Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Pata Tiba ya Tatizo la Nguvu Za Kiume........Inasaidia Kukufanya Urudie Mara 5 na kuchelewa kwa Dakika 20

$
0
0
TATIZO LA UPUNGUFU WA NGUVU ZA KIUME NA MAUMBILE MADOGO LINATIBIKA.Baada ya utafiti wa mda mrefu juu ya matatizo ya upungufu wa nguvu za kiume na ukosaji wa hamu ya tendo la ndoa ama kushindwa kurudia tendo kwa haraka DR Magise imekuletea tiba ya matatizo hayo kwa kutumia dawa za: 
 
FULL POWER:Ni dawa asili ya vidonge inayotibu tatizo la upungufu au ukosefu wa nguvu za kiume,dawa hii inamchanganyiko wakutosha wenyekuzalisha vichocheo vingi vya Hemone za Gestrogen vikiwemo vitamin B6&B1,vitamini E,pamoja na madini aina ya zinc vitakufanya kuwa na nguvu na mzunguko mzuri wa damu na kuongeza hamu na uwezo wa kufanya tendo la ndoa zaidi ya hatua nne au zaidi,na kuchelewa kufika kileleni zaidi dakka 20-30.
 
NYAMVA:Inarutubisha maumbile ya uume yani kurefusha na kunenepesha nchi 4-7 upana cm3-4 standard kiafya haijalishi umri wako hata kwa wazee ukiitumia maumbile yako yatabaki kuwa hivyo siku zote,Pia tunatibu Presha,kisukari siku7,ngiri,chango la tumbo tumbo kujaa gesi,kutopata choo vizuri

 TUPO TZ DAR ES SALAAM   MBAGALA RANGI TATU.HUDUMA HII UTALETEWA POPOTE ULIPO .WASILIANA NAMI 0783741788,0715741788 -DR MAGISE

SORRY MADAM -Sehemu ya 92 & 93 (Destination of my enemies)

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
ILIPOISHIA

Sa Yoo akajikuta akishangilia kwa furaha, ila sura ya Madam Mery ikapoteza furaha, na kumfanya Eddy naye kupoteza furaha yake.
“Ina maana hamuniamini au?”  
“Phidaya nina mjua Godwin hawezi kukamatika kiholela kiasi hicho”
Madam Mery alizungumza kwa msisitizo, huku akiwa amemkazia macho madam Mery
“Jamani nimemkuta akiwa amelala chini mguuni amepigwa risasi”
“Kwa nini tubishane twendeni tukamuone”
Sa Yoo akaanza kukisukuma kitanda cha Eddy huku Phidaya na Madam Mery wakiwa wametangulia mbele, huku Shamsa akifwata kwa nyuma. Wakatoka kwenye vyumba hivyo na kwenda nje. Walipo fika kila mmoja akabaki ameduwaa hususani Phidaya kwa maana Raisi Godwin na Rahab wametoweka eneo hilo

ENDELEA
“Wamekwenda wapi?”
Phidaya aliuliza huku macho yakiwa yamemtoka. Madma Mery akajikuta akikaa chini, huku nguvu za mwili zikiwa zimemuishia.
“Tuondokeni eneo hili si salama”
Eddy alizungumza huku akijaribu kukaa kwenye kitanda, maumivu makali aliyo yapata kwenye mbavu zake hayakumzuia kabisa kuweza kunyanyuka na kukaa kitako.
“Utataka kwenda wapi Eddy?”
“Ni bora nyinyi kuondoka kuliko kuingia mikononi mwa askari”

“Unataka kusema kwamba…….”
Phidaya aliuliza huku macho yake akiwa amemtolea Eddy aliye lala kwenye kitanda hicho.
“Ondokeni eneo hili sio salamaa”
Eddy alizungumza kwa msisitizo na kuwafanya  Shamsa kuelewa maana yake ni nini. Shamsa kwa haraka akaingia ndani, moja kwa moja akaelekea katika chumba ambacho walikuwepo. Akachukua mbastola nne zenye magazine zilizo jaa risasi kisha akatoka nje kwa haraka.
“Inabidi kuondoka eneo hili sasa hivi”
“Na Eddy?”
“Mimi mutaniacha hapa, ondokeni”
Taarifa hiyo, ikauingiza moyo wa Phidaya simanzi kubwa sana, kwa maana hakujua ni kwanini mume wake amechukua maamuzi kama hayo. Kwa haraka akamfwata Eddy kitandani na kukumbatiana huku Phidaya machozi yakimwagika, na Eddy machozi yakimlenga lenga.

“Nitakuwa salama”
Phidaya hakujibu kitu cha aina yoyote zaidi ya kuzidi kumwagikwa na machozi, tayari Shamsa alisha ingia kwenye moja ya gari, ambalo ni mali ya ikulu. Madam Mery na Sa Yoo nao wote wakaingia ndani ya gari hilo na kumsubiria Phidaya anaye endelea kumng’ang’ania mume wake.
“Nenda mke wangu nitakuwa salama”
“Niahidi hauto kufa?”
“Nakuahidi, kimbia kabla askari hawajafika hapa”
Phidaya akamuachia Eddy na kumpiga busu la mdomo, kisha akashuka kwenye ngazi hizo kwa haraka na kuingia ndani ya gari, Shamsa ambaye tayari alisha lifungua geti hilo muda alipo kuwa anashuka chini, akakanyaga mafuta ya gari hilo ambalo ni aina ya Aud 5q lenye sifa ya kuto kuingia risasi na ndio gari ambalo hutembelea raisi Godwin.
Kipindi gari hiyo inamalizikia kutoka nje, machozi yakatiririka usoni mwa Eddy ambaye hakuweza kujumuika katika safari hiyo, kwanza kutokana na mshono wa oparesheni aliyo fanyiwa jana tu, pili ni kutokana hajulikani kama yeye ndio Eddy, ila anajulikana kwa jina la Erickson Forrd hii ni kutokana na sura yake.

Hazikupita hata dakika tano, ving’ora vya gari za polisi pamoja na usalama wa taifa vikasikika nje ya nyumba ya Eddy. Alicho kifanya Eddy ni kujilaza kitandani hapo huku machozi yakiendelea kumwagika.
Askari wengi wenye bunduki mikononi mwao wakaingia ndani humo kwa umakini, wakaanza kukagua maiti moja baada ya nyingine.
“Erickson”
Eddy akamuona Manka akimfwata sehemu alipo lala. Taratibu Manka akapiga magoti chini, na kumbusu Eddy mdomoni.
“Nashukuru Mungu nimekupata”
Eddy hakujibu kitu zaidi ya kumwagikwa na machozi usoni mwake. Madaktari wa jeshi walio fika eneo hilo la tukio, wakamchukua Eddy na kumuingiza kwenye gari ya wagonjwa, huku akiambatana na Manka ambaye hakuhitaji kumpoteza tena.

Askari walio baki huku nyuma kazi yao ikwa ni miili ya askari walio pigwa risasi, kati ya askari ishirini walio fika katika eneo hilo, ni mmoja tu ambaye ni mlinzi wa raisi Godwin aliye weza kuwa hai japo hali yake ni mbaya
“Muheshimiwa raisi…..a…me..ch…..u”
Hakumalizia kitu alicho kuwa anakizungumza akapoteza fahamu.
“Muwahisheni hospitalini, huyu atatufaa”
Mkuu wa kitengo cha polisi kanda maalimu bwana Erinest Komba aliwaeleza vijana wake, ambao wakafwata amri kama alivyo zungumza mkuu wao. Habari ya raisi Godwin kutoweka ikaanza kusambaa kwa kasi kupitia mitandao  ya kijamii, huku vituo vya televishion na maredio vikiwa vinatafuta ukweli juu ya jambo hilo. Hapakuwa na mkuu yoyote wa jeshi aliye weza kudhibitihs habari hizo kwa maana hapakuwa na mtu mwenye ushahidi katika hilo.
                                                                                                         ***
“Jikaze usilie, unavyo lia unadhani mimi nitafanyaje?”
Shamsa alizungumza huku akimtazama Phidaya anaye lia njia mzima
“Ila mume wangu atakuwa kwenye matatizo”
“Sio rahisi kwa Eddy kuingia kwenye matatizo ndio maana akatuambia tuondoke”
Muda wote madam Mery akawa kimya akilichunguza gari hilo, kwa bahati nzuri akaona kifaa maalumu ambacho kipo siti ya nyuma ya dereva eneo alilo kaa yeye kinacho weza kuonyesha ni sehemu gani raisi yupo, hata walinzi wake wanapo kaa ikulu.
“Shamsa simamisha gari?”
“Kuna nini?”
“Simamisha gari kwanza”
Shamsa ikambidi kutii kile kitu ambacho madam Mery amemueleza, kwa haraka madam Mery akashaka kwenye gari, akamuomba Shamsa kufungua buti ya gari, Shamsa akaminya batani iliyo ruhusu buti ya gari hilo kufunguka, madam Mery akalinyanyua, akakuta kifaa kidogo kinacho ongoza kifaa alicho kiona ndani ya gari hilo.

“Ohoo ni GPRs system”
Sa Yoo alizungumza mara baada ya kuona kifaa hicho.
“Ndio nini?”
Shamsa aliuliza mara baada ya kushuka kwenye gari na kuzunguka nyuma kwenye buti ya gari hilo.
“Sehemu yoyote  tunapo kwenda nah ii gari lazima tuonekane”
“Sasa inakuwaje?”
Hata kabla Sa Yoo hajajibu swali hilo, wakaziona gari nne nyeusi, aina ya GVC zinazo piga ving’ora zikiwafwata kwa kasi katika eneo hilo.
“Ohooo rudini kwenye gari wote”
Shamsa alizungumza kwa haraka akafunga buti ya gari hilo, wote wakaingia ndani gari, bila ya kupoteza muda, Shamsa akakanyaga mafuta ya gari na kuondoka eneo hilo kwa kasi kubwa.
“Fungeni mikanda”
Shamsa alizungumza huku akifunga mkanda wa siti aliyo kalia. Gari  hizo nne za makachero wa usalama wa taifa, zikazidi kuifukuza gari hiyo ya raisi huku mkuu wao aliye panda gari la mbele akiwa na simu maalumu inayo onyesha gari hilo la raisi kila sehemu anapo kwenda.

“Ongeza mwendo, hawa watu ndio walio mteka raisi”
“Sawa mkuu”
Dereva huyo, ambaye naye ni kachero anaye sifika katika maswala ya uendeshaji wa gari kwa kasi, akawa ndio kama amechochewa, akazidi kukanyaga mafuta kwa kasi, hadi madereva wezake wanao endesha magri matatu yaliyo nyuma yao akawaacha kwa umbali kidogo.
“Wanazidi kutufwata”
Sa Yoo alizungumza huku mara kwa mara akigeuza kichwa chake nyuma. Katika uendeshaji wa gari, Shamsa anajimudu sana, ila kitu kinacho mfelisha kwa wakati huu, ni bega lake lililo pigwa risasi, na ndio kwanza kidonda hakijapona na maumivu anayo yaoata hapo ni makali kupindukia sema tu anajikaza kuwaokoa wezake kwa maana wakiingia mikononi mwa Makachero hao, hakuna mtu mwenye jawabu la kujua ni nini atakacho fanywa.

TANGA RAHA- Sehemu ya Tatu ( 3 )

$
0
0
MWANDISHI: EDDAZARIA G.MSULWA
 ILIPOISHIA  
Nikajipapasa haraka haraka kwenye mifuko yangu, ya pensi niliyo ivaa na kukuta kweli walet yangu haipo, ambayo ndani yake inapesa nyingi pamoja na vitambulisho vyangu vya kazi na bima za afya, tunazopewa wafanyakazi wa serikalini kwa ajili ya matibabu ya bure katika hospital yoyote ndani ya nchi ya Tanzania
"Asante sana dada yangu sijui nikuchukuru vipi sema nikupe nini?"

ENDELEA
"Hapana kaka yangu asante"
"Hapana jamani basi turudi nikakulipie sahani ya chipsi uliyo agizia"
"Nashukuru kaka yangu siku nyingine utanilipia"
Kabla sijazungumza simu ya yule dada ikaita akapokea ikanibidi nikae kimya, nimpe nafasi ya kuzungumza na mtu aliye mpigia
"Halow baby nakuja namalizia kufungia hizi chipsi”
“Jamani mume wangu kuna foleni kama nini"
Akamaliza kuzungumza na simu, na kukata simu
"Kaka yangu Mungu akipenda tutaonana shemeji yako ana wivu sana"
"Sawa nisalimie shemeji yangu kwa maana anafanya kazi sana"
”Kazi gani?” Dada aliuliza huku akitabasamu usoni mwake
“Kazi ya kukutunza, ndio maana ulipo ingia pale tukakukodolea macho”

"Hahaaa, mbona kawaida”
“Kwako ndio kawaida ila sisi, mmmmm”
“Usijali utapata mwenye naniliu kama langu”
"Samahani kama huto jali chukua namba yangu"
Nikamtajia namba zangu kisha akaondoka kwa mwendo wa haraka na kuniacha nimeduwaa nikiyatazama makalio yake makubwa jinsi yanavyo tingishika kama simu ya kichina yenye vibrate kali
"Mmm huku Tanga ni noma"
Nilijisemea kimoyo moya na kuanza kupiga hatua za taratibu za kurudi kwangu mtaa wa pili kutoka ninapo ishi.Nikiwa njiani nikastuka nikiitwa na sauti ya mtoto wa kiume huku akinikimbilia akinifwata sehemu nilipo
"Shikamoo Sir Eddy"
"Marahaba hujambo mtoto mzuri?"
Nikaanza kujiuliza huyu mtoto amenijuaje wakati kwa makadirio ya macho yangu hajamaliza darasa la saba, kutokana na kimo chake pamoja na sura yake bado niyakitoto

"Sijambo"
"Unaitwa nani?"
"Jumaa"
"Jina langu amekuambia nani?"
Kikajichekesha kisha kikanijibu
"Ameniambia dada yangu yule pale nje"
Nikageuka kumtazama sehemu anayo nionyesha nikaona wadada wanne wakiwa wamekaa kibarazani wanacheza karata huku macho yakitutizama kwa kuiba iba, nikawasalimi wakaitikia kwa pamoja
"Haya rafiki yangu nenda kacheze"
"Sir Eddy naweza kuja kutazama DSTV kwako"
Nikajikuta nikiguna kimoyo moyo kwani sijui huyu mtoto amejuaje nimenunua DSTV wakati mimi minaishi mtaa wa mbele kutoka pale

"Mbona usiku labda kesho utakuja si unapajua kwangu?"
"Ndio ila leo kuna mechi za mpira ligi ya uingereza"
"Mmmm unashabikia timu gani?"
"Madrid ila uingereza nashabikia Liverpool"
Sikuwa na jinsi za kumkubalia akawaaga ndugu zake na tukaondoka.Tukafika kwangu nikamuwekea mechi ya mpira anayo itaka kupitia akaanza kuangalia huku akionekana kufurahi sana
Nikafungua kifuko changu cha chipsi nikamkaribisha Jumaa hakufanya makosa akaanza kuokota mskaki huku akiokota na chipsi nyingi
"Leo nitalala njaa"
Nikajisemea kimoyo moyo huku Jumaa akizidi kunichezea rafu kwenye kula hadi tukamaliza kwa hesabu za haraka haraka nimekula chispi kama ishirini tu kati ya nyingi zilizopo kwenye kifuko changu
Nikafungua friji na kumpa Jumaa soda akaonekana kuzidi kufurahi huku akipata midadi ya mpira unao chezwa
"Dogo saa nne huogopi kwenda kwenu?"
"Hapana si hapo nyuma tu"
Ikanibidi nikae kimya,dakika tano mbele mlango wangu ukagongwa huku sauti ya dada nisiye mjua akiita jina la Jumaa

Rais Magufuli Aungana na Wauminii Katika Misa ya Majivu

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akipakwa majivu wakati wa ibada ya Jumatano ya Majivu katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam asubuhi ya leo.


RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli ameungana na waumini wa Kanisa Katoliki na wakristo wengine katika ibada ya Jumatano ya majivu inaoashiria kuanza kwa mfungo mtukufu wa kwaresma.

Magufuli akiwa na mkewe, Mama Janeth Magufuli wameungana na waumini hao katika ibada iliyoongozwa na Muadhama Askofu Mkuu, Polycarp Kardinali Pengo wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam katika Kanisa la Mtakatifu Joseph, Dar, leo Februari 14, 2018.

Rais John Magufuli akisalimiana na Muadhama Askofu Mkuu Polycarp Kardinali Pengo wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam baada ya kujiunga na waumini wengine katika ibada ya Jumatano ya Majivu katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam asubuhi ya leo Feb 14.
Mama Janeth Magufuli akisalimiana na Muadhama Askofu Mkuu Polycarp Kardinali Pengo wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam baada ya kujiunga na waumini wengine katika ibada ya Jumatano ya Majivu katika kanisa la Mtakatifu Joseph jijini Dar es salaam asubuhi ya leo Feb 14.

Serikali kutolea mwongozo matamko ya Makonda na Mnyet

$
0
0
Hatua ya wakuu wawili wa mikoa, paul Makonda na Alexander mnyeti kutoa matamko ya kusimamisha shughuli au kuvunja mabaraza ya kata, Serikali imesema inaandaa mwongozo kuhusu suala hilo.

jumatatu iliyopita, Makonda ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam alitoa tamko la kusimamisha mabaraza hayo katika mkoa wake kabla ya Mnyeti wa Mkoa wa Manyara kutamka kuvunja baraza la Ardhi Kata ya Murray, wilayani Mbulu juzi.

Alipotafutwa jana kuzungumzia hatua ya wakuu hao, katibu Mkuu Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Mussa Iyombe alisema, “tunakamilisha mwongozo kuhusu suala hilo wiki hii, fanyeni subira.”

Uamuzi wa Mnyeti
Mnyeti alitangaza uamuzi huo baada ya kupokea malalamiko ya wananchi kunyanyaswa, kuombwa rushwa na kunyimwa haki.

Akizungumza katika Kata hiyo alisema hawezi kuliacha baraza hilo liendelee kufanya kazi ilhali wananchi wananlalamika kukosa haki.

Alimuagiza mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya mji wa Mbulu, Anna Mbogo kuanza mchakato wa kupatikana viongozi wapya waadilifu wa baraza hilo la kata ili waendelee kuwatumikia wananchi na kuagiza mikutano ya wananchi kuwachagua wajumbe wengine ianze upya.

“Tafuteni watu waadilifu, wenye weledi na hofu ya Mungu, ambao wanaweza kuwahudumia wananchi ili washike nafasi hizo na kutekeleza majukumu yao ipasavyo,” alisema mnyeti.

Hatua ya Mnyeti ilitokana na malalamiko kutoka kwa mkazi wa Murray, Michael Amme kwamba baraza hilo halitendi haki na wananchi wanyonge wanonewa. amme alidai kwamba familia yake iliporwa eneo kutokana na uamuzi wa barazsa hilo.

Mjumbe wa baraza hilo, Verani Anthony alisema wananchi wanapaswa kupatiwa elimu kuhusu utendaji kazi wa baraza hilo kwa kuwa wao hutekeleza wajibu wao ipasavyo.

Kuhusu Makonda
Juzi, iyombe akizungumza kuhusu tamko la Makonda, alisema mkuu huyo wa mkoa alishatoa ufafanuzi kwa maandishi akikana kusimamisha mabaraza hayo kufanya kazi.

“Tulimtaka atuandikie barua ya kutueleza na tayari ameshafanya hivyo, tumemalizana nae kwa maandishi, hakusimamisha mabaraza hayo kufanya kazi,” alisema Iyombe.

Hata hivyo, katibu mkuu huyo alipoulizwa kama Makonda alitakiwa kuandika barua baada ya kuvunja kipengele kipi cha sheria kutokana na tamko lake, alisema

“Sitaki kusema alivunja kipengee ni wewe wasema, ninachokisema wananchi wakielewe, kulikuwa na maswali watu wanahoji kuhusu suala hilo ndiyo maana tukamtaka atufafanulie na amefanya hivyo kwa maandishi.”

Waraka wa Tume
Andiko la Tume ya Kurekebisha Sheria kwenye mapitio ya mfumo wa utoaji haki katika mashauri ya madai, sehemu ya III la Julai 2012 linalopatikana kwenye mtandao linaelezea utekelezaji wa Sheria ya Mabaraza ya Kata ya mwaka 1985.

Linasema mabaraza hayo yanapaswa kuwa chini ya usimamizi wa Serikali za Mitaa na wajumbe huteuliwa na kamati ya maendeleo ya kata. Baraza huongozwa na mwenyekiti anayeteuliwa na halmashauri husika.

Majukumu ya baraza ni kutunza amani kwenye kata, kutatua migogoro, kusuluhisha ndoa na kusimamia utekelezaji wa sheria ndogondogo kama zilivyopitishwa na halmashauri husika. Baraza pia lina uwezo wa kutatua migogoro yote ya ardhi katika kata, iwe ardhi iliyopimwa au isiyopimwa.

Uteuzi wa viongozi wa mabaraza Kwa mujibu wa sheria, uteuzi wa mwenyekiti wa baraza la ardhi na nyumba la wilaya unafanywa na wizara inayohusika na masuala ya ardhi wakati uteuzi wa wajumbe wa baraza la kata unafanywa na halmashauri husika.

Hata hivyo, katika andiko hilo, Tume ilibaini kuwa vyombo vilivyopewa uwezo wa kuajiri au kufanya uteuzi wa nafasi hizo vina mwingiliano wa kisiasa ambao unaweza kuingilia utendaji kazi wa maofisa wanaowateua au kuwashawishi katika uamuzi wanaoyafanya.

Chanzo: Mwananchi

Katibu wa Bunge Azungumzia Afya ya Spika Job Ndugai

$
0
0
Katibu wa Bunge, Stephen Kagaigai amesema hali ya afya ya Spika wa Bunge, Job Ndugai aliyepo nchini India inaendelea vizuri.

Kagaigai amesema leo Februari 14,2018 kuwa Spika Ndugai yupo India kwa ajili ya kuangalia afya yake (check-up) na anatarajiwa kurejea nchini wakati wowote.

Katibu huyo wa Bunge amesema, “Tulikwisha kusema kwamba Spika yuko India kwa ajili ya ‘check-up’ na hali yake inaendelea vizuri.”

Alipoulizwa kuwa Spika atakuwa ughaibuni hadi lini, Kagaigai amesema: “Hilo ni kati ya daktari wake na yeye lakini ninachoweza kusema wakati wowote anaweza kurudi nchini.”

Watatu wakamatwa na Jeshi la Polisi Mkoani Mbeya kwa kukutwa na Meno ya Tembo

$
0
0
Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya limeendelea kufanya misako, operesheni na doria zenye tija katika maeneo mbalimbali ili kudhibiti uhalifu na wahalifu na limekuwa likishirikiana na wananchi na wadau wengine katika jitihada hizo za kukabiliana na uhalifu na wahalifu na kupata mafanikio makubwa ikiwa ni pamoja na kupungua kwa matukio makubwa ya uhalifu.

Aidha Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya limeendelea kukabiliana na matukio makubwa ya uhalifu pamoja na wahalifu. Jitihada zinaendelea kwa kushirikiana na wananchi kuhakikisha mkoa wetu unakua mahala salama. Hata hivyo kumekuwa na matukio kama ifuatavyo:-

KUKAMATWA KWA WATUHUMIWA WATATU WAKIWA NA NYARA ZA SERIKALI.

Mnamo tarehe 05 Februari, 2018 majira ya saa 19:45 usiku huko maeneo ya Mwanjelwa, Kata ya Ruanda, Tarafa ya Iyunga, Jijini Mbeya, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya likiwa katika majukumu yake ya kuhakikisha usalama wa raia na mali zao, limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa watatu wakiwa na nyara za Serikali ambazo ni vipande vinne vya meno ya Tembo.

Watuhumiwa waliokamatwa wamefahamika kwa majina ya 1. KENEDY LUPEMBE SIMSOKWE [43] Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha SAUT – Tawi la Mbeya na Mkazi wa Iyela 2. MATHEW ELIKANA MWANJALA [42] Mpiga picha na Mkazi wa Iyela na 3. SHABAN MKWICHE [24] Mkazi wa Iyunga.

Aidha baada ya kukamatwa na kupekuliwa, watuhumiwa walikutwa na nyara hizo [Vipande vinne vya Meno ya Tembo] ambavyo vina uzito wa kilogram 5 na thamani ya Tshs 33,000,000/=. 

Taratibu za kisheria zinafanyika ili watuhumiwa wafikishwe mahakamani kwa hatua zaidi.

WITO:

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Naibu  Kamishna wa Polisi MOHAMMED R. MPINGA  anatoa wito kwa jamii kuacha tabia ya kuwa na tamaa ya kujipatia utajiri wa haraka kwa kutumia njia za mkato zisizo halali, badala yake wafanye kazi halali ili kupata kipato halali. Aidha Kamanda MPINGA  anatoa rai kwa yeyote mwenye taarifa juu ya  mtu/ watu au kikundi /mtandao wa watu  wengine wanaojihusisha na  matukio ya ujangili wazitoe katika mamlaka husika ili  hatua za kisheria dhidi yao zichukuliwe mara moja.

          Imesainiwa na:

[MOHAMMED R. MPINGA – DCP]

KAMANDA WA POLISI MKOA WA MBEYA.

Rais Mstaafu Mkapa Aongoza Harambee Ya Kuchangia Mfuko Wa Udhamini Wa Kudhibiti Ukimwi

$
0
0
RAIS Mstaafu Benjamin Mkapa amewataka wadau mbalimbali na wananchi kuendelea kuchangia Mfuko wa Udhamini wa Kudhibiti Ukimwi (ATF) kwa ajili ya kukabiliana na ugonjwa huo nchini ambapo zaidi ya sh.milioni 200 zilipatikana.

Mkapa alitoa ombi hilo wakati akiongoza harambee ya kuchangia mfuko huo iliyofanyika Hoteli ya Serena jijini Dar es Salaam jana na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali, wawakilishi wa mashirika ya nje na ndani pamoja na mabalozi wanaowakilisha nchi zao hapa nchini.

“Ni wajibu kwa kila mwananchi na wadau mbalimbali kuendelea kuchangia mfuko huu ili kusaidia mapambano ya Ukimwi hapa nchini na kuwa mapmbano hayo si ya mtu mmoja” alisema Mkapa.

Katika hatua nyingine Rais Mstaafu Mkapa ameiomba Serikali kuendelea kutenga fedha za Ukimwi katika bajeti zake.

Akizungumza katika harambee hiyo Waziri wa Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Walemavu, Mheshimiwa Jenista Mhagama alisema kwamba Serikali itaendelea kusimamia Tume ya Taifa ya Kudhibiti Ukimwi (TACAIDS) katika matumizi ya  fedha hizo.

Mhagama alisema asilimia 60 ya fedha hizo zitatumika kununulia madawa, asilimia 25 itatumika katika kutoa huduma za kinga pamoja na kutoa elimu ya kujikinga na maambukizi mapya ya Ukimwi na asilimia 15 zitatumika  kwa ajili ya uwezeshaji na ufuatiliaji wa programu za Ukimwi.

Mhagama aliongeza kuwa matumizi ya dawa za kufubaza VVU kwa wanawake ni asilimia 92.9 wakati wanaume ni 86.1 na kuwa katika tisini ya tatu kati ya watu wanaoishi na VVU wenye umri wa miaka 15-64 ambao wametoa taarifa kuwa wanatumia dawa za kufubaza VVU asilimia 87.7 ya watu hao inaonyesha kiasi cha VVU kimefubazwa wanawake ni asilimia 89.2 na wanaume ni asilimia 84.

Alisema utafiti huo pia umeonyesha kuwa maambukizo mapya ya VVU (HIV incidence) kwa mwaka kwa watu wenye umri wa miaka 15-64 Tanzania Bara ni asilimia 0.29 ambayo ni sawa na watu 81,000.

Mwenyekiti wa Bodi ya Mfuko huo, Bw. Godfrey Simbeye alisema sekta binafsi imeunga mkono kwa kiasi kikubwa katika kuchangia mfuko huo na kuwa hakutakuwa na matumizi mabaya ya fedha hizo na zitakwenda kutumika kwa kile kilichokusudiwa.

 Mkurugenzi Mtendaji wa Tume ya Kudhibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS), Dk. Leonard Maboko alimshukuru Rais Mstaafu Mkapa kwa kukubali kushiriki kuongoza harambee hiyo na kueleza kuwa Tacaids imekuwa ikiendesha harambee mbalimbali pamoja na kuandaa mashindano ya michezo na viingilio vyake vimekuwa vikiingia katika mfuko huo.

Rais Magufuli amteua Meja Jenerali Yakubu Hassan kuwa Mnadhimu Mkuu wa JWTZ

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 14 Februari, 2018 amemteua Meja Jenerali Yakubu Hassan Mohamed kuwa Mnadhimu Mkuu wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).

Pamoja na uteuzi huo, Mhe. Rais Magufuli amempandisha cheo kutoka Meja Jenerali na kuwa Luteni Jenerali.

Luteni Jenerali Yakubu Hassan Mohamed anachukua nafasi ya Luteni Jenerali James Alois Mwakibolwa ambaye amestaafu.

Aidha, Mhe. Rais Magufuli amewapandisha vyeo kutoka Brigedia Jenerali na kuwa Meja Jenerali wafuatao;
  1.     Brig Jen. J.G. Kingu
  2.     Brig Jen. M.S. Busungu
  3.     Brig Jen. R.R. Mrangira
  4.     Brig Jen. B.K. Masanja
  5.     Brig Jen. G.T. Msongole
  6.     Brig Jen. A.F. Kapinga
  7.     Brig Jen. K.P. Njelekela
  8.     Brig Jen. A.S. Bahati
  9.     Brig Jen. M.E. Mkingule
  10.     Brig Jen. S.S. Makona
Mabrigedia Jenerali wote waliopandishwa vyeo watapangiwa vituo vya kazi baadaye.

Mnadhimu Mkuu wa JWTZ Luteni Jenerali Yakubu Hassan Mohamed ataapishwa kesho tarehe 15 Februari, 2018 saa 5:00 asubuhi Ikulu Jijini Dar es Salaam.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
14 Februari, 2018

Zuma kupigiwa kura ya kutokuwa na imani Alhamisi

$
0
0
Kikao cha wabunge wa chama tawala cha African National Congress (ANC) leo kimepitisha uamuzi kwa kauli moja kuwasilisha hoja ya kupiga kura ya kukosa imani dhidi ya Rais Jacob Zuma siku ya Alhamisi.

Kwa mujibu wa watu kutoka ndani ya kikao hicho, Spika wa Bunge, Baleka Mbete atapanga ratiba kuruhusu chama cha Economic Freedom Fighters (EFF) kuwasilisha bungeni hoja hiyo Alhamisi mchana. Kisha hoja hiyo itafanyiwa marekebisho na wabunge wa ANC.

Vyanzo kutoka ANC vinasema ni Naibu Waziri wa Mawasiliano, Tandi Mahambehlala pekee aliyejaribu kuanzisha mjadala kuhusu jambo hili, lakini alipingwa na wabunge wenzake ambao ni wengi.

Kikao hicho kilifanyika katikati ya mvutano mkubwa wa kisiasa ndani ya chama chenye Serikali ambacho kimeshindwa kumshawishi Rais Zuma kuondoka ofisini kwa hiari.

Mhasibu Mkuu wa ANC, Paul Mashatile ndiye alihutubia kikao hicho siku ambayo watu watatu wanaotuhumiwa katika kashfa ya kuiweka Serikali mfukoni walikamatwa na polisi wa kitengo cha kupambana na ufisadi (Hawks).

Kikosi hicho cha Hawks kilivamia Jumatano asubuhi makazi ya familia ya Guptas ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakinyoshewa kidole kwa tuhuma zinazomkabili Zuma za kuiweka Serikali mfukoni.

Awali kikao hicho kilipangwa kufanyika saa 4:00 asubuhi, lakini kilisogezwa hadi saa 5:00 kwa matarajio kwamba Zuma angehutubia Taifa saa nne.

Hata hivyo, baadaye ilitolewa taarifa iliyoonyesha kwamba Zuma bado hakuwa tayari kuutangazia umma. Kulikuwa na uvumi kwamba Zuma angeweza kutumia fursa hiyo kujiuzulu baada ya ANC kumpa onyo la mwisho.

DPP kutoa uamuzi kuhusu Mhasibu wa TAKUKURU

$
0
0
Jalada la kesi inayomkabili Mhasibu Mkuu wa TAKUKURU, Godfrey Gugai anayedaiwa kumiliki mali zenye thamani ya Sh. Bilioni 3 ambazo haziendani na kipato chake limepelekwa kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa ajili ya kulipitia na kulitolea maamuzi.

Hayo yameelezwa na Wakili wa Serikali, Wankyo Simon mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba wakati shauri hilo lilipokuja kwaajili ya kutajwa.

Wankyo alieleza awali  jalada hilo lilipelekwa kwa DPP ambapo alilipitia na kulirejesha TAKUKURU na kuelekeza baadhi ya maeneo yafanyiwe uchunguzi zaidi.

Alidai kuwa maeneo hayo yamekwisha fanyiwa kazi na jalada limerejeshwa tena kwa DPP kwa ajili ya kulipitia na kulitolea maamuzi.

Wankyo baada ya kuyaeleza hayo aliiomba Mahakama iipangie kesi hiyo tarehe nyingine ili waweze kueleza hali ya upelelezi ikoje.

Kwa upande wa mshtakiwa Gugai alidai kuwa sasa wamefikisha siku 90 hivyo anaomba kesi ipangiwe siku saba ili waweze kujua hali ya upelelezi ikoje.

Baada ya kueleza hayo, Hakimu Simba aliiahirisha kesi hiyo hadi February 21,2018 na kuutaka upande wa mashtaka uhakikishe wanalifanyia kazi jalada hilo kwa kuwa limeanza kuzeeka.

Mbali na Gugai, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni George Makaranga, Leonard Aloys na Yasini Katera. Washtakiwa hao wanaokabiliwa na mashtaka 43 yakiwemo 20 ya utakatishaji fedha haramu, kumiliki mali zisizoendana na kipato na kughushi mikataba ya mauziano ya viwanja katika maeneo mbalimbali.

Malawi Yaonesha Nia Kupata Gesi Kutoka Tanzania

$
0
0
Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani amekutana na Ujumbe wa Mawaziri wawili kutoka Malawi na kuzungumza kuhusu uwezekano wa Malawi kupata Gesi Asilia kutoka Tanzania na Uendelezaji wa pamoja wa Bonde la Mto Songwe kwa ajili ya matumizi mbalimbali ikiwemo uzalishaji umeme.

Ujumbe wa Malawi uliongozwa na Waziri wa Maliasili, Nishati na Madini, Aggrey Masi na Waziri wa Viwanda, Biashara na Utalii, Henry Mussa ambao waliambatana na Balozi wa Malawi nchini, Hawa Ndilowe na wataalam kutoka Taasisi mbalimbali zilizo chini ya wizara zao.

Waziri Kalemani alikutana na ujumbe huo Februari 12, 2018 katika Ofisi za Wizara ya Nishati jijini Dar es Salaam ambapo alielezwa dhumuni la ziara hiyo ya Mawaziri hao wawili kutoka nchini Malawi.

Akizungumza katika mkutano huo, Waziri wa Nishati wa Malawi, Aggrey Masi alisema kuwa Malawi inaupungufu mkubwa wa nishati ya umeme na kwamba jitihada mbalimbali zinafanyika kuhakikisha kiwango cha uzalishaji umeme kinaongezeka.

Alisema umeme unaozalishwa nchini humo kwa sasa ni Megawati 140 pekee huku idadi ya watu ikiwa ni milioni 17 kiasi ambacho alisema kimeshindwa kukidhi mahitaji.

“Sasa hivi tumebaki na megawati 140 peke yake, hali siyo shwari; suluhisho la haraka linahitajika ili kuweka mambo sawa. Imani yetu ni kwa Tanzania kutazama namna ya kusaidia katika hili,” alisema.

Alibainisha kwamba chanzo kikuuu cha uzalishaji wa umeme nchini humo ni maporomoko ya maji na kwamba kutokana na mabadiliko ya tabia nchi, chanzo hicho kimeshindwa kuzalisha umeme wa kutosha kukidhi mahitaji ya kila siku.

Aliongeza kwamba Serikali ya Malawi imeamua kuwa na vyanzo mbadala vya kuzalishia umeme ikiwemo Gesi Asilia hata hivyo alisema hakuna Gesi Asilia inayozalishwa nchini humo na kwamba matarajio yao ni kupata Gesi Asilia kutoka nchini Tanzania.

“Tumefarijika, tumepokelewa vizuri, lengo la ujio wetu ni kubaini uwezekano wa kupata Gesi Asilia kwa ajili ya kuzalisha umeme,” alisema Masi.

Alisema kwamba baada ya tathmini waliyoifanya wamebaini kwamba chanzo cha haraka kinachoweza kuwasaidia kuvuka kwenye upungufu mkubwa wa umeme uliyoikumba nchi hiyo kwa sasa ni Gesi Asilia kutoka nchini Tanzania.

Aliongeza kuwa tayari mwekezaji amepatikana ambaye atazalisha umeme kwa kutumia Gesi Asilia na kwamba atajenga mitambo yake kwenye eneo la Kalonga mpakani mwa Tanzania na Malawi.

Kwa upande wake Waziri Kalemani alisema suala hilo linaweza kujadiliwa baada ya wataalam wa Tanzania kujiridhisha uwezekano wake.

“Tupo tayari kushirikiana, kinachohitajika hapa ni majadiliano ya kitaalam na wataalam wetu waliopo hapa ili kuelewa mwelekeo,” alisema Waziri Kalemani.

Dkt. Kalemani aliwasisitiza wataalam hao kabla hawajafanya majadiliano wanapaswa kuelewa mambo makuu matatu ambayo wingi wa Gesi Asilia iliyopo kwa sasa, matakwa ya Sera ya Nishati na namna ambavyo Gesi hiyo inaweza kusafirishwa hadi huko Kalonga.

“Je tunayo gesi ya kutosha kugawana ama ni ya kutosha kwa matumizi yetu tu? Je Sera inaruhusu suala hilo? Na kama masuala hayo yanakubalika, Je ni vipi tutaifikisha hiyo Gesi huko mpakani?” alihoji Dkt. Kalemani.

Aliueleza ujumbe huo kuandaa mpango wa ombi lao kimaandishi pamoja na kuandika ombi rasmi na kuwasilisha katika utaratibu maalum wa Kiserikali ili majadiliano yafanyike.

Aidha, suala la Uendelezaji wa pamoja wa Bonde la Mto Songwe, Mawaziri hao kwa pamoja walikubaliana kupitia taarifa ya Tume ya Uendelezaji wa Bonde hilo ambayo inaundwa na nchi hizo mbili ili kubaini hatua za kuchukua kwenye kipengele cha kuzalisha umeme.

Miradi inayotarajiwa kutekelezwa katika bonde hilo ni pamoja na ujenzi wa Bwawa la kuzalisha umeme kiasi cha Megawati 180 ambazo zitagawanya sawa kwa nchi hizo, kilimo cha umwagiliaji, (hekta 6,200) usambazaji wa maji kwa wananchi, ujenzi wa miundombinu ya jamii (bararabara, shule, na vituo vya afya).

Miradi mingine ni uanzishaji wa viwanda vidogo na vya kati, uvuvi, utalii na uboreshaji wa mazingira, hususan kuimarisha kingo za mto ambao ni mpaka wa Tanzania na Malawi.

Halmashauri Ya Longido Yapewa Gari La Chanjo

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amemkabidhi mbunge wa jimbo la Longido, Dkt. Stephen Kiruswa gari aina Tunland Double cabin kwa ajili ya kuboresha huduma za chanjo na afya katika jimbo hilo.

Amemkabidhi gari hilo leo (Jumatano, Februari 14, 2018) mbele ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya hiyo,  Bw. Jumaa Mhina na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Longido, Bw. Sabore ole Moloimet.

Waziri Mkuu amesema amekabidhi gari hilo ikiwa ni utekelezaji wa ahadi aliyoitoa alipofanya ziara wilayani Longidi, Agosti, 2017. Gari la kutolea huduma za chanjo lilikuwa ni miongoni mwa changamoto zilizokuwa zinaikabili wilaya hiyo.

Kwa upande wake, Dkt. Kiruswa alitumia fursa hiyo kumshukuru Waziri Mkuu kwa niaba ya wananchi wa Halmashauri ya wilaya ya Longido. “Gari hili ni zuri sana na linahimili mazingira ya wilaya ya Longido.”

“Naishukuru sana Serikali ya Awamu ya Tano kwa kuboresha huduma mbalimbali wilayani Longido zikiwemo za afya na maji licha ya jimbo hilo kukaa muda mrefu bila ya kuwa na mbunge.”

Amesema atahakikisha gari hilo linatunzwa na linatumika kwa ajili ya matumizi yaliyokusudiwa ambayo ni huduma za chanjo na afya pamoja na huduma za mama na mtoto.

Waziri Mkuu: Bil. 161.9 Zimetumika Kuboresha Vituo Vya Afya 170

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema Serikali imetumia sh. bilioni 161.9 kuboresha vituo vya afya 170 nchini pamoja na kugharamia huduma ya Afya ya Mama na Mtoto kwa lengo la kuokoa maisha yao.

Amsema Serikali itaendelea kukarabati na kupanua miundombinu ya kutolea huduma pamoja na kununua vifaa vya kisasa katika Hospitali za Mloganzila, Benjamini Mkapa, Dodoma na Hosptali za Rufaa katika Mikoa na Kanda.

Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Jumatano, Februari 14, 2018) wakati akizindua jengo  jipya la mama na mtoto katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa-Amana iliyopo wilayani Ilala jijini Dar es Salaam.

Jengo hilo la ghorofa mbili limejengwa kwa ufadhili wa kundi la kampuni za AMSONS na lina thamani ya sh bilioni 1.2.

Amesema uzinduzi wa jengo hilo  unakwenda sambamba na azma ya Rais Dkt. John Magufuli za kuimarisha sekta ya afya na kuifanya kuwa miongoni mwa sekta za kipaumbele.

Amesema lengo la Serikali ni kuhakikisha inasogeza huduma za afya karibu na wananchi. “Mfano, Hospitali za Rufaa za Amana, Mwananyamala na Temeke, zimeendelea kuhudumia wagonjwa kutoka Zahanati, Vituo vya Afya vya Serikali, binafsi na vya dini kutoka mikoa jirani ya Pwani, Morogoro na Lindi.

Pia amesema Serikali itaendelea kutekeleza Ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2015 – 2020, kuhusu kuwapatia wananchi huduma bora za afya pamoja na kujenga hospitali nyingine za Rufaa kwa ajili ya Kanda ya Kusini, Kati na Magharibi.

Akizungumzia kuhusu changamoto ya idadi ndogo ya watumishi na ukosefu wa huduma za uangalizi maalumu (ICU) katika hospital ya Amana, Waziri Mkuu amesema Serikali inaendelea kufanyia kazi changamoto zote zilizopo katika sekta ya afya zikiwemo n aza hospital hiyo.

Waziri Mkuu amesema Serikali itaendelea kuthamini na kutambua mchango wa wadau mbalimbali pamoja na kuendelea kushirikiana nao katika kuhakikisha kuwa huduma za afya nchini zinaboreshwa.

Hivyo, alitumia fursa hiyo  na kulipongeza kundi la kampuni za AMSON’s lililoamua kujenga jengo la mama na mtoto katika hospital hiyo kwa ushawishi wa Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Paul Makonda.

Awali, Mganga Mkuu Hospitali ya Rufaa ya Mkoa – Amana, Dkt. Meshack Shimwella alisema wazazi wanaolazwa katika hospitali hiyo kwa siku ni 180 hadi 250 na uwezo wa hospitali ni vitanda 353, ambapo vitanda 250 vinatumika wodi ya wazazi.

Alisema idadi hiyo hailingani na idadi ya wagonjwa, hivyo kusababisha wakati mwingine wagonjwa kulala zaidi ya mmoja kwenye kitanda kimoja kutokana na kasi ya ongezeko wa wagonjwa wanaolazwa hususani wodi ya watoto na akinamama.

Dkt. Shimwella alisema wamefanikiwa kuongeza jingo la kutolea huduma ya mama na mtoto lenye ghorofa mbili ilililojengwa kwa ufadhili wa AMSONS lenye uwezo wa vitanda 100, ambalo ndilo liliongeza idadi ya vitanda kutoka 253 hadi kufikia 353.

“Kutokana kukamilika kwa jengo hilo kwa sasa akinamama wanaonyonyesha wanalala wakiwa mmoja mmoja, watoto wachanga wanahudumiwa katika mazingira mazuri yanayofanana na viwango Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto.”

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Bw. Makonda aliwashukuru wafadhili waliojenga jengo hilo kwa sababu si kila mtu anayekwenda hospitali na kukuta changamoto na akaamua kuzifanyia kazi.

Bw. Makonda alisema awali akinamama walikuwa wanalala hadi watatu katika kitanda kimoja, hivyo madhumuni ya ujenzi wa jego hilo ni kupunguza msongamano katika wodi ya wazazi.

Mwigulu Nchemba awakemea wanasiasa wanaoihusisha Serikali na kushambuliwa kwa Tundu Lissu

$
0
0
Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Dkt. Mwigulu Nchemba amewataka wanasiasa kuacha kutumia kuumia kwa mbunge Tundu Lissu kama chambo ya kisiasa katika majukwaa.

Dkt. Mwigulu amesema hayo jana mkoani Singida wakati wa kampeni za udiwani kata ya Mitunduluni.

Mwigulu  amewataka wanasiasa  waache kutumia matatizo ya ndugu yao kama mitaji ya kisiasa badala  yake waje na hoja za maana za kusaidia katika maendeleo ya nchi.

Aliongeza kusema kuwa mwaka uliopita uhalifu wa ajabu ulitokea ambapo kuna watoto wadogo wa chekechea walitekwa na kuuwawa ambao hawakuwa  hata na  shida na mtu yoyote na wazazi wao ni watu wa kawaida kabisa je serikali ndio imehusika.

“Sisi tunaoshughulika na maswala ya uhalifu tunatafuta wahalifu wanaofanya maswala ya kihalifu, kuna watu wanaona ni ajenda ya kisiasa wakati sisi tunaombea mtu apone” alisema Dkt. Mwigulu

Dkt. Mwigulu ameongeza na kusema kuwa je angeamua kuendelea  kusema kuhusu kupigwa risasi kwa mwanajeshi masaki inauhusiano gani na shida za kata ya Mitundulini, hivyo wananchi wa Singida wawaadhibu kwa kuwanyima kura katika uchaguzi wa tarehe 17 mwezi huu.

Uchaguzi mdogo katika kata ya Mitunduluni unafanyika baada ya Diwani aleyekuwepo katika kata hiyo kufariki dunia kwa maradhi.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Alhamisi ya February 15

Zari atangaza kuachana na Diamond

$
0
0
Zarinah Hassan maarufu kama Zari ama Zari The Boss Lady ametangaza kuachana na mzazi mwenzake, Naseeb Abdul maarufu Diamond Platnumz kufuatia kuwapo kwa tuhuma nyingi kuhusu mwanamuziki huyo kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wasichana wengine.

Zari ametangaza uamuzi huo kupitia ukurasa wake wa Instagram ambapo amesema kuwa kumekuwapo na tuhuma na wakati mwingine kuna uthibitisho katika mitandao kuhusu tabia ya mara kwa mara ya Diamond kuchepuka, na hivyo ameamua kuachana na kwa sababu heshima yake, utu wake haviwezi kuharibiwa.

Zairi amesema kwamba anaachana na Diamond kama mpenzi wake lakini wataendeleaa kuwa wazazi wenza.

Aidha, katika waraka wake, Boss Lady amesema kuwa, tukio hilo halitapunguza namna anavyowajali wanae, na Zari ambaye amekuwa akifahamika kwa kujituma siku zote.

Zari ametangaza uamuzi wa kuachana na Diamond jana wakati watu wakisherehea siku ya wapendanao, ambapo wengi wameigeuza na kuwa siku ya wapenzi ambapo kila mmoja anajaribu kumuonyesha mwenzake namna anavyompenda kwa kufanya mambo mbalimbali.

Zari ameandika;
Understand that this is very difficult for me to do. There have been multiple rumors some with evidence floating around in ALL SORTS of media in regards to Diamond’s constant cheating and sadly I have decided to end my relationship with Diamond, as my RESPECT, INTEGRITY, DIGNITY & WELL BEING cannot be compromised.

We are separating as partners but not as parents. This doesn’t reduce me as a self-made individual, and as a caring mother, and the boss lady you have all come to know.

I will continue to build as a mogul, i will inspire the world of women to become boss ladies too. I will teach my four sons to always respect women, and teach my daughter what self-respect means. Unlike many, I’ve been in the entertainment industry for 12 years, and through all my challenges I came out a victor because I am a winner, and so are all of you Zari supporters.

HAPPY VALENTINE’S.

BREAKING: Morgan Tsvangarai Afariki Dunia

$
0
0
Kiongozi mkuu wa upinzani nchini Zimbabwe Morgan Tsvangirai amefariki dunia nchini Afrika kusini.

Kwa mujibu wa kiongozi Mwandamizi wa chama cha MDC, Tsvangirai mwenye umri wa 65, na aliyewahi kushika nafasi ya Uwaziri mkuu nchini Zimbabwe ameripotiwa kuwa alikuwa akisumbuliwa na Saratani ya utumbo.

Makamu Rais wa chama chama cha MDC Elias Mudzuri ameliambia Shirika la Habari la Uingereza Reuters kwamba marehemu alifariki jioni ya Februar 14.

Katika kipindi cha uhai wake, maisha yake ya kazi yaligubikwa na harakati nyingi za kisiasa dhidi ya mpinzani wake Rais wa zamani wa Zimbabwe Robert Mugabe.

Aliwahi kupigwa na kufungwa mara kadhaa.

Morgan Tsvangirai alianzisha chama cha Movement for Democratic Change -MDC- mwaka 2000, na kuanza kutoa changamoto kwa Rais wa zamani wa nchi hiyo aliyekaa madarakani muda mrefu.

Kufuatia kifo hicho Bwana Tsvangirai . MDC inaelekea kugawanyika juu ya nani atakayeongoza uchaguzi hapo baadaye mwaka huu dhini ya chama tawala cha Zanu PF, ambacho kwa sasa kinaongozwa na Emmerson Mnangagwa.

BREAKING: Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini Ajiuzulu

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini, Jacob Zuma ametangaza kujiuzulu nafasi yake, baada ya kushinikizwa na chama chake cha African National Congress (ANC).

Kamati Kuu ya ANC ilikutana Jumanne na kumtaka Rais Zuma ajiuzulu kabla ya kuisha kwa siku ya Jumatano, kutokana na tuhuma mbalimbali za rushwa zilizokuwa zikimkabili.

Mapema jana  mchana Rais Zuma alifanya mahojiano na kituo cha runinga cha Afrika Kusini na kusema kwamba hawezi kujiuzulu kwa sababu wale wote wanaomtaka ajiuzulu hawajaweza kumwambia ni kosa gani amefanya.

Kama Rais Zuma asingejiuzulu, Bunge la nchi hiyo leo Alhamisi lingepiga kura ya kutokuwa na imani na Rais, ambapo kama matakwa ya sheria yangetimia, basi Rais Zuma angeng’olewa madarakani.

Akilihutubia taifa, Rais Zuma amesema kwamba hataki kuona chama tawala, ANC kinagawanyika ikiwa chanzo ni yeye, hivyo ameamua kujiuzulu nafasi hiyo aliyoitumikia tangu mwaka 2009.

Rais Zuma aliingia madarakani baada ya mtangulizi wake Thabo Mbeki kujiuzulu kufuatia kushinikizwa na chama chake.

Kufuatia kujiuzulu kwa Zuma, kiongozi wa ANC, Cyril Ramaphosa anatarajiwa kuapishwa kuchukua nafasi ya kuliongoza taifa hilo.

Licha ya kuchukua uamuzi wa kujiuzulu, Rais Zuma amesema kwamba hakubaliani na namna ANC walivyoshubghulikia suala lake, kwani kwa miaka yote aliyokuwa madarakani amewatumikia raia wa Afrika Kusini kwa uwezo wake wote.
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images