake wingi au au uchache wa idadi ya watu sio tatizo bali tatizo ni pale ambapo kasi ya ongezeko la idadi hiyo inazidi kasi ya ukuaji wa  uchumi na hivyo kulifanya Taifa kushindwa kumudu ipasavyo mahitaji ya wananchi.

Dk.Mpango alisema kasi ya ongezeko la idadi ya watu pia inaleta changamoto ya idadi kubwa ya watoto na vijana .”Kwa mfano takwimu nilizozizindua leo zinaonesha asilimia 50 ya watu wote nchini ni watoto wenye umri chini ya miaka 18.

“Asilimia hii kubwa ya watoto katika nchi zinazoendelea inatokana na mabadiliko ya kidemografia kutoka viwango vya juu vya vifo lakini wakati huo viwango vya uzazi vibaki juu,” alisema.

Aliongeza asilimia kubwa ya watoto ni changamoto kwa maendeleo ya nchi yoyote duniani kwa vile kundi hilo lina mahitaji ya kipekee ambayo lazima yatimizwe na Serikali na jamii kwa ujumla wake.

Dk.Mpango alisema mojawapo ya changamoto hizo ni kiwango cha juu cha utegemezi kinachotokana na idadi kubwa ya watoto.

Alisema kwa mfano kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi ya mwaka 2012 kiwango cha utegemezi kiumri  ni asilimia 92 ikilinganishwa na wastani wa asilimia 40 kwa nchi zinazoendelea.

Hiyo ikiwa na maana kuwa kwa Tanzania kila watu 100 wenye umri wa miaka 15 hadi 64 wanategemewa na watu 92 wenye umri chini ya miaka 15 wenye umri zaidi ya miaka 65.

Kabla Sijafa - Sehemu ya 01 ( Simulizi ya Kweli)

$
0
0
Mwandishi: Grace G. Rweyemam
“Habari Grace. Ninaitwa Ninah, ningependa katika simulizi unazotuma fesibuku, nikupe na wosia wa kaka yangu marehemu, uwaandikie watu. Kabla hajafa aliniomba sana niwambie watu wengi kadiri niwezavyo kile alichotaka wajue. Akaniachia barua ndefu sana aliyoiandika mwenyewe”

Nilisoma ujumbe huo nikastuka na kutamani kujua huo wosia wa marehemu aliotaka uwafikie watu unahusu nini. Nilimpa anuani yangu ya barua pepe na kumuomba aniandikie huo wosia humo, nijue kama kweli ungefaa kuwafikia watu kama ambavyo marehemu alidai.

Nirudi nyuma kidogo, Kuna mdogo wangu yuko katika kundi moja la fesibuku, la wasichana na wanawake, amekuwa akinisimulia visa kadha wa kadha vinavyowatokea wadada wengi walio kwenye ndoa.

Mambo mengi ambayo huwa hunisimulia hunifanya nijue kumbe kweli UKIMWI bado upo na unaua. Kuna kisa fulani aliniambia miezi kadhaa iliyopita, kikanifanya nitamani kama watu wengi zaidi wangeelewa uhalisia wa huu ugonjwa na jinsi unavyowamaliza wengi mpaka leo hii, hata wale wasiotegemea.

Mbaya zaidi kwa sasa ambapo kumekuwa na dawa za kuongeza kinga, wagonjwa wengi wa UKIMWI hawajulikani kwa kuonekana kwa macho, na huo umekuwa mtego kwa watu wengi.

Kuna binti mmoja, nitampa jina la Vero, kwenye hilo kundi ana ndoa ya miaka mitatu na wana mtoto mmoja, aliwahi kufuma jumbe za mapenzi kwenye simu ya mume wake, mwanaume akawa akijitetea na kuomba msamaha, binti akasamehe.

Siku moja binti aliamua kufuatilia namba, alipofuma tena ujumbe wa mapenzi kwa mume wake, akaja kugundua kumbe ni ya jirani yao, cha kumshangaza zaidi huyo jirani yao ni kijana wa kiume.

 Binti akachanganyikiwa ndipo akaamua kuomba ushauri kwenye hilo kundi, pasipo kujitaja jina lake, watu wakamshauri asamehe, asimfuatilie mwanaume, wengine wakashauri aachane naye, na kuna waliomshauri akapime na akikutwa salama basi amuache.

Sasa akiwa anafikiria nini cha kufanya, siku mbili baadaye akiwa nyumbani kwake, alitembelewa na jirani yake mwingine nitamuita Siwema. Katika maongezi yule mwanamke Siwema, bila kujua chochote akaanza kuelezea kuwa yule kijana jirani ambaye Vero aligundua kwamba ana mahusiano na mumewe ni shoga na ni muathirika.

Siwema aliongea kwa malalamiko kuwa kuna mtoto wa dada yake (naye ni wa kiume) alikuja kuishi kwake kwa muda wa miezi mitatu akiwa likizo ndefu ya chuo kikuu, kumbe walianzisha mahusiano na yule mvulana. Sasa anadai siku kadhaa zilizopita amegundulika ameathirika, amechanganyikiwa sana kijana pamoja na mama yake.

Siwema alisema alishasikia tetesi hapo nyuma kuwa yule kijana ameathirika, ila hakutilia mkazo sana, mpaka alipogundua amemuambukiza huyo mtoto wa dada yake, kwani kijana baada ya kupimwa na kukutwa na UKIMWI alimueleza mama yake ukweli kuhusu ni wapi anahisi ameutoa.

Akielezea tena Vero kupitia kwa kiongozi (admini) wa hilo kundi, alisema, “Nikiwa bado nawaza kuhusiana na ushauri wenu, nilikuja kugundua kuwa yule kijana anayetembea na mume wangu ni kweli ni shoga na ameathirika. 

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Tanzania yazikataa meli za Korea Kaskazini

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Nje, Dk. Augustine Mahiga amewafahamisha  mabalozi wa nchi tano ambazo ni wajumbe wa kudumu wa baraza la usalama la Umoja wa Mataifa kwamba meli mbili zilizoonekana zikielekea Korea ya Kaskazini zikipeperusha bendera ya Tanzania; zilishafutiwa usajili miaka miwili iliyopita.

Inadaiwa kuwa Meli hizo zilizokuwa zikipeperusha bendera ya Tanzania zilionekana kwa njia ya satelaiti, moja ikielekea Korea ya Kaskani moja kwa moja na nyingine ilinaswa ikihamisha mizigo ambayo haikutambulika kwenye meli nyingine ambayo baada ya zoezi hilo la uhamishaji ilielekea Korea ya Kaskazini baada ya kupakia mizigo hiyo.

Balozi Mahiga amewaomba Mabalozi hao kutoka Marekani, Uingereza, Ufaransa Urusi na China kuisadia Tanzania kuweza kuzibaini meli zinazopeperusha bendera ya Tanzania na kwenda kinyume na utaratibu wa kimataifa wa usafirishaji baharini.

Januari mwaka huu Tanzania ilizifutia usajili meli zote 450 zilizokuwa zinapeperusha bendera ya Tanzania kwenye maji ya kimataifa baada ya kupatikana kwa meli iliyokuwa imebeba shehena ya silaha na dawa za kulevya huku ikipeperusha bendera ya Tanzania.

Wiki moja iliyopita Rais wa Marekani Donald Trump alitishia kuyawekea vikwazo vya Kiuchumi Kidplomasia Kisiasa na kibiashara mataifa yote yatakayokiuka vikwazo vilivyowekwa na Umoja wa Mataifa na Marekani dhidi ya Korea ya Kaskazini.

Habari Njema: Tunatibu Busha, Korodani Kuvimba,Ngiri, Miguu Kufa Ganzi Pamoja na Matatizo ya Nguvu za Kiume

$
0
0
Ni dawa ya nguvu za kiume inayorefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo (Inch 1-7) kwa muda wa siku 6 tu.Dozi hii itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa muda wa dakika 30, utarudia tendo la ndoa zaidi ya mara 4 bila hamu kuisha bila kujali umri na garantee ni miaka 60 baada ya kutibu tatizo.

Pia tunatibu Busha bila kufanyiwa Oparesheni, korodani moja kuvimba, ngiri, tumbo kujaa gesi na kuunguruma, kutopata choo vizuri, miguu kuwaka moto na kufa ganzi, chango la wanawake, kisukari na kutokwa na kinyama sehemu ya haja kubwa.

MIHAYO:
Inarudisha mke, mchumba, hawara na atakutimizia kila kitu unachotaka kutoka kwake ndani ya  saa 2 tu hata kama yupo mbali. atarudi na kumfunga asiwe na mwingine zaidi yako.

Umefukuzwa kazini? unataka kupandishwa cheo? Umepoteza pesa zako kwenye biashara bila kujua umepandikizwa chuma ulete? Njoo urudishe pesa zako. Unauza mali yako haiendi? Wasiliana na mtaalam Challo kwa; 0714006521

Tupo Mbagala

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FULL POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

Wimbo wa Kibamia wamponza Roma Mkatoliki, afungiwa miezi sita

$
0
0
Naibu Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, Juliana Shonza amemfungia msanii Roma Mkatoliki kutojihusisha na tasnia ya muziki kwa kipindi cha miezi sita.

Akizungumza leo Machi 1, 2018 na baadhi ya wasanii aliowaita na kuwaeleza dosari zilizopo katika nyimbo zao, Shonza amesema baada ya Roma kupewa muda wa kufanya marekebisho wimbo wake wa Kibamia ameshindwa kutekeleza agizo hilo.

“Mpaka sasa hajaufanyia marekebisho na wimbo huo unaendelea kurushwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari. Tulitoa muda kwa Roma kufanyia marekebisho wimbo wake tangu mwaka jana mwishoni lakini mpaka leo ni miezi mitatu ameshindwa kutekeleza hilo,” amesema Shonza.

Amesema jana msanii huyo alipigiwa simu ili leo afike katika kikao hicho kwa ajili ya kujitetea, pia hakutokea.

Shilole ahukumiwa kulipa faini Milioni 14

$
0
0
Mahakama ya Mwanzo ya Wilaya ya Kinondoni, Jijini Dar es Salaam imemhukumu msanii wa muziki wa Bongo Fleva na mjasiriamali, Zuwena Mohamed maarufu Shilole kulipa faini ya kiasi cha shilingi milioni 14, baada ya kupatikana na hatia ya kutapeli na kusababisha hasara kwa kushindwa kufika kwenye tamasha.

Katika kesi hiyo imethibitika kuwa Shilole alilipwa kiasi cha shilingi Milioni tatu na Mary Musa ambaye ndiye muandaaji wa shoo hiyo,  ili aweze kutumbuiza siku ya mkesha wa Pasaka wa mwaka jana, 2017 katika ukumbi wa Heineken uliopo Mbagala-Kijichi jijini Dar es Salaam, lakini hakufika kama walivokuwa wamekubaliana.

Baada ya mashabiki waliokuwa wameahidiwa kupata burudani kutoka kwa Shilole kutokumuona, walipandwa na hasira na kufanya vurugu kubwa iliyosababisha uharibifu wa mali za thamani ya shilingi milioni 14.

Kutokana na kitendo hicho, Mahakama imemuamuru Shilole kulipa kiasi hicho cha fedha kama fidia kwa mlalamikaji ambaye ni Mary Musa.

Mlipuko wa transfoma wazua kizaazaa mahakamani

$
0
0
Shughuli katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu zilisimama kwa muda baada ya kutokea kwa hitilafu ya umeme katika transfoma ya Shirika la Umeme Tanzania (Tanesco) iliyopo katika eneo la mahakama hiyo.

Trasfoma hiyo imelipuka na kusababisha nyaya mbili kushika moto na kuzua hofu miongoni mwa watu waliokuwa mahakamani hapo, kuanza kukimbia hovyo.

Tukio hilo limetokea leo asubuhi Machi 1, 2018 wakati kesi mbalimbali zikiendelea kusikilizwa.

Mtendaji wa Mahakama Mkoa wa Dar es Salaam, Gasto Kanyairita amesema baada ya kutokea kwa mlipuko huo ulizuka moto  na kushika nyaya mbili, ikiwemo ya intaneti ambazo hutumiwa kwa ajili ya mawasiliano ya simu.

"Moto uliingia moja kwa moja katika jengo letu na kushika seva yetu ambayo tunatumia kwa ajili ya mawasiliano ya simu,” amesema.

"Baada ya kushika nyaya hizo,  moto huo uliambaa amba na kuingia katika chumba cha Tehama na kisha kushika soketi ya umeme iliyopo ndani ya jengo la mahakama.”

Baada ya kutokea kwa hitilafu hiyo ya umeme,  askari polisi walikuwepo mahakamani hapo,  alitumia vidhibiti moto na kufanikiwa kuuzima.

Dakika tano, baada ya kutokea kwa hitilafu hiyo,  gari la zimamoto lilifika mahakamani hapo na kukuta tayari moto huo umezimwa.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live


Latest Images