Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Jaji Ramadhani azungumzia uadilifu wa Jaji Kisanga...Awapa Neno Majaji

$
0
0
Jaji Mkuu mstaafu, Augustino Ramadhani amemzungumzia Jaji Robert Kisanga kuwa mtu aliyebobea katika taaluma na hakuwahi kujihusisha na rushwa.

Amesema hayo leo Alhamisi Januari 25,2018 Oysterbay jijini Dar es Salaam alikokwenda kuhani msiba wa Jaji Kisanga (85).

Jaji Ramadhani amesema hakuna hata siku moja aliwahi kusikia malalamiko dhidi ya Jaji Kisanga kutokana na uadilifu wake.

"Mimi ni miongoni kwa watu waliopitia kwenye mikono yake, yeye ndiye aliyenifundisha masuala ya Mahakama ya Rufaa," amesema.

Amesema, “Alikuwa mahiri kwenye kazi na kama uko naye kwenye kesi ni muhimu usome sana kwa sababu alikuwa anasoma na kila jambo alilichimba kwa undani."

Jaji Ramadhani amesema, "Naweza kusema ni miongoni mwa majaji waadilifu, kwake rushwa ilikuwa mwiko, hakuwahi kujihusisha na vitendo hivyo ndiyo sababu sikuwahi kusikia malalamiko dhidi yake."

Amesema majaji wanatakiwa kujifunza tabia hiyo kutoka kwa Jaji Kisanga.

"Majaji wanapaswa kutambua kuwa hakuna kitu kibaya kama kuuza utu wa mtu, mwenzetu Kisanga alizingatia mno sheria na hata mawakili waliokuwa wanapangiwa kesi kwake walikuwa wanajipanga," amesema.

Jaji Kisanga alifariki dunia Jumanne Januari 23,2018 katika Hospitali ya Regency jijini Dar es Salaam alikokuwa akipatiwa matibabu ya saratani.

Mwalimu Atiwa Mbaroni Kwa Lugha Ya Matusi Mtandaoni

$
0
0
JESHI  la Polisi Mkoa wa Mwanza linamshikilia Mwalimu wa Shule ya Sekondari  Mkolani, Deogratius Kisandu, akidaiwa kutumia lugha ya matusi, kejeli na kudhalilisha katika ukurasa wake wa Facebook.

Akizungumza na waandishi wa habari jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Ahmed Msangi, alisema  Kisandu alikamatwa jana baada ya kuwapo taarifa kuhusu kuonekana ujumbe wa matusi na lugha zisizofaa  katika ukurasa  wake ya Facebook.

Alisema walimfuatilia mtuhumiwa na kumkamata akiwa na simu yake ambayo huitumia kupeleka na kuandika matusi hayo kinyume na Sheria Namba 4 ya Makosa ya Mtandao ya Mwaka 2015.

“Polisi bado wanaendelea na  na mahojiano na upelelezi dhidi ya mtuhumiwa. Utakapokamilika atafikishwa mahakamani kwa mujibu wa sheria.

“Taarifa zinaonyesha kuwa mtuhumiwa amewahi kushtakiwa kwa makosa kama hayo kipindi cha nyuma,” alisema Kamanda Msangi.

Kamanda   amewataka  vijana wanaotumia mitandao ya  jamii kuacha kwa sababu  ni kosa kwa mujibu wa Sheria ya Makosa ya Mtandao ya Mwaka 2015.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, John Mongella, alisema alipokea  malalamiko kutoka kwa wananchi siku mbili zilizopita kuhusu lugha ya kudhalilisha, matusi na kejeli  inayotumiwa na Kisandu ambaye pia ni mtumishi wa umma, katika  ukurasa wake wa Facebook.

“Tumetumia siku mbili mpaka kumpata Kisandu. Mwanzoni nilifikiri labda haya mambo yanafanywa na mtu ambaye si raia wa Tanzania lakini katika mahojiano amekiri yeye ni Mtanzania.

“Kwa kweli lugha anayoitumia ni ya kudhalilisha, matusi na kejeli na haifai kutumiwa kutokana na utamaduni wetu,” alisema.

Meneja wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Kanda ya Ziwa,   Lawi Odiero, alisema sheria ipo na inakataza matumizi mabaya ya mitandao na  kwa kuwa kesi hiyo ipo polisi  atatoa ushirikiano unaohitajika kusaidia uchunguzi.

Rais Magufuli akutana na Mjumbe Maalum wa Rais Kagame

$
0
0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo tarehe 25 Januari, 2018 amekutana na Mjumbe Maalum wa Rais wa Rwanda na aliyewahi kuwa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika (AfDB) Dkt. Donald Kaberuka na kuzungumzia masuala mbalimbali yanayohusu maendeleo ya Tanzania na umoja wa Afrika (AU).

Baada ya mazungumzo hayo yaliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa Dkt. Kaberuka amesema uchumi wa Tanzania unakua vizuri na amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa jinsi anavyosimamia ukuaji wa uchumi huo.

“Nimefurahi sana jinsi Tanzania inavyokwenda mbele, maendeleo yanakwenda kwa kasi na Mhe. Rais anafahamu kabisa kwamba katika Afrika nchi zetu zinahitaji kuwa na uchumi bora, ningependa kumpongeza Mhe. Rais na Watanzania wote kwa kazi nzuri wanayofanya” amesema Dkt. Kaberuka.

Dkt. Kaberuka amesema katika mazungumzo hayo pia amewasilisha ujumbe wa Rais wa Rwanda Mhe. Paul Kagame ambaye kuanzia mwezi huu atakua Mwenyekiti wa Umoja wa Afrika (AU), na ndiye aliyekabidhiwa majukumu ya kufanya mabadiliko ndani ya umoja huo.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli ameagana na Balozi wa Zimbabwe hapa nchini anayemaliza muda wake Mhe. Edzai Chimonyo na kumpongeza kwa uwakilishi mzuri alioufanya kwa miaka 10 aliyoiwakilisha Zimbabwe hapa nchini.

Mhe. Rais Magufuli amemuomba Mhe. Chimonyo kumfikishia salamu za pongezi Mhe. Emmerson Mnangagwa kwa kuchaguliwa kuwa Rais wa Zimbabwe na amemuhakikishia kuwa Tanzania itaendeleza uhusiano na ushirikiano mzuri wa kihistoria na kidugu uliopo kati yake na Zimbabwe.

“Naomba umwambie Mhe. Rais Mnangagwa kuwa namkaribisha atembelee Tanzania na namtakia heri katika majukumu yake, natarajia ataendeleza uhusiano na ushirikiano wetu ili tuweze kujiimarisha zaidi kiuchumi kwa manufaa ya nchi hizi mbili” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Mhe. Chimonyo ameshukuru kwa ushirikiano mkubwa alioupata katika kipindi chake cha Ubalozi hapa nchini na amempongeza Mhe. Rais Magufuli kwa namna anavyoiongoza nchi, huku akitaja baadhi ya mambo yanayofanywa kwa mafanikio makubwa kuwa ni mapambano dhidi ya rushwa, ujenzi wa miundombinu hususani barabara, madaraja na viwanja vya ndege.

Mhe. Chimonyo ambaye alikuwa kiongozi wa Mabalozi wa Afrika wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini na Kaimu Kiongozi wa Mabalozi wote wanaowakilisha nchi zao hapa Tanzania amesema Mabalozi hao wanafurahishwa na wanaunga mkono juhudi mbalimbali zinazofanywa na Mhe. Rais Magufuli ikiwemo kuhamia makao makuu Dodoma.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
25 Januari, 2018

Hiki ndicho amekisema Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuhusu watu ambao wanamtusi Rais Magufuli

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda amefunguka na kusema kuwa wao kama viongozi wanazidi kuimarisha huduma mbalimbali za afya ili watu ambao wanamtusi Rais John Pombe Magufuli wazidi kuwa na afya nzuri.

Makonda amesema hayo leo Januari 25, 2018 akiwa katika hospitali ya Mwananyamala jijini Dar es Salaam alipofanya ziara na kumpongeza Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Alli Hapi kwa kazi nzuri anayofanya kuhakikisha masuala ya maendeleo kwa wananchi yanaonekana na kufanyika.

"Wanaoatamba na kumtukana Rais Magufuli ni kwa sababu wazima lakini wakiugua watakuja Mwananyamala, Amana, wengine wataenda Temeke, Muhimbili hata Mlonganzila kuomba matibabu, ila wakiwa wazima waache waseme wanavyotaka, sasa kazi yetu sisi kuwafanya wawe wazima, wakiwa wazima wakija kushukuru sawa na wasipokuja kushukuru basi mwenyezi Mungu anajua namna ya kubariki viongozi wetu wanaofanya kazi zao, lakini mwisho wa siku kubariki Chama Cha Mapinduzi ambacho kimetupatia viongozi waadilifu na waaminifu wanoifanya hii kazi" alisema Makonda

Mbali na hilo Mkuu huyo wa mkoa wa Dar es Salaama amesema kuwa kwa sasa wanampango wa kuingia kwenye mfumo wa matibabu kwa njia ya kadi na kudai kuwa njia hiyo itapunguza kero mbalimbali na usumbufu usio na msingi kwa wagonjwa.

"Tiba kwa kadi ni muhimu sana na tutakuja kuzindua kampeni kubwa sana hapa na tutatoa muda fulani kwamba kila mwananchi wa mkoa wa Dar es Salaama lazima awe na kadi yake na kama huna kadi huwezi kupata matibabu, sasa isije kufika hiyo hatua ya kukulazimisha wakati jambo la afya ni muhimu sana" alisisitiza

Serikali yazifutia usajili kampuni tatu

$
0
0
Serikali yasitisha Shughuli za Kampuni Tatu (3) za Wakala binafsi wa huduma za ajira hapa nchini kutokana na kukiuka matakwa ya sheria ya huduma za ajira Na.9 ya mwaka 1999 na Kanuni zake.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama amesema kuwa Ofisi yake imekuwa ikipokea malalamiko kutoka kwa wafanyakazi na wadau mbalimbali kuhusu utaratibu unaotumiwa na baadhi ya wakala binafsi wa huduma za ajira nchini.

Kampuni zilizofutiwa usajili baada ya kukiuka sheria ni pamoja na Sasy Solution Company Ltd, Bravo Job Centre Agency na Competitive Manpower International Ltd ambapo Kampuni hizo haziruhusiwi kujihusisha na shughuli za Uwakala  binafsi wa ajira  nchini.

Akifafanua Mhe. Mhagama amesema kuwa uchunguzi umebaini ukiukwaji wa taratibu za usajili ambapo baadhi ya mawakala wamekuwa wakitumia nyaraka zilizopatikana kwa njia isivyo halali katika kujipatia leseni za uwakala hali iliyowawezesha kukwepa kodi na kujipatia faida.

Aliongeza kuwa ukiukwaji wa taratibu za kisheria umeleta athari mbalimbali kwa wafanyakazi hasa kwa wale wanaoenda kufanya kazi Mataifa ya Nje ambapo wafanyakazi hao wamekuwa wakifanyiwa vitendo vya ubaguzi na unyanyasaji katika ajira, malipo ya mishahara na stahiki mbalimbali.

Aidha, Mhe. Mhagama amesema kuwa Ofisi ya Waziri Mkuu imesitisha mara moja shughuli za Mawakala Binafsi wa huduma za Ajira zinazohusika na kuwatafutia kazi wafanyakazi nje ya nchi (cross border placement) hadi hapo Serikali itakapoleta mfumo wa kusimamia jambo hili na kutoa taarifa kwa umma.

Mbowe Asikitishwa Kesi ya Sugu Inavyoendeshwa

$
0
0
Mwenyekiti wa Chama cha Kidemokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Taifa, Freeman Mbowe amedai amesikitishwa na namna inavyoendeshwa kesi ya Mbunge wa Mbeya Joseph Mbilinyi 'Sugu' na Katibu CHADEMA kanda ya Nyasa Emmanuel Masonga iliyoahirishwa leo.

Freeman Mbowe ameeleza hayo wakati alipokuwa anazungumza na waandishi wa habari hii leo katika viunga vya Mahakama ya mkoani Mbeya mara baada ya kuahirishwa kwa kesi hiyo na kuzitaka mamlaka husika zinazosimamia sheria nchini kujiangalia vizuri katika utendaji kazi wake.

"Tumesikitishwa kwa namba suala hili jinsi lilivyo shughulikiwa, sipendi kuingilia uhuru wa Mahakama, mienendo ya kimahakama lakini mimi kama raia na kiongozi nafikili vyombo vinavyostahili kutoa haki kwa wananchi vinawajibu wa kujiangalia vizuri. 

"Mahakimu, Majaji, Mawakili wa Serikali pamoja na Askari wenyewe hawa wote ni binadamu haina maana kwamba wao hawawezi kufanya makosa wao ni binadamu kama walivyo wengine", alisema Mbowe.

Kesi inayowakabili Mbunge wa Mbeya Joseph Mbilinyi 'Sugu' na Katibu CHADEMA kanda ya Nyasa Emmanuel Masonga imehairishwa leo na kutajwa kusikilizwa Februari mbili baada ya Mawakili watatu kujitoa kuwasimamia katika kesi hiyo.

Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Ijumaa ya January 26

Dk. Kigwangalla Akunjua Makuva......Ataja Majina ya Watuhumiwa wa Ujangili Huku Akiwavaa Mawaziri Wakuu na Polisi

$
0
0
Na Hamza Temba - Dodoma
.........................................................................
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla jana Januari 25, 2018 mjini Dodoma ametaja majina ya watuhumiwa wa ujangili ambao wengi wao ni wamiliki na washirika wa Kampuni za uwindaji wa kitalii na kuwapa siku saba wawe wamefika kwa hiari yao wenyewe katika ofisi za Wizara hiyo Mjini Dodoma, Swagaswaga House kwa ajili kutoa maelezo kwanini wasichukuliwe hatua za kisheria ikiwemo kujibu tuhuma hiyo na nyingine nyingi zinazowakabili mbele ya kamati atakayoiunda.

Akizungumza na waandishi wa habari mjini hapa, Dk. Kigwangalla ametaja baadhi ya tuhuma hizo ambazo ziko kinyume cha sheria na taratibu za uwindaji wa kitalii kuwa ni uwindaji haramu, uhawilishaji wa umiliki wa vitalu vya uwindaji pasipo kufuata sheria, udanganyifu kwenye kujaza fomu za uangalizi,  rushwa, uhalifu dhidi ya rasilimali za wanyamapori na uhujumu uchumi.

Alitaja tuhuma zingine kuwa ni ukiukwaji wa kanuni za uwindaji (kupiga wanyama usiku, kuwinda wanyama bila kujali umri, kupiga wanyama nje ya maeneo waliyopewa), kukutolipa tozo mbalimbali za maendeleo za jamii kwenye vijiji jirani na maeneo wanaoendesha biashara ya uwindaji, kushindwa kuendesha ipasavyo shughuli za kuzuia ujangili.

Dk. Kigwangalla aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni ndugu Pasanis na wenzake ambao wanamilikia kampuni ya Berlette Safari Corporation Ltd na Ngugu Shein Ralgi na wakurugenzi wenzake wa kampuni ya Game Frontiers of Tanzania Ltd.

Wengine ni Ndugu Howel na wakurugenzi wenzake wa kampuni ya Mkwawa Hunting Sfaris Tanzania Ltd, Ndugu Thomas Fredikin na wenzake wa Kampuni ya Mwiba Holdings Ltd, Wengert Windrose Safaris Tanzania  Ltd na Tanzania Game Trackers Safaris Ltd, na Ndugu Awadh na wenzake ambao wanamiliki kampuni ya Uwindaji wa Greenmiles Safaris Ltd.

Aliwataja washirika wengine kuwa ni Ndugu ni Kwizema, Ndugu Robert, Ndugu Solomon Makulu, Ndugu Siasa Shaban, Ndugu Hamis Abdul Ligagabile na mtumishi wa Wizara Wizara ya Maliasili na Utalii, Alex Aguma.

Katika hatua nyingine Dk. Kigwangalla ametoa Ilani ya siku 30 kwa watu mbalimbali ikiwemo Mawaziri Wakuu Wastaafu waliovamia kiwanja chenye hati namba 4091 kilichopo Njiro Jijini Arusha wafike kwa Kamishna Mkuu wa Ardhi waweze kuhakikiwa na kuthibitisha umiliki wao halali ama sivyo wavirejeshe Serikalini viweze kumilikishwa kwa mmiliki wake halali.

“Natoa ilani ya siku 30 kwa mtu yeyote ambaye anajua alivamia kiwanja katika eneo hili ambalo lina hati namba 4091 kilichopo Njiro, Arusha, haraka sana ajipange kupeleka taarifa zake mbele ya Kamishna wa Ardhi kabla hatujachukua hatua nyingine za kisheria, hati iliyoko pale ipo katika jina la Bodi ya Utalii Tanzania japo wao wanadai wana hati nyingine.

“Wengi wao wamejenga nyumba za kudumu katika eneo lile, na wengine ni viongozi waliokuwa mawaziri wakuu wastaafu nao wana viwanja katika eneo hilo na wamejenga nyumba zao katika eneo hilo,” alisema Dk. Kigwangalla.

Alisema kiwanja hicho kilichokuwa na ekari zaidi ya 40 kilikuwa kinamilikiwa na taasisi ya Serikali ambayo ni kampuni tanzu ya Bodi ya Utalii Tanzania iliyokuwa inajulikana kama Serengeti Safari Lodges na baadae kikauzwa kwa Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro.

Wakati huo huo, Dk. Kigwangalla ametoa siku saba kwa Jeshi la Polisi nchini kuchukua hatua dhidi ya watuhumiwa wanne wanaojihusisha na mtandao wa ujangili pamoja na kupanga njama zilizopelekea mauaji ya Mhifadhi wa Wanyamapori Ndugu Wayne Lotter, raia wa Afrika ya Kusini ambaye alikuwa Mkurugenzi wa Kampuni Pams Foundation, aliyeuawawa eneo la Chole Masaki Jijini Dar es Salaam mwezi Agosti mwaka jana.

“Natoa siku saba kwa wenzetu wa jeshi la Polisi wachukue hatua dhidi ya watu wanne, ambao mimi majina yao ninayafahamu ambao miongoni mwao watatu wanahusika na kuendesha biashara ya ujangili, na ni watu wakubwa, ni matajiri wakubwa na wana mitandao mikubwa ya ujangili.

“Ninafahamu taarifa hizi polisi wanazo lakini hawajachukua hatua za kuwakamata watu hawa na kuwafikisha kwenye macho ya sheria, muda ni mrefu  na sisi wenye taarifa hizi sasa tumeanza kuchoka kusubiri.

“Hawa watu wanne walihusika kupanga njama ambazo zilipelekea kusababisha mauaji ya kikatili ya Mkurugenzi wa Kampuni ya Palm Foundation, Ndugu Wayle Lotter mwezi Agosti mwaka jana eneo la Chole Masaki mwezi Agosti mwaka jana.

“Nataka ndani ya siku hizi saba wawe wamechukua hatua na kama hawatochukua hatua manaake tutajua wana vested interest (maslahi) kwahivo tutaenda kuripoti kwa Amiri Jeshi mkuu ambaye ni Mhe. Rais aliyetutuma kazi ya kusimamia sekta hii,”. Alisema Dk. Kigwangalla.

Rais Wa Simba Fc Alazwa Muhimbili.....Mahakama yaelezwa anasumbuliwa na Figo

$
0
0
MWENDESHA Mashtaka Mwandamizi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana Rushwa ,(Takukuru) , Leonard Swai ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa Rais wa Klabu ya Simba, Evans Aveva amelazwa Hospital ya Taifa ya Muhimbili akisumbuliwa na Figo.

Aveva ni mshtakiwa wa kwanza katika kesi ya uhujumu uchumi ambapo anashtakiwa pamoja na Makamu rais wa klabu ya Simba, Godfrey Nyange ‘Kaburu’ ambaye alikuwepo mahakamani hapo

Wakili Swai amedai mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Victoria Nongwa kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.

Amedai, walishachukua maelezo ya mshtakiwa wa pili na kwamba wanaangalia jinsi ya kupata maelezo ya mshtakiwa wa kwanza ambaye kwa sasa ni mgonjwa.Baada ya kueleza hayo Hakimu Nongwa ameaihirisha kesi hiyo hadi February 8,2018 kwaajili ya kutajwa.

Aveva na Kaburu wanakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha fedha Dola za kimarekani 300,000.

Kesi ya Tundu Lissu Yapigwa Kalenda

$
0
0
Kesi inayomkabili Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu na wahariri wa Gazeti la Mawio katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeahirishwa hadi Februari 26.

Wakili wa Serikali, Elia Athanas jana alimueleza Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kuwa kesi imepangwa kwa ajili ya kutajwa na kwamba hadi sasa hawajajua hali ya mshtakiwa wa nne, Lissu.

Kesi hiyo ambayo ipo katika hatua ya usikilizwaji wa ushahidi wa upande wa mashtaka, inamkabili Lissu na wenzake Simon Mkina, Jabir Idrisa na Mchapishaji wa Kampuni ya Jamana, Ismail Mehbooh.

Kwa pamoja washtakiwa hao, wanakabiliwa na mashtaka matano likiwamo la kuandika habari za uchochezi kinyume na Sheria ya Magazeti ya Mwaka 2002.

Inadaiwa kuwa Januari 12 hadi 14, 2016 jijini Dar es Salaam, washtakiwa Jabir, Mkina na Lissu, waliandika na kuchapisha taarifa‎za uchochezi zenye kichwa cha habari kisemacho, ‘Machafuko yaja Zanzibar.’

Katika shtaka la pili wanadaiwa kuwa Januari 14, 2016 walichapisha habari hizo ili kuleta chuki kwa wananchi wa Zanzibar.

Mshtakiwa Mehboob anadaiwa kuwa Januari 13 ,2016 katika jengo la Jamana lililopo Manispaa ya Ilala, alichapisha gazeti la Mawio lililokuwa na taarifa za uchochezi.

Inadaiwa kuwa mshtakiwa huyo pia alichapisha gazeti hilo bila ya kuwasilisha hati ya sheria ya kiapo kwa Msajili wa Magazeti.    

Bill Gates amuonya Trump kuhusu Afrika

$
0
0
Tajiri na Mfanyabiashara mkubwa duniani, Bill Gates amemuonya rais wa Marekani Donald Trump kwa misimamo ya sera yake ya “Marekani Kwanza” kuwa inaweza kuharibu uhusiano wa nchi hiyo na bara la Afrika.

Ameyasema hayo katika mkutano wa dunia wa uchumi World Economic Forum (WEF) unaofanyika huko Davos nchini Switzerland ambapo amesema kuwa kunatakiwa kuwepo kwa uwiano wa wenye nguvu kubwa na nguvu kidogo.

Amesema kuwa Marekani inaweza kupoteza ushawishi wake barani Afrika huku nchi kama China zinazidi kuimarisha uhusiano na bara hilo kwa kuwekeza katika sekta mbalimbali.

Bill Gates anamfuko wake barani Afrika unaoitwa Bill & Melinda Gates Foundation, ambao umekuwa ukijihusisha kwa kiasi kikubwa kutoa huduma za afya katika nchi kadhaa.

Hata hivyo, Rais Trump amesema kuwa atakata msaada wa bajeti ya afya kwa takribani dola bilioni 2.2 katika mfuko wa dunia, huku akiwakasirisha viongozi wa Afrika bada ya kuyaita mataifa ya Afrika machafu kupindukia.

Mkurugenzi halmashauri Ngara ahimiza michango shuleni Licha ya Serikali Kuzuia

$
0
0
Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ngara, Aidan Bahama amewaomba wadau mbalimbali kuchangia elimu wilayani humo licha ya Serikali kuzuia michango shuleni.
 
Bahama ametoa kauli hiyo jana Januari 25, mwaka 2018 wakati akizungumza na wakuu wa shule za sekondari, msingi, wenyeviti wa bodi na maofisa wa elimu katika kikao cha utendaji.
 
Amesema baada ya tamko la Rais John Magufuli la kupiga marufuku michango shuleni ili kutekeleza mpango wa elimu bure, viongozi hao wanapaswa kusimamia agizo hilo licha ya kuwepo kwa changamoto katika sekta ya elimu.
 
Amesema wadau wa maendeleo ya elimu wakichangia fedha wataweza kupunguza  uhaba wa vyumba vya madarasa, matundu ya vyoo, madawati ,nyumba za walimu na mahitaji mengineyo.
 
 “Hatumzuii mwenye nia ya kuchangia maendeleo ya shule lakini zifuatwe taratibu kwa kuhakikisha kuwa mwalimu hahusiki kushika fedha hizo. Mwalimu abaki kufundisha wanafunzi,” amesema.
 
Amesema shule nyingi wilayani humo zimesajili wanafunzi wengi, baadhi darasa moja lina wanafunzi zaidi ya 120.
 
Amesema shirika la Swash limejitolea Sh1.2bilioni kwa ajili ya kujenga vyoo katika baadhi ya shule za msingi wilayani humo.
 
Ofisa elimu kata ya Muganza, Mohamed Namtimba amesema baadhi ya shule za msingi na sekondari zitaathirika baada ya kusitishwa kwa michango kwa maelezo kuwa michango hiyo ilikuwa ikitumika kulipa walinzi na kununua chakula kwa ajili ya wanafunzi.

Nabii Tito Ajaribu Kujiua....Ashonwa Nyuzi 25

$
0
0
Siku mbili baada ya kukamatwa na polisi kwa mahojiano kwa Tito Machibya, maarufu Nabii Tito, anadaiwa kujaribu kujiua kwa kujikata na wembe tumboni na kushonwa nyuzi 25.

Nabii Tito alikamatwa na polisi mkoani Dodoma kwa kosa la kufundisha mafundisho yaliyo kinyume na dini kwa kuhamasisha watu kunywa pombe kwani si dhambi na kuoa wafanyakazi wao wa ndani ambapo hata hivyo, jeshi hilo lilisema nabii huyo ana matatizo na akili yaliyothibitishwa na daktari wa Hospitali ya vichaa ya Milembe mkoani Dodoma.

Inadaiwa kuwa, jana polisi waliambatana na nabii huyo nyumbani kwake Ng’ong’ona mkoani humo kwa ajili ya upekuzi ambapo aliingia ndani na kutoka akiwa anavuja damu tumboni huku ameshikilia wembe mkononi ambapo iliwalazimu polisi hao kumkimbiza Zahanati ya Polisi ya Mkoa wa Dodoma.

Mmoja wa madaktari wa zahanati hiyo kwa sharti la kutotajwa jina amesema nabii huyo alifikishwa, saa tisa alasiri akiwa na jeraha kubwa tumboni.

“Alifikishwa na kushonwa nyuzi 25 na kuruhusiwa kwani hakuwa na shida nyingine yoyote halafu jeraha lake halikufunguka kwa ndani sana, kwa hiyo hakutoka damu nyingi sana alitibiwa na kuondoka na askari.

Kamanda wa Polisi Mkoani Dodoma, Gilles Muroto alipoulizwa kuhusu tukio hilo hilo alisema hana taarifa.

Chanzo: Mtanzania

Shaka Ampiga Vijembe Maalim Seif

$
0
0
Wakati wananchi wa Jimbo la Kinondoni wakijiandaa na kampeni za ubunge wa jimbo hilo, Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM), umemtaka Katibu Mkuu wa Chama cha Wananchi (CUF), Maalim Seif Shariff Hamad akijiandaa kushiriki kampeni hizo kwanza awathibitishie wanachama wake ni lini ataapishwa kuwa Rais wa Zanzibar kama alivyowaahidi.

Kaimu Katibu Mkuu wa UVCCM, Shaka Hamdu Shaka amesema hayo jijini Dar es Salaam jana, mara baada ya kikao na watendaji wa sekretarieti za Wilaya za Dar es Saalam.

Shaka amesema Maalim Seif ni miongoni mwa wanasiasa ambao hawapaswi kusikilizwa na wananchi kutokana na kufanya siasa ionekane ni sehemu ya uongo kwani haaminiki.

“Maalim Seif kwanza awaambie wale aliowadanganya lini ataapishwa kuwa Rais wa Zanzibar, amewaongopea sana wanachama wake na sasa amechusha, kelele za kulilia urais wa Zanzibar kwa njia ya uongo zimezimika, tunamsubiri kwa hamu aje Kinondoani vijana tumejipanga kushughulika naye,” amesema.

Waziri Lukuvi atangaza uamuzi mzito Mwanza

$
0
0
WANANCHI wanaomiliki nyumba 664 katika mitaa ya Kigoto na Kabuhoro katika Kata ya Kirumba Manispaa ya Ilemela jijini Mwanza wametakiwa kuwa na subira wakati serikali ikitafuta ufumbuzi wa mgogoro uliopo kati yao na Jeshi la Polisi.

Pia wamezuiwa kujenga nyumba zingine mpya kwenye maeneo ya mitaa yao na badala yake wawe walinzi na kuonya watakaothubutu kujenga hawatalipwa fidia ambapo awali walitakiwa kuondoka na kupisha eneo hilo baada ya kuandikiwa ilani ya siku saba na jeshi la polisi.

Akizungumza na wananchi hao Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi William Lukuvi alisema serikali imesikia kilio chao na hivyo amekuja chunguza mgogoro huo ili ifanye uamuzi wa kuutatua.

 Alisema serikali inataka kufahamu mahitaji ya wananchi na polisi na kuonya wananchi wanaoishi kwenye maeneo hayo wasithubutu kujenga (kuongeza) majengo mengine zaidi ya yaliyopo sasa na watakaokaidi hawatalipwa fidia.

“Nimekuja kuangalia mgogoro huu na kuchungumza jambo hili ili serikali ifanye uamuzi. Msidhani nina majibu, majibu yatatolewa ndani ya mwaka mmoja lakini msituhubutu kuongeza nyumba zingine zaidi, kuweni walinzi wa maeneo haya na tunataka muwe maeneo mzuri ili tuwarasimishie,”alisema Lukuvi.

Waziri huyo wa ardhi alisisitiza baada ya uchunguzi atamshauri vizuri Rais John Magufuli namna ya kumaliza mgogoro huo baina ya wananchi na taasisi hiyo ya serikali.

Lukuvi alieleza eneo la Kigoto ambalo Polisi inadai inataka kujenga Chuo cha Polisi wanamaji, nyumba za askari na  gati la boti na meli za doria zinaweza kujengwa popote lakini eneo hilo lazima lipangwe upya hata kama matumizi yakibadilishwa kwa kuwa haiwezekani watu waishi kwenye nyumba za ovyo ovyo.

“Miaka 70 hadi leo kwa nini ujenzi haukuzuiwa,hakuna viongozi hapa na kama mngewashirikisha wangewasaidia kuzuia.Je, upembuzi yakinifu ulifanyika kwenye eneo mnalotaka kujenga mdomo huo wa gati la boti za polisi?

Aidha akizungumza kwa niaba ya wenzao ,Ferdinand Mtundubalo alimweleza Waziri kuwa hawana tatizo na ujenzi wa gati la boti za polisi isipokuwa warasimishiwe makazi yao ili waondokanane na mgogoro huo.

Katika hatua nyingine Waziri Lukuvi aliwataka wataalamu wa wa Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela waainishe eneo la Uwanja wa Ndege wa Mwanza na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) kikosi cha Ihale ili kila mmoja alinde eneo lake.

Pia alishauri eneo la Nyamwilolelwa litakalobaki baada ya kutengwa la uwanja wa ndege na JWTZ lipimwe wapewe wananchi wa eneo wapatao 1,961 na kuhusu barabara ya Mwanza –Igombe uamuzi wa Rais Magufuli ubaki ulivyo na uheshimiwe.

Aliyekuwa Mkurugenzi wa TBC Tido Mhando Afikishwa Mahakamani

$
0
0
Aliyekuwa  Mkurugenzi  wa  Shirika la Utangazaji la Taifa (TBC), Tido Mhando amefikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar leo kwa tuhuma za matumizi mabaya ya madaraka wakati akiwa TBC.

==>Habari Kamili inakuja

Chanzo cha Tatizo la Upungufu wa Nguvu za Kiume na Tiba Yake

$
0
0

Tendo la ndoa limengawanyika katika makundi matatu baadhi yake makudi hayo niuhanisi, kufanya tendo la ndoa maramoja na kushidwa kurudia tena 

sababu zinazo pelekea ni ugonjwa wa kisukari, kujichuwa, maumivu ya mgongo na kiuno, tumbo kuuguruma na kujaa gesi, msogo wa mawazo, presha, kutokuwa nyama sehemu ya haja kubwa yani mgoro, ulevu wa kupidukia, kuadhilika na madawa ya kulevya 

ARRBERA 1 Ni dawa ya asili ambayo imefanyiwa tafiti kwa hali ya juu isiyo na kemikali yoyote kwa mtumiaji ambayo humfanya mtumiaji kufanya tendo la ndoa maratatu bila kuchoka 

Pia ARRBERA 2 ni dawa asili abayo huimalisha ukuaji wa umbile la kiume lililo sinyaa na kunenepesha saizi upedayo. sihayo tu upade wa wamatatizo kisukari yakushuka na kupada kuna dawa ya kutumia siku saba na kufanya sukari ibaki nomo balasi abayo ni 4-5-6 vilevile kwaupade wa kina mama matatizo ya uzazi na hedhi kuvurugika na kutokwa maji maji sehemu za sili fagasi na kifafa cha mimba kwa kina mama waja wazito na kifafa cha kawaida 

FIKA OFISINI KWETU MBANGALA RAGI TATU ASIYE KUWA NA NAFASI HUDUMA YETU UTALETEWA POPOTE ULIPO KWA KWA KAZI WA DSM muone dr kabero simu 0758078280 au 0713 293 988 wote mnakalibishwa
No automatic alt text available.

Kwa Nini Wanaume Wengi Wanaupungufu Wa Nguvu Za Kiume Na Maumbile Madogo?

$
0
0
Asilimia 45 ya wanaume wapo tofauti na wengine kwa kuwatimizia vyema wake au wapenzi Wao na kuwasababishia kutoka nje ya ndoa zao.

NINI CHANZO CHA HAYO?Kupiga punyeto,Ngiri,Vidonda vya tumbo,Magonjwa ya moyo,Presha,Kisukari,Korodani moja kuvimba,Msongo wa mwazo,Kufanyiwa tohara ukiwa mtu mzima n.k.DOKTA MANYANDA sasa kapata tiba sahihi ya tatizo la NGUVU ZA KIUME.

MUHAMA:Hii hutibu na kuponyesha kabisa tatizo la nguvu za kiume,utakuwa na uwezo wa kurudia tendo zaidi ya mara tatu bila kuchoka na itakufanya uchelewe kufika kileleni kwa mda wa dakika 15-20.DAWA hii imechanganywa miti 12.Hata wazee wenye umri mkubwa wanapona kabisa.OKO NDOA YAKO SASA. 

MANGUNGU MIX: Ndio tiba tosha kwa sasa ambayo hurefusha na kunenepesha uume saizi uipendayo inch 1-8 na unene sentimita 1-5,dawa hii ipo ya kupaka na kunywa na haina madhara yoyote kwa mtumiaji.

NITOFAUTI NA ULIZO WAHI KUZITUMIA.Pia tuna dawa za kupatanisha mke,mme,mpenzi au bosi wako kwa mda mfupi sana,Uzazi,Kusafisha nyota,

Je unamali yako unauza hupati wateja?Wasiliana nami 0716-263605 

DOKTA MANYANDA ANAPATIKANA KASULU KIGOMA,Kwa wale wa mikoani huduma hii utaipata popote pale.

Rais Magufuli na Mkewe Wamemchangia Wastara Mil 15/= Za Matibabu

$
0
0
 Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike akiwasilisha mchango wa shilingi milioni 15 kwa mwigizaji Wastara  kutoka kwa Rais Dkt Magufuli na mkewe mama Janeth Magufuli kwa ajili ya matibabu. SHILAWADU ndio waliomuibua mwigizaji huyo kiasi hata ugonjwa wake uliwagusa wengi pamoja na JPM na mkewe.

Samike (wa pili kulia) akiwa na watangazaji wa kipindi cha SHILAWADU baada ya kumkabidhi Wastara fedha hiyo.
Katibu wa Rais Bw. Ngusa Samike akiwa na mwigizaji Wastara pamoja na SHILAWADU baada ya kumkabidhi msaada wa 15m/- kutoka kwa Rais Dkt Magufuli na mkewe mama Janeth Magufuli kwa ajili ya matibabu. Pia aliwasilisha mchango wa sh milioni moja na laki tisa toka kwa wasaidizi wa Rais. SHILAWADU ndio waliomuibua mwigizaji huyo kiasi hata ugonjwa wake uliwagusa wengi pamoja na JPM na mkewe.

WastaraAfunguka Baada ya Rais Magufuli Kumchangia Milioni 15

$
0
0
Msanii wa filamu nchini Wastara Juma amefunguka na kudai hakutegemea kama Rais Magufuli angeweza kulipa kipaumbele tatizo lake alilokuwa kwa sasa huku akimshukuru kwa kuweza kumsaidia suala hilo.

Wastara ameeleza hayo wakati alipokuwa akipokea pesa ya matibabu iliyotolewa na Rais Magufuli na mke wake Mama Janeth jumla ya milioni 15 ili iweze kumsaidia katika matibabu yake kama waliyovyoongea katika simu hapo awali.

"Kubwa niseme tu nashukuru, kwa sababu sikutegemea kama tatizo langu Mhe. Rais angeweza kulipa kipaumbele. Nashukuru pia naomba mpeleke salamu zangu kwa Mhe kwamba natamani siku moja nisimame ili niweze kuwa naye bega kwa bega katika kazi za kujenga nchi yetu ya Tanzania",alisema Wastara.

Pamoja na hayo Wastara ameendelea kwa kusema "natambua kuna watu wengi wana shida, mimi kama mimi natamani nifanye kazi yangu ili niweze kutoa 'percent' yangu niweze kuwasaidia na nimekuwa nikiomba sana muda mwingi jambo hilo".
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images