Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Upatikanaji wa dawa waongezeka na kufikia asilimia 95

$
0
0
Serikali yasema upatikanaji wa dawa katika hospitali, zahanati na vituo vya afya vya hospitali umefikia asilimia 95 kutoka ilivyokuwa awali 80% huku ikibainisha kuwa bei ya dawa kushuka kwa 40%.

Serikali imesema utekelezaji wa ujenzi wa barabara ya juu ya Tazara Fly Over umefikia asilimia 70 ambapo unatarajiwa kukamilika mwezi Oktoba mwaka huu.

Serikali imesema kuanzia mwezi Juni au Julai mwaka huu itaanza ujenzi wa barabara za juu (FlyOver) kwenye makutano ya barabara za Chang’ombe, Uhasibu, Kamata, Morocco, Mwenge, Magomeni na Tabata, ujenzi huo utasaidia kuondoa changamoto ya foleni jijini Dar es Salaam.

Awamu ya pili ya mradi wa mabasi ya mwendo kasi jijini Dar es Salaam unatarajiwa kuanza mwaka huu, mradi huo utahusisha ujenzi wa barabara za mwendokasi za Kilwa hadi Mbagala, na Uhuru hadi Gongo la Mboto.

Serikali imepanga kubadilisha mfumo wa masoko ya mazao mbalimbali kwa kuanzisha Soko la Kimataifa la Bidhaa za Kilimo.

Wahamiaji Walowezi Watakiwa Kujiorodhesha Uhamiaji

$
0
0
IDARA ya Uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam imewataka  wahamiaji walowezi kujiorodheshwa katika ofisi zao za uhamiaji  wilaya.

Lengo ni kwamba baada ya kufanya hivyo watapewa vibali vya ukaazi vitavyowafanya kuishi nchini kwa mujibu wa sheria , kanuni na taratibu.

Hayo yamesemwa jana  jijini Dar es Salaam,  na Naibu wa Idara ya Uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam, Petro Malima na kuwa zoezi la  uandikishaji wahamiaji walowezi ni la nchi nzima.

“Hivyo kwa wahamiaji walowezi lazima wajiorodheshe kwa kuwa na picha tatu za Paspoti zilizo katika wakati na wenye watoto wanatakiwa kuwa na picha tatu hizo”, alisema.

Aliongeza kwa wale wataofanya hivyo watatambulika na kuendelea kuishi nchini bila kusumbuliwa kuhusu masuala ya uhamiaji na kutofautisha na wakimbizi na wahamiaji haramu.

Malima alisema wageni wote wanatakiwa kuitikia mwito huo wa Serikali pamoja na wale ambao wanaishi nchini na  kufanyakazi au biashara kinyume na sheria za nchi wanatakiwa kufika katika ofisi za wilaya ili  kuhalalisha ukaazi na kupewa vibali vinavyostahili kwa mujibu wa sheria za nchi.

Alisema  yeyote atakayejificha katika mchakato huo na baadaye kubainika anaishi kinyume cha cha sheria hatua kali zitachukuliwa.

Hatua hizo ni pamoja na kufukuzwa nchini mara moja au kufikishwa mahakamani kwa makosa ya kukiuka sheria.

Aidha Malima alisema kuna matapeli wamekuwa wakiwasumbua wageni wanaoingia nchini kwa kudai wao ni askari au maofisa wa uhamiaji na wakiwa hawana hata sare.

“Viongozi wetu wanajitahidi kwa kila hali kuitangaza nchi yetu na kuvutia wawekezaji sisi uhamiaji Dar es Salaam hatuwezi kukaa kimya na kuona hii ni nia njema ya Serikali inaharibiwa na watu wachache wasiotakia mema nchi yetu."

Tazama Hapa Msimamo,vinara Wa Mabao Na Kutoa Pasi Za Mabao Ligi Kuu Ya Vodacom Tanzania Bara

Uhamiaji Yawachunguza Watoto Watatu Raia Wa Rwanda Kwa Kuingia Nchini Bila Kibali

$
0
0
Na Jumbe Ismailly, Singida
IDARA ya Uhamiaji Mkoa wa Singida inawashikilia kwa uchunguzi watoto wa kike watatu raia wa  Rwanda wenye umri chini ya miaka 18 kwa tuhuma za kuingia nchini kinyume cha sheria.

Kaimu Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Singida,Kamishna Msaidizi, Angela Shija amesema watoto hao wenye umri kati ya miaka 9 na 13 walikamatwa Januanri 30,mwaka 2018 wilayani Manyoni.

Amesema walikuwa  wakitokea nchini Rwanda wakielekea nchini Zambia kuwaona wazazi wao.

“Januari 30 mwaka 2018,  ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Singida ilifanikiwa kuwakamata watoto wa kike watatu raia wa Rwanda.

“Walikamatwa wilayani Manyoni mkoani Singida wakiwa kwenye basi namba T 265 BFY mali ya Kampuni ya Katagi,” amefafanua Kamishina huyo msaidizi

Kwa mujibu wa Ofisa Uhamiaji  Idara ya Uhamiaji ilifanikiwa kuwakamata watoto hao kutokana na taarifa za raia wema na watoto hao wamedai wanaelekea nchini Zambia kuwaona wazazi wao.

Hata hivyo Kamishina Msaidizi huyo wa Jeshi la Uhamiaji aliweka bayana kuwa Idara ya Uhamiaji mkoani Singida inaendelea na uchunguzi ili kubaini watu waliojihusisha na biashara hiyo ya   usafirishaji wahamiaji haramu.

Aidha Kaimu Ofisa Uhamiaji Mkoa wa Singida ametoa mwito kwa wananchi  kujenga utamaduni wa kutoa taarifa kwenye ofisi zao au kwenye vituo vya polisi vilivyo karibu mara wanapowaona watu wasiowafahamu.

Amefafanua kuwa taarifa hizo zitaisaidia  Uhamiaji kufanyia kazi za kubaini matukio ya watu wa aina hiyo na kuwachukulia hatua za kisheria.

Amesisitiza baada ya uchunguzi kukamilika na kuwabaini waliohusika katika biashara hiyo ya kuwasafirisha,na kwa sababu wana umri chini ya miaka 18,watoto hao watarudishwa nyumbani kwa wazazi wao nchini Rwanda.

Sakata la Msamaha wa Babu Seya na Mwanaye Laibuka Bungeni

$
0
0
Mbunge wa Temeke kwa tiketi ya (CUF) Mhe. Abdalah Mtolea ameibua sakata la kusamehewa Babu Seya na mwanae, Johnson Nguza 'Papii Kocha' na kusema halikuwa jambo jema kwa kuwa watu hao mahakama iliwabaini kuwa ni wabakaji.

Mtolea amesema hayo jana Februari 7, 2018 akiwa bungeni na kudai kitendo cha watu hao kuachiwa na kupewa heshima na Serikali ikiwa pamoja na kuwapandisha kwenye majukwaa mbalimbali na kuwapa ufadhili haileti picha nzuri kwa jamii.

"Kwenye maadhimisho ya Uhuru wa Tanganyika ukatoka msamaha kwa Babu Seya na wenzake watu ambao pasipo na shaka mahakama zilithibitisha kwamba hawa watu ni wabakaji sasa tunapokuwa tunasamehe wabakaji uko wapi ulinzi wa watoto wa taifa hili,tunawapandisha kwenye majukwaa wafanye show yaani tunawaona kwamba ni kioo cha jamii je wanafundisha nini? Alihoji

Mhe. Mtolea aliendelea kusema kuwa "Je, mnataka kwamba siku ya mwisho tukiwauliza watoto ukiwa mkubwa unataka kuwa kama nani aseme nataka kuwa mbakaji?

Babu Seya na mwanaye Papii wanategemea kuachia kazi yao mpya muda si mrefu baada ya kuiaanda mara tu baada ya kupewa msamaha na Rais John Pombe Magufuli

Sakata la Pasipoti Mpya Lazidi Kunoga......Uhamiaji Yawatuhumu Wanasiasa, Yawataka Wananchi Wawapuuze

$
0
0
IDARA ya uhamiaji nchini imewataka watanzania kupuuza habari zinazozagaa kuhusu uvumi wa pasipoti mpya kuwa zimechakachuliwa.

Kauli hiyo imetolewa  jana na Kamishna Jenerali wa Uhamiaji nchini, Dkt. Anna Makakala  jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na waandishi wa habari.

Alisema wananchi wanatakiwa kupata taarifa sahihi kila mara juu ya kila jambo linalohusu maendeleo yao na mambo yanayoletea ustawi wa Taifa , na kwamba wao Idara ya Uhamiaji  ndio wenye taarifa sahihi zinazohusu Mchakato mzima wa Pasipoti Mpya za Kielektroniki
 
Hivi karibuni Rais Dkt. John Magufuli wakati akizindua hati mpya za kusafiria alisema kumekuwapo na wahujumu wa mchakato huo ambao hawakufanikiwa kuiba sh. bilioni 400.
 
Alisema kumekuwapo na watu waliozunguka kila kona na kutumia kila njama zote kupiga vita mchakato huo wakidhani watafanikiwa kuhujumu serikali.
 
Dkt. Anna Makakala alisema hatua hizo za kutoa na kueneza taarifa zisizo sahihi zinawaletea mkanganyiko wananchi na kudhoofisha mawazo na fikra chanya kwa Taifa lao
 
Alisema ni vyema jamii ikatambua kuwa mchakato wa Pasipoti mpya ya kidigitali ni hatua kubwa kwa Taifa hili na si vyema kuutolea Taarifa zisizo sahihi. Aliwasihi wanahabari kupata taarifa kutoka katika vyanzo sahihi na kuzifikisha kwa walaji ambao ni Wananchi.
 
Alisisitiza hatua ya mafanikio ya matumizi ya hati hizo hazitarudi nyuma kwa sababu ya kuwapo na taarifa zisizo sahihi zenye lengo la kupotosha ukweli wa mchakato huo.
 
“Ni vyema jamii kuelewa kazi ya hati hizo ni kulinda usalama wa nchi yetu, hivyo Uhamiaji tutaendelea kudhibiti mipaka ya Tanzania na kulinda usalama wa nchi kwa kuwezesha jamii na raia wa kigeni kufuata taratibu katika utokaji,ukaaji na uingiaji wa kila mmoja,” alisema Dkt. Makakala.
 
Alisema kila nchi yenye kuhitaji maendeleo ni muhimu kutumia hati ya kusafiria ya kielektroniki ili kufikia mabadiliko ya sayansi na teknolojia.
 
“Mabadiliko ya kidunia katika maendeleo yanatuonyesha wazi kuwa Taifa hili limefikia kuwa na hati za kisayansi na kiteknolojia hivyo katika hati mpya,mtu yeyote hataweza kutumia ujanja au kughushi na kutumika kwa matumizi yasiyo sahihi,” alisema Dkt. Makakala.
 
Alisema anaamini idara hiyo haitashindwa na wachache wanaokubali kutumika kuhujumu mchakato huo kwa maslahi binafsi kwakuwa kushindwa kwa mchakato huo ni kupunguza hadhi ya usalama wa nchi.
 
“Pasipoti ndio kitu kinachotuwezesha kudhibiti wanaoingia nchini na kutoka, hiki ni kitambulisho cha raia sehemu yoyote duniani wenye Pasipoti za Tanzania ni mabalozi wa Tanzania.

" Mfumo huu utawezesha kudhibiti ujanja wote unaotumika, kutakuwa na cheap na security features nyingi. Sifa ya Taifa letu dunia imeharibika lazima kufanya maamuzi kwa maslahi ya Taifa letu,” alisema.
 
Dk. Anna alisema kufanikiwa kwa mradi huo wa e-Immigration kwa gharama ya dola za Marekani milioni 57 imekuwa mwiba kwa vigogo walioondolewa Uhamiaji na sasa wanahaha kwa aibu wakidai kwamba gharama iliyotajwa ni kwa ajili ya mradi mmoja tu wa e-Pasipoti.
 
“Ni wajibu wa kila mtanzania kuwa macho na wale wote wanaotumiwa na mafisadi kwa ajili ya kuichafua serikali kwakuwa imezuia na kupambana na uhujumu uliotaka kujitokeza,” alisema.
 
Alisema hati hizo zitawezesha waliopotelewa na hati zao kutumia mfumo wa kiteknolojia na kupakua app yake hata katika simu ya mkononi, hivyo kutambulika na kupewa msaada haraka kokote duniani.
 
Alisema hati hiyo inaviwango vyote vya ubora wa kimataifa pia itatumika kama kitambulisho kwa nchi za Afrika Mashariki.

Asilimia 2.7 Ya Wafungwa Wanaishi na UKIMWI

$
0
0
Asiilimia  2.7 ya wafungwa na mahabusu waliopimwa virusi vya Ukimwi (VVU) kwa mwaka 2016/17 wamegundulika kuwa na virusi vya ugonjwa huo.

Matokeo hayo yamebainika baada ya Jeshi la Magereza kuwapima Ukimwi wafungwa na mahabusu 34,793. Kati yao, wanawake ni 1,451 na wanaume ni 33,342.

Akiwasilisha bungeni mjini hapa jana taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ukimwi, Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Jasmin Bunga, alisema wafungwa waliokutwa na maambukizi ni 953 (asilimia 2.7), akibainisha kuwa wanaume ni 818 na wanawake 135.

Alisema kamati yake pia ilielezwa kuwa jeshi hilo katika mwaka 2015/16 waliwapima wafungwa na mahabusu 8,287 na kati yao, waliokutwa na maambukizi ya Ukimwi ni 376, sawa na asilimia 4.5.

"Kamati ilipokea taarifa kuhusu hali ya maambukizi ya VVU magerezani pamoja na upatikanaji wa kinga na tiba ya magonjwa nyemelezi," alisema na kufafanua zaidi:

"Katika mahojiano hayo, kamati ilielezwa kuwa Jeshi la Magereza lina jukumu la kuhakikisha wafungwa na mahabusu wanapata huduma bora za afya kama ilivyo kwenye jamii nyingine."

Vilevile, alieleza kuwa kamati yake ilielezwa uwapo wa msongamano wa wafungwa na mahabusu unaoathiri huduma bora kwa wafungwa, akibainisha kuwa kwa sasa kuna wafungwa na mahabusu 39,312 wakati uwezo wa magereza ni kuhifadhi wafungwa na mahabusu 29,552.

Kutokana na hiyo, Bunga alisema kamati yake inashauri serikali itumie adhabu mbadala kwa makosa madogo kwa kuwa kufanya hivyo kutapunguza msongamano, gharama kwa serikali na uwezekano wa kuambukizana magonjwa ya homa ya ini, Ukimwi na kifua kikuu.

Alisema kamati yake pia ilitaka kutolewa elimu ya mara kwa mara ili wafungwa na mahabusu wapate uelewa namna ya kupambana na janga la Ukimwi pamoja na wapatiwe chanjo ya kuzuia ugonjwa wa homa hatari ya ini.

"Shughuli zozote zinazohusu dawa za kulevya na Ukimwi magerezani, uongozi wa magereza uwahusishe waratibu wa Ukimwi na dawa za kulevya wa mikoa na wilaya ili kubadilishana uzoefu na elimu," alisema.

Kiongozi huyo wa kamati pia alisema wamebaini kuna upungufu wa dawa aina ya Septrine ambazo ni muhimu kwa watu wanaoishi na VVU (WAVIU).

Kutokana na changamoto hiyo, alisema kamati yake inaishauri serikali kuhakikisha dawa hizo zinazotumika kupambana na magonjwa nyemelezi, zinapatikana kwa wingi na ziingizwe katika orodha ya dawa za ARVs ambazo wanapewa WAVIU ili kufubaza makali ya VVU na kuepusha magonjwa nyemelezi.

Bunga pia alisema kamati yake imebaini kampeni za mwitikio wa masuala yanayohusiana na VVU na Ukimwi ni kama zimekufa na hivyo watu sasa wanafanya ngono zembe bila hofu.

Alisema ukimya huu umesababisha watu kujisahau na hivyo kufanya ngono zembe, hali ambayo inaweza kuleta mfumuko mkubwa wa maambukizi mapya ya VVU.

"Kamati inashauri serikali kuwa na mikakati kuhakikisha kamati za kudhibiti Ukimwi katika kila ngazi zinafanya kazi ipasavyo," alisema.

Kutana na Mtaalam wa Kutafsri Ndoto Yoyote...Anasafisha Nyota na Kutoa Mikosi

$
0
0
SHEIKH SHARIF OMARY
Wasiliana na Mtaalam Huyu Kwani yeye hufaulu Pale wote waliko Shindwa na Pia Humaliza kazi zilizo Shindikana ama Zilizo Achwa ndani ya Siku Moja 1.
 
SHEIKH SHARIF ANAWASHUKURU WALE WOTE WANAOPIGA SIMU ZA SHUKRANI NA KUTOA SHUHUDA JINSI TIBA ZAKE ZINAVYO SAIDIA(Rudisha Mahusiano yako Ndani ya Saa 12 tu)
 
SHEIKH SHARIF ni Mtabibu wa Nyota za Binadamu na Dawa za Asili Mwenye Uwezo wa Kubaini Tatizo lako tu Pindi Utakapo Fanya Mawasiliano Kupitia Wasaa Husika.
 
(NA ANATIBU KWA NJIA YA SIMU UKIWA NCHI YOYOTE MKOA WOWOTE ENDAPO UTAFATA MAELEKEZO YAKE..)
Je Unasumbuliwa na Mapenzi..?
 
Umeachwa na UMPENDAE Awe Mume/Mke na Bado Unampenda
Je Umejaribu Sehemu Nyingi Bila Mafanikio?
Mpigie Simu sasa Hivi Ujionee Muujiza wa Papo kwa Papo..
Anauwezo wa Kurudisha Mahusiano yako na Kuimarisha NDOA Ndani ya saa 12 tu.
 
Je Umekimbiwa na Mumeo/Mkeo au Mpenzi na Anaishi na Mtu Mwingine..?
Muone akutatulie Anauwezo wa Hali ya Juu wa Kusambalatisha Mahusiano yao (Mfarakano/Kimavi) Endapo Utafata Atakacho Kuelekeza.
 
Je Una Mpenzi wako ana Pesa na unataka Kumkamata? Muone SHEIKH SHARIF Atamfanya Atimize Ahadi zote Ndani ya Muda Mfupi..
SHEIKH SHARIF Anatumia Jina La Muhusika au Picha Kumaliza Tatizo..
 
Anatibu Kutumia QUR_AN DAWA ZA ASILI YA AFRICA, Dawa za KIARABU NA MAJINI..
ANATAFSIRI NDOTO. ANAPANDIKIZA NYOTA YA KUSHINDA BAHATI NASIBU, KUSAFISHA NYOTA NA KUKUPA MVUTO WA AJABU, KUTOA NUSKI NA VIFUNGO MBALIMBALI.
 
ZINDIKO ZA NYUMBA NA BIASHARA.. PETE ZA BAHATI.. HUMALIZA KABISA TATIZO LA NGUVU ZA KIUME NA KUREFUSHA UUME KWA SAIZI UNAYOTAKA. HUZUIA CHUMA ULETE KWENYE BIASHARA. HURUDISHA MALI ZILIZOPOTEA..
 
MAGONJWA SUGU, MIGUU KUWAKA MOTO AU KUFA GANZI, HUTIBU BUSHA BILA KUPASUA..ANAO UWEZO WA KUMRUDISHA ALIE MBALI AU ALIECHUKULIWA MSUKULE..
 
Humaliza Kesi ya Aina Yoyote Ndani ya Siku 7 tu..
Hutoa Jini la MALI kwa wale Wanao Hitaji Utajiri Bila Masharti..
 
Mawasiliano ..+255 743 203 171

Tiba Asili ya Kuondoa Chunusi, Kupunguza Tumbo, Maziwa Makubwa na Nguvu za Kiume

$
0
0
Asilimia 90 ya wanaume hushindwa kufanya tendo la ndoa kikamilifu kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo za kiafya  kama vile kisukari, punyeto ambayo huathiri mfumo mzima wa wa misuli inayozalisha vichocheo ashiki , kutopata choo vizuri hali ambayo huchakiwa na kula chakula kisicho na asili,tumbo kuunguruma, kujaa gesi,kiuno kuuma, mgongo na miguu kufa ganzi

SUPER HOLO; Ni dawa itokanayo na miti shamba, ipo katika mfumo wa vidonge na unga. Hutibu na kumaliza tatizo la upungufu wa nguvu za kiume kwa muda mfupi tu.,SUPER HOLO hurudisha heshima ya ndoa, itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa dakika 15-30. Itakupa hamu ya kurudia tendo la ndoa zaidi ya mara 3. Pia itaimarisha misuli iliyosinyaa na kulegea. Dawa hii hutumiwa kwa watu wa umrii wa miaka 20- 80

NZOGIWE ni dawaya maumbile.Hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo urefu wa nchi 4-8 na unene wa sentimita 2-4 za upenyo

NZOGOMA ni dawa asili ya miti shamba, huboresha mbegu za uzazi...huzibua mirija na kusafiisha ili kuweza kushika mimba au kutia mimba.

Pia tunayo dawa ya kupunguza tumbo, unene, maziwa makubwa, kuongeza hips, makalio na kutoa chunusi

TUNAPATIKANA MTONI MTONGANI. KANA HAUNA NAFASI YA KUFIKA UTALETEWA ULIPO. WASILIIANA NA DR. MBUSI.  PIGA SIMU NAMBA:   0718 431222

Huna Sababu ya Kuaibika Tena.....Jipatie Dawa Asili ya Tatizo la Nguvu za Kiume

$
0
0
Matatizo ya nguvu za kiume  yamekua yakiathiri watu wengi sana kisaikologia hasa baada ya kujiona wakotofauti sana na wengine, kawaida mwanaume anatakiwa awe na uume kuanzia nchi (6-8) vinginevyo mtuhuyo anamatatizo.

Zipo sababu nyingi zinazosababisha tatizo hili, chango :- hushambulia never ambayo huasili misuli ya uume, Ngiri :- hii huleta maumivu ya tumbo chini ya kitovu na kufanya tumbo kuunguluma na kujaa gesi, kolodani moja kuvimba au kuingia ndani pamoja na kutopata choo vizuli Sababuhizi na nyingine hufanya uume kulegea na kusinyaa na kuwa mfupi na mwembamba namarakwamara husababisha kukosa hamu ya kuludia tendo la ndoa na baadae kukosa kabisa

MIHINI:- Nidawa ya vidonge iliyotengenezwa kwa mitishamba, huongeza nguvu za kiume maradufu kuanzia umri wa miaka (15-80) inakomaza mbegu zisizo na viini vya uzazi (manii) ,inaimalisha mishipa iliyolegea wakati wa tendo la ndoa, itakufanya uwe na hamu ya kuludia tendo la ndoa zaidi ya maratatu bilahamu kuisha wara kuhisi kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kilelen Kwa mda wa dk (18-25).

SUNUPER :- hurefusha na kunenepesha maumbile madogo ya uume uliosinyaa inchi 6-8 na unene wa sm 3-4 kwamda mfupi sana , ni Dr GALIMU mtatuzi wa matatizo yako kunadawa ya kupunguza unene, kitambi (nyamazembe),matiti makubwa kuwa madogo, uzazi, kuludisha mali iliyopotea, kuuzavitu bila kununuliwa, biashara, wachimba madini kusafisha nyota, kuludishwa kazini mvuto wa mapenzi nk.

KWAHUDUMA NA MSAADA WASILIANA NA DR GALIMU ATAKUSAIDIA SM NO :- 0744 594 994

Habari Njema Kwa Wahitaji Wa Dawa Lishe Ya Kunenepesha Mwili.

$
0
0
Dawa  lishe  ya  kunenepesha  mwili  ni  dawa  ya  asili  inayo  saidia  kuongeza  na  kunenepesha  mwili.

Habari  njema  kwa  wahitaji  wa  dawa hii  ni  kwamba  sasa  inapatikana  ikiwa  imekamilika  kabisa yani  dawa  yenyewe  pamoja   asali  ya  tende  ambayo  ipo  tayari.   Awali  watumiaji  wa  dawa  hii  walikuwa  wanalazimika  kuitumia  pamoja  na  vitu  vingine  kama  vile  tangawizi, maziwa,  na  uji  wa  ufuta  jambo  lililo  kuwa  linaleta  usumbufu  kwa  baadhi  ya  watumiaji  ambao  walikuwa  hawana  nafasi  ya  kuandaa na  kutayarisha  hivyo  vitu  vingine  yaani  tangawizi, maziwa  na  uji  wa  ufuta.

Habari  njema  ni  kwamba, sasa  dawa  lishe  inapatikana  ikiwa  imekamilika tayari  kwa  kutumia , ambapo  mtumiaji   atatumia  kuichemsha  na  kuinywa  bila kuhitajika  kuwa  na  vitu  nilivyo  vitaja  hapo  juu.

Ama  kwa  upande  wa  asali  ya  tende  hapo  awali  mtumiaji  wa  dawa  lishe  ya  kunenepesha  na kuongeza  mwili  alilazimika   yeye  mwenyewe  kuandaa  na  kutyarisha  asali  ya  tende ambayo  hutumika  pamoja  na  dawa  lishe  ya  kunenepesha  mwili.

Kuandaa  na  kutayarisha   Asali  ya  Tende ambayo  ni  kiambatano  muhimu  sana  katika  lishe  ya  kuongeza  na  kunenepesha  mwili  ni  jambo  liliko  kuwa  linawashinda  watu  wengi  kwa  sababu  mchakato  wa  kuandaa  na  kutayarisha  asali  ya  tende  ulikuwa  mrefu  wenye  gharama  na  unao  tumia  muda  mwingi.

Habari  njema  ni  kwamba, sasa  Asali  ya Tende  inapatikana  ikiwa  imekamilika  kabisa. Kazi  yako  kama  mtumiaji  itakuwa  ni  kutumia  tu  asali  ambayo ipo  tayari.

Kwa  mahitaji  yako  ya  Dawa –Lishe  ya  kuongeza  na  kunenepesha  mwili, fika  katika  duka  la  Neema  Herbalist. Tunapatikana  UBUNGO  jijini  Dar  Es  Salaam  nyuma  ya  jengo  la  UBUNGO  PLAZA  jirani  na  Shule  Ya  Msingi  UBUNGO  NATIONAL  HOUSING.

Kwa  wateja   waliopo  jijini  Dar  Es  Salaam, ambao hawana  nafasi  ya  kufika  ofisini  kwetu, tunao  utaratibu  wa  kuwafikishia  dawa  mahali  walipo  ( HOME  & OFFICE  DELIVERY )

Kwa  wateja  waliopo  nje  ya  mkoa wa  Dar  Es  Salaam, tunawatumia  dawa  kwa  kutumia  usafiri  wa  mabus  mbalimbali.

Wasiliana  nasi  kwa  simu  namba  0766  -53 83 84.

Kwa  taarifa  kuhusu  huduma  zetu nyinginezo, tutembelee  kila  siku  kupitia  blogu yetu :

Magereza Wataja Sababu za Kumzui Profesa Jay Kumuona Sugu Gerezani

$
0
0
Mbunge wa Mikumi mkoani Morogoro, Joseph Haule ‘Profesa Jay’  jana alizuiwa kumuona mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi pamoja na katibu wa Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga baada ya kuzuiwa na maofisa wa magereza.

Profesa Jay aliyeambatana na mke wake, Grace Haule walifika jana jijini Mbeya na kwenda gerezani kuwaona Sugu na Masonga ambao wapo mahabusu wakikabiliwa na kesi ya kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli.

Mkuu wa magereza Mkoa wa Mbeya, Kamshina Msaidizi Mwandamizi (SACP), Paul Kijida alisema walimzuia Profesa Jay kwa sababu haikuwa siku ya kuwaona mahabusu.

‘Kweli amekuja hadi ofisini kwangu, lakini taratibu hazipo hivyo. Siku za kawaida kama hizi tunamruhusu mtu anayempelekea chakula au ataruhusiwa pale mfungwa au mahabusu anaumwa au mwanasheria wake anaruhusiwa kama tu kuna kitu muhimu’’ alisema Kijida na kuongeza kwamba, 

‘’Lakini tukisema kila mtu kwa muda na siku anayotaka iwe siku ya kuwaona wafungwa au mahabusu hatutafanya kazi sasa. Siku za kuwaona wafungwa na mahabusu kwa watu wa kawaida ni Jumamosi na Jumapili tu,” alisema mkuu huyo wa magereza.

‘’Nimejaribu kuonana na RPO (mkuu wa magereza mkoa) lakini naye ameonekana kusita kunipa kibali cha mimi kuonana nao. 

"Na inaonyesha kuna kitu nyuma kimejificha. Lakini nimefunga safari kuja kuonana nao hivyo siwezi kuondoka bila kuonana hivyo kesho(leo) nitakuwepo mahakamani, nitazungumza nao,” alisema Profesa Jay jana.

Alisema anachotambua ni kuwa mbunge hazuiliwi kuwaona mahabusu gerezani, lakini jambo hilo limemshangaza.

Akizungumza na mama yake Sugu aitwaye Desderia, alimtaka kuwa na ustahimilivu katika kipindi hiki ambacho mwanaye yupo kwenye misukosuko.

Profesa Jay alisema, “mama usihofu, yule hajabaka wala hajaiba bali kilichomuweka ndani ni kutetea masilahi ya wananchi. Na ndio maana hata sisi tumeacha kazi zote huko kuja kuhakikisha tunashughulikia jambo hilo na naamini haki itatendeka tu. 

"Na hapa usione tupo wachache kuja hapa nyumbani, lakini Sugu ana kundi kubwa sana la watu na tumegawana majukumu ya kufanya kuhusu hili tatizo.”

Hoteli ya Hyatt Regency Yatangaza Chumba cha Milioni 22..4 kwa Usiku mmoja tu wa Valentine Day...Kazi Kwako Mdau!

$
0
0
Hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es Salaam juzi ilitangaza ofa ya chumba cha Sh22.4 milioni katika Usiku wa Valentine na kusema kuwa Watanzania mbalimbali wamekuwa wakipiga simu kutaka kujua kama ni bei halisi na wengine kuomba punguzo.

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Masoko na Mauzo, Denis Glibic alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu chumba hicho na namna watu walivyolipokea tangazo hilo.

Glibic alisema tangu watangaze ofa hiyo ambayo ni kwa ajili ya wapendano katika sikukuu ya Valentine, wamepokea simu nyingi kutoka kwa Watanzania wakitaka kujua kama kweli hilo ni tangazo lao halisi na wengine wakitaka wapate nafasi hiyo kwa punguzo la bei. 

Kuhusu chumba hicho ambacho kinatumiwa na marais mbalimbali duniani wanapokuja nchini, meneja mwendeshaji wa hoteli hiyo, Timothy Mlay alisema, kwa kawaida bei yake huwa ni Sh11.4 milioni kwa siku.

Alisema pamoja na kuwapo kwa malalamiko ya maisha magumu, wanaamini watu watapatikana kwani kwao kuanzia Desemba mpaka sasa ni kipindi ambacho hupata wateja wengi.

Alisema huduma zitakazotolewa kwa wateja wa chumba hicho siku hiyo zitakuwa tofauti kwa wateja wengine, kwani mbali ya kwenda kuchukuliwa na gari la kifahari eneo wanaloishi, pia watapatiwa zawadi za mapambo ya mwilini yenye madini ya Tanzanite

Meneja wa Diamond Amtolea Uvivu Ruge Mutahaba wa Clouds Media

$
0
0
Meneja wa label ya WCB, Sallam SK amefunguka kwa kuendelea kudai kw Fmamba kampuni yao haina tatizo na chombo chochote cha habari isipokuwa Ruge Mutahaba ambaye ni Mkurugenzi wa Uzalishaji wa Vipindi Clouds FM na Clouds TV ndio mwenye tatizo na label hiyo.

Mapema wiki hii meneja huyo alianza kwa kuandika ujumbe mtandaoni unaodai kuna mtu anataka kumshusha Diamond huku akidai hakuna mtu wa kumshusha katika utawala huu wa Rais John Pombe Magufuli.
Sallam ameendeleza mashambulizi hayo ambapo jana amemtaja mtu aliyedai kwamba ana njama za kumshusha Diamond.

“Kwa heshima ya Joe Kusaga kukuombea msamaha kwa leo Bw Ruge Mutahaba naamua kukusitiri, ila ukiendelea kuyafanya ambayo unayafanya basi nitayaanika maovu yako yote unayoyafanya kwenye Industry ya muziki. WCB haina tatizo na media yoyote na wala haina tatizo na Clouds Media Group ila huyu Ruge Mutahaba ndio mwenye tatizo #TumekataaKuwaKaa,” aliandika Sallam kupitia Instagram.

Meneja huyo anaonekana kutaka kuendeleza harakati hizo kwani toka aanze kutoa waraka huo amekuwa akiweka hushtag ambayo imekuwa ikitumika na Clouds Media, #TumekataaKuwaKaa.

Ruge bado hajazungumza chochote kuhusiana na tukio hili

Tanzania kuwa na watu 58 milioni ifikapo mwishoni mwa mwaka huu

$
0
0
Tanzania inatarajiwa kufikisha idadi ya watu milioni 58 ifikapo mwishoni mwa mwaka huu ikiwa ni ongezeko la juu ikilinganishwa na idadi ya awali ya watu milioni 46 iliyoripotiwa mwaka 2010.

Kwa mujibu wa Idara ya Jamii na Mambo ya Uchumi ya Shirika la Umoja wa Mataifa (UN), makadirio hayo ni sawa na kila kilomita moja ya mraba kuna wakazi 67 tofauti na makadirio ya mwaka 2010 ya watu 52.

“Tanzania ina kiwango kikubwa cha kuzaliana duniani na zaidi ya asilimia 44 ya watu ni chini ya miaka 15. Kiwango cha kuzaliana ni watoto 5.01 kwa mwanamke mmoja ambacho ni kikubwa kwa nchi kama Tanzania,” ripoti hiyo ya makadirio ya UN inaonyesha.

Inasema kila sekunde 14, mtoto mmoja anazaliwa nchini huku mtoto mmoja akifariki dunia kila baada ya sekunde moja.

Makadirio hayo pia yanaonyesha kuwa idadi ya watu nchini imeongezeka kwa asilimia 3.15 kwa kipindi cha miaka minane iliyopita wakati kiwango cha kuzaliana kilikuwa ni asilimia 5.17 kati ya mwaka 2015 na 2018.

Ikiwa hali hiyo itaendelea hivyo, ripoti hiyo inabainisha kuwa kwamba idadi ya watu itaongezeka kufikia milioni 95.5 ifikapo mwaka 2050 na watu milioni 300 ifikapo mwaka 2099.

Mchanganuo wa ripoti hiyo unaonyesha kuwa makadirio hayo ni sawa na asilimia 0.77 ya idadi ya watu duniani kwa mwaka huu kutoka asilimia 0.66 katika mwaka 2010.

Tanzania imewekwa katika nafasi ya 24 miongoni mwa nchi zenye idadi kubwa ya watu duniani mwaka huu, kiwango ambacho ni kikubwa ikilinganishwa na mwaka 2010 ambapo ilikuwa nafasi ya 28.

Idadi ya hivi sasa ya watu waishio mijini inakadiriwa kufikia milioni 19.2 sawa na asilimia 31 ya idadi ya watu wote ikilinganishwa na ile ya awali ya mwaka 2010 iliyokuwa milioni 12.6 ambayo ilikuwa sawa na asilimia 27.4.

Hata hivyo, kulingana na makadirio ya idadi ya watu nchini mwaka 2016-17 yaliyofanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS), ilikadiriwa kwamba kungekuwa na idadi ya watu milioni 51.55 katika kipindi cha mwaka jana.

Tambwe Hizza wa Chadema Afariki Dunia

$
0
0
Mwanasiasa mkongwe na kada wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Tambwe Hizza amefariki dunia asubuhi ya kuamkia leo (Alhamis ) akiwa nyumbani kwake kwa ugonjwa wa pumu.

Msemaji wa Chadema, Tumaini Makene amethibitisha kifo hicho akisema Hiza amefariki leo asubuhi nyumbani kwake Mbagala akiwa amelala.

Hiza amefariki kipindi ambacho alikuwa katika timu ya kampeni za kumnadi mgombea wa ubunge wa Chama hicho katika Jimbo la Kinondoni, Salumu Mwalimu na jana jioni alipanda jukwaani kumnadi.

Mwalimu akizungumzia kifo hicho amesema “sina maneno yanayoweza kumwelezea Tambwe, Tambwe alikuwa mtu muhimu sana katika timu yangu ya kampeni, kaniacha kipindi muhimu sana.”

“Alikuwa nguzo yangu, katika muda aliokuwa nasi ndani ya chama Tambwe alikuwa na ushawishi mkubwa sana, hadi jana saa 4 usiku tulikuwa sote, Tambwe kaniacha kipindi muhimu kweli kweli sijui hata niseme nini,” ameongeza Mwalimu

Kuhusu kuendelea na kampeni, Mwalimu amesema “mimi binafsi sidhani kama nitaweza, lakini ngoja nisubiri chama, kwa sasa nakwenda msibani ila baadae tutajua.”

Mwaka 2015, Hiza alitangaza kujiunga na Chadema wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu akitokea CCM ambako aliwahi kuhudumu kama mkuu wa kitengo cha propaganda wa chama hicho tawala.

Kabla ya kujiunga na CCM alihama kutoka katika Chama cha Wananchi (CUF) ambako pia alihamia kutoka NCCR-Mageuzi.

Katika kampeni za urais 2015, Hiza alikuwa katika jopo la kumnadi mgombea wa Chadema aliyeungwa mkono na vyama vinavyounda Ukawa, Edward Lowassa na mara zote alikuwa anapanda jukwaani mwanzoni kama alivyokuwa akifanya kwenye kampeni za  Mwalimu zinazoendelea.

Waziri Mkuu apinga madai ya mbunge wa Chadema Kuhusu wagombea Chadema kutotangazwa washindi

$
0
0
Waziri Mkuu  Kassim Majaliwa amesema hajui kama kuna kata ambayo mgombea wa Chadema ilishinda lakini hakutangazwa, badala yake akatangazwa mshindi kutoka chama kingine cha siasa.

Ametoa kauli hiyo leo Februari 8, 2018 bungeni Dodoma katika kipindi cha maswali ya papo kwa hapo kwa Waziri Mkuu, wakati akijibu swali la mbunge wa viti maalumu (Chadema), Devotha Minja.

Katika swali lake, Minja ametaka kujua Serikali inasema nini kuhusu ukandamizwaji wa haki unaofanywa na wasimamizi wa uchaguzi ambao wanawatangaza wagombea ambao hawakushinda na kuwaacha walioshinda.

Mbunge huyo ametoa mfano wa Kata ya Sofi mkoani Morogoro ambako mgombea wa Chadema alipata kura 1908, wa  CCM kura 1878.

Pia, ametaja Kata ya Siyui mkoani Singida, mgombea wa Chadema alipata kura 1,358 huku wa CCM akipata kura 1304, lakini waliotangazwa wote walikuwa wa chama tawala.

Katika majibu yake, Waziri Majaliwa amesema hatarajii kuwa tume inaweza kuwatangaza walioshindwa na kuwaacha washindi.

"Lakini sheria zinaipa nafasi Tume  ya Uchaguzi (NEC) kukutana na vyama vinavyogombea ili kuwapo na nafasi ya kujadiliana kwenye upungufu," amesema Majaliwa.

Hata hivyo, amewataka wanaohisi kuonewa waende mahakamani kudai ushindi wao katika kipindi kisichozidi miezi mitatu ili sheria itazamwe kwenye ushindi huo.

Majibu ya Serikali Kuhusu Zile Milioni 50 Ilizoahidi Kwa Kila Kijiji

$
0
0
Mkurugenzi wa Idara ya Habari na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dk. Hassan Abbasi amesema kuwa serikali itaweka utaratibu utakaowezesha kutekelezwa kwa ahadi ya kutolewa milioni 50 kila kijiji, hivyo wananchi wasiwe na hofu.

Dkt Abbasi aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu masuala mbalimbali na miradi inayotekelezwa na serikali, na kuweka bayana kwamba, tayari mambo makubwa zaidi yameshafanyika, na hivyo hilo la milioni 50 kila kijiji litatekelzwa pia.

Majibu hayo aliyatoa baada ya mmoja wa waandishi wa habari kuulizwa swali, baada ya kuona ni mwaka wa tatu sasa tangu Rais Dkt Magufuli alipoingia madarakani, lakini ahadi yake ya kutoa TZS milioni 50 kila kijiji kwa ajili ya kuwasaidia kina mama na vijana kujikwamua kiuchumi haijatekelezwa.

“… 50 nyenyewe tutaweka utaratibu itakuja tu ikifika. Lakini maji si yanakuja bana, dawa si zipo, barabara si zipo, sasa kama wewe ulitaka ile 50 ili upige dili, tulia kwanza.”

Aidha, Dkt Abbasi amesema kwamba, ilani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) haikusema ni lini ahadi hiyo itatekelezwa, kama ni 2017 au 2018, hivyo akawataka wananchi kuwa na subira, pindi utaratibu ukikamilika watapatiwa fedha hizo.

==>Msikilize hapo chini

Jaji Mkuu Aionya Serikali

$
0
0
Jaji Mkuu nchini Kenya David Maraga, ameilaumu serikali ya nchi hiyo kwa kufanya maamuzi kinyume cha Sheria na Katiba ya nchi hiyo katika kukabiliana na upinzani.

 Jaji Maraga ametoa kauli hiyo ikiwa imepita masaa kadhaa tokea kufukuzwa kwa mwanasheria maarufu ambaye alikuwa miongoni mwa watu walioshuhudia kuapishwa Raila Odinga katika uwanja wa ‘Uhuru Park’ kufukuzwa nchini humo na kupelekwa Canada.

Katika ukurasa wake wa Twitter Jaji Maraga amesema malalamiko yaliyopelekwa Mahakamani yalikuwa wazi na majukumu ya kufanyia maamuzi yalikuwa ya Mahakama kutokana na kwamba ndio chombo pekee cha kutetea haki kwa kila mmoja pamoja na serikali yenyewe.

Jaji huyo ametoa tamko hilo la kuionya serikali kwa kushindwa kutii sheria kutokana na kitendo cha serikali ya Kenya kuonekana kudharau maamuzi ya mahakama

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya February 9

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images