Quantcast
Channel: MPEKUZI
Viewing all 45270 articles
Browse latest View live

Serikali Kujenga Mtambo Wa Kuzalisha Umeme Wa Maji Mto Rufiji

$
0
0
Serikali inatarajia kujenga mradi mpya wa kuzalisha umeme  wa maji wa mega watt 2100 kwenye maporomoko ya mto Rufiji ambao utasaidia kuimalisha  miundombinu ya umeme na upatikanaji wa uhakika kwa wananchi.

Akizungumza wakati wa ziara ya siku moja ya  kikazi Wilayani Chato Mkoani Geita iliyokuwa na lengo la kukagua na kujionea miundombinu ya umeme wa Rea  awamu ya tatu ,Waziri wa Nishati ,Dr Medadi Kalemani ,alisema kuwa hali ya umeme inaendelea kuimarika siku hadi siku na kuna maeneo mengi yameanza kupata umeme wa kutosha.

“Hapo Nyuma mwezi Novemba tulikuwa tunajitahidi kukarabati mahali ambapo kulikuwa na ubovu wa mitambo lakini kwa sasa hali inaendelea vizuri maeneo mengi ya nchi yetu yanapata umeme kwa wingi  na  tunaanza kujenga mradi mpya wa kuzalisha umeme wa maji wa  mega watt 2100 kwenye maporomoko ya mto Rufiji  ambao utasaidia kuimalisha  miundo mbinu ya umeme na upatikanaji wa umeme hapa nchini”Alisema Kalemani.

Aidha Dr,Kaleman  amewasisitiza wananchi kutoa taarifa kwenye maeneo yao pindi kunapotoakea tatizo na kwamba wateja ambao wamelipia umeme kwa mwaka 2017 ni vyema Tanesco wakahakikisha wanawaunganishia umeme haraka iwezekanavyo kwani mwaka 2018 haitakiwi kuwepo kwa mteja ambaye ajaunganishiwa  huduma hiyo.

Kiwanda cha Alizeti Mount Meru Millers Ltd kimefungiwa

$
0
0
Serikali imekifungia Kiwanda cha kukamua mafuta cha  Alizeti Mount  Meru Millers Ltd   muda usiojulikana kwa madai ya kukaidi agizo la kulipa faini ya Sh20milioni.

Uamuzi wa kukifunga kiwanda hicho umetolewa  Jumatano na Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano na Mazingira ,Kangi Lugola  alipokuwa kwenye kwanda hicho kilichopo  kijiji cha Manguanjuki Manispaa ya Singida.

Kabla ya kutoa uamuzi huo  mbele ya kamati ya ulinzi na usalama ya wilaya ya Singida, Lugola alisema Novemba 29 mwaka jana, mtangulizi wake Luhaga  Mpina, aliuagiza uongozi wa  kiwanda hicho ulipe  faini ya Sh20milioni kwa kosa la kutiririsha  maji taka yenye kemikali kwenye makazi ya watu .

“Maji taka yameelekezwa kwenye makazi ya wananchi wanaokizunguka kiwanda .Pia maji  hayo yenye kemikali, yameelekezwa kwenye ziwa la Singidani lenye viumbe hai wakiwemo samaki. lakini hadi leo, agizo la Waziri  Mpina, halijatekelezwa’’ amesema Lugola na kuongeza kwamba

‘’Kutokana na  ukiukwaji wa  sheria za mazingira, Mpina alikipa adhabu ya kulipa faini  Sh20milioni ambayo haijalipwa hadi leo”, amesema Waziri Lugola kwa masikitiko.

Lugola amesema kwamba  kiwanda hicho kimetekeleza agizo la kununua mashine ya kutibu maji taka, lakini maji taka hayo, hayajaelekezwa kwenye mashine hiyo.

 “Maji hayo yenye kemikali bado yameendelea kuwa kero kwa wananchi hadi leo, na yanaathiri viumbe hai vilivyopo kwenye ziwa Singidani. Hii dharau kwa serikali haikubaliki”, amesema

Naibu waziri huyo, amesema  wananchi wanaozunguka kiwanda hicho wamekuwa wakitoa kilio chao serikalini kwa miaka minne, kwamba wanaathiriwa na maji yenye kemikali  na moshi mnene wa kiwanda cha Maount Meru.

“Binafsi leo nimefika kwenye kiwanda hiki na baada ya kufanya ukaguzi wa kina, nakiri kwamba kilio cha wananchi wa Manguanjuki ni cha kweli na kinahitaji tiba ya kudumu. Mkuu wa wilaya ya Singida, naagiza kuanzia sasa, usimamie kufungwa kwa kiwanda hiki”,amesema na kuongeza;

“OCD pia nakuagiza uwatafute Wakurugenzi wa kiwanda hiki Atul Nittal, Arvind Mittal na Tarsem Aggarwal, popote walipo na kuwakamata na kuwafikisha mbele ya vyombo vya sheria kwa kukaidi agizo la Serikali”.

Kwa upande wake meneja Uhusiano, Nelson Mwakambuta, amesema kiwanda hicho kimekuwa kikifanyiwa ukaguzi mara kwa mara na mamlaka mbalimbali. Lakini  wamekuwa wakiaambiwa na viongozi hao kuwa   kiwanda hicho, hakina tatizo lolote linalohusiana na kwenda kinyume na sheria za  mazingira.

“Kufungwa kwa muda usiojulikana kwa kiwanda hiki, kutaathiri ustawi wa watumishi wengi wa kiwanda na familia zao. Pia  wakulima wa zao la alizeti ndani na nje ya mkoa wa Singida, nao watakuwa wamepata pigo. Hatupingani na serikali tutatekeleza yale yote tuliyoagizwa”,amesema meneja huyo.

George Weah ndiye rais mpya Liberia

$
0
0
Aliyekuwa nyota wa soka, George Weah, ametangazwa mshindi wa uchaguzi wa marudio wa urais uliofanyika nchini Liberia.

Tume ya uchaguzi ya nchi hiyo ilisema kwamba Weah alipata asili mia 61.5 ya kura zote zilizopigwa na kupata ushindi kwenye kaunti 14 kati ya 15.

Weah, mwenye umri wa miaka 51, alikuwa anashindana na makamu wa rais Joseph Boakai, kila mmoja akitaka kujaza nafasi ya rais Ellen Johnson Sirleaf, ambaye anaondoka mamlakani baada ya mihula miwili inayoruhusiwa na katiba ya Liberia.

Sirleaf alimshinda Weah kwenye uchaguzi wa mwaka  2005, baada ya nchi hiyo ya Afrika Magharibi kuibuka kutoka kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Tume ya uchaguzi ilisema asilimia 56 ya wapiga kura walijitokeza, ambao ni wachache kuliko waliojitokeza tarehe 10 mwezi Oktoba, wakati wa duru ya kwanza ya uchaguzi huo.

Waangalizi walisema kwamba vituo vya kupigia kura wiki hii vilikuwa na utaratibu mzuri kuliko uchaguzi wa oktoba.

Mgombea mwenza wa Weah, Jewel Howard Taylor, ni mke wa zamani wa aliyekuwa rais wa Liberia Charles Taylor, aliyeanzisha vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini humo na ambaye anatumikia kifungo cha miaka 50 nchini Uingereza kwa majukumu yake katika ukatili uliotokea nchini Sierra Leone.

Weah alikuwa mwanasoka mwenye umaarufu mkubwa mnamo miaka ya 90. Alichezea timu kama vile Chelsea, Manchester City na AC milan.

UVCCM: Huu si wakati wa kuabudu cheo cha Mtu

$
0
0
Mwenyekiti wa Umoja wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) Taifa, Kheir James, amesema wakati wa kufanya kazi kwa woga ndani ya umoja huo umepitwa na wakati.

Akizungumza na wanachama wa CCM na jumuiya zake visiwani Zanzibar, alisema huu ni wakati wa kufanya kazi kwa ushirikiano badala ya kumuabudu mtu kutokana na cheo chake.

Alisema kiongozi anayejitambua ni yule anayefanya kazi kwa maslahi ya vijana wenzake na kilichobaki kwa sasa ni kupambana ili jumuiya hiyo ya vijana iweze kufika mbali kwa maslahi ya vijana na taifa kwa ujumla.

Aidha, alisema wakati wa vijana wanaopenda kulalamika umefika mwisho hivyo ni vyema wakajitahidi kufanya kazi bila ya upendeleo na woga.

Aliwataka viongozi wenzake katika jumuiya hiyo kuanza kuhakiki mali za chama na aliyekuwa haendani na kasi ya chama hicho awapishe wanaoweza.

"Umegombania nafasi na tumekupa, sasa tufanyeni kazi ili vijana wajue thamani ya uongozi," alisema.

Kheir alisema uhakiki wa mali za chama hicho kwa upande wa Zanzibar utafanywa na Wazanzibari wenyewe na atahakikisha anapatiwa ripoti ya uhakika kwenye taarifa watakazozipeleka kwa uongozi wa juu na uhakiki wa watumishi hewa pia utaangaliwa.

Makamo Mwenyekiti wa Umoja huo, Tabia Maulid Mwita, alisema yupo tayari kufanya kazi kwa ushirikiano wa hali ya juu na vijana wote na kuwashukuru kwa kumchagua kushika nafasi hiyo na kuendeleza ahadi zake alizoziahidi kipindi cha kampeni.

Aidha, aliwataka vijana kuacha makundi kwa kuwa uchaguzi umekwisha hivyo atahakikisha haki inatendeka bila ya kumuonea mtu wala kujali cheo chake na kufanya maamuzi kwa matakwa yake bila ya kumshauri mtu.

"Vijana ndio jeuri ya chama ila kwa anayejitambua na sio kukaa kutukana katika majukwaa kijana mzuri ni yule anayependa kusikiliza ushauri wa wakubwa wake," alisema.

Mapema akitoa utambulisho kwa viongozi, Kaimu Katibu wa Umoja huo Zanzibar, Abdulghafar Idirissa Juma, alisema Umoja huo utaangalia upya vitega uchumi vyake ili viweze kuleta tija kwa wanachama na kuiendeleza jumuiya yao.

Akizungumzia mradi wa Darajani alisema kuwa ulihodhiwa na baadhi ya viongozi wa serikali hivyo alimtaka Mwenyekiti wa Umoja huo kulifuatilia suala hilo ili mipango iendelee na mradi huo uweze kuleta tija kwa vijana na taifa kwa ujumla.

Malinzi na wenzake kula Mwaka Mpya mahabusu

$
0
0
Kesi  ya  kutakatisha Dola za Marekani 375,418 inayomkabili aliyekuwa Rais wa shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi na wenzake, imepigwa kalenda hadi Januari 11, 2018 baada ya upande wa Jamhuri kudai bado haujakamilika.

Hata hivyo,  upande wa utetezi uliiomba  Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,  Dar es Salaam, kuuamuru upande wa mashtaka kuharakisha upelelezi wa kesi hiyo.

Kesi hiyo ilitajwa jana na  Hakimu Mkazi Mkuu Wilbard Mashauri.

Wakili wa Serikali Mwandamizi, Leonard Swai, alidai kuwa  upelelezi bado haujakamilika, hivyo akaomba tarehe nyingine ya kutajwa.

Wakili wa utetezi, Nehemiah Nkoko, alidai kuwa kesi hiyo ni ya muda mrefu na kila siku wanaambiwa jalada bado lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP).

Hakimu Mashauri alisema mahakama hiyo inafanya kazi ya kutafsiri sheria na kama itafanya vinginevyo itakuwa nje ya sheria.

Alisema kesi hiyo itatajwa Januari 11, 2018 na washtakiwa wataendelea kukaa mahabusu.

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ni Katibu wa TFF, Mwesigwa Selestine na Mhasibu wa shirikisho hilo, Nsiande Mwanga ambao wanakabiliwa na mashtaka 28, ikiwamo ya utakatishaji fedha ambazo ni Dola za Marekani, 375,418.

Walichosema TAKUKURU Mahakamani kuhusu nyaraka walizoomba kutoka kwa Aveva

$
0
0
Upande wa Jamhuri katika kesi ya tuhuma za utakatishaji fedha inayowakabili waliokuwa vigogo wa Klabu ya Simba, Evance Aveva na Godfrey Nyange maarufu kama Kaburu, umedai mahakamani kwamba bado haujapokea nyaraka kutoka kwa rais huyo.

Madai hayo yalitolewa na Wakili wa Serikali, Leonard Swai, mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Victoria Nongwa, anayesikiliza kesi hiyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam.

Alidai kuwa kesi hiyo ilipangwa jana  kwa ajili ya kutajwa lakini upelelezi bado haujakamilika na kwamba bado wanasubiri nyaraka kutoka kwa Aveva.

"Mheshimiwa Hakimu, upande wa Jamhuri bado hatujakabidhiwa nyaraka tulizoomba kutoka  ofisi ya Aveva ili wakamilishe upelelezi," alidai Swai.

Hata hivyo, upande wa utetezi alidai kuwa wameipokea barua ya Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa  (Takukuru) kuhusu maombi hayo na wanayafanyia kazi.

Hakimu Nongwa alisema kesi hiyo itatajwa  Januari 11, 2018 na washtakiwa wataendelea kukaa mahabusu.

Awali, upande wa Jamhuri  uliomba ufunguo kutoka kwa Aveva ili kuwawezesha kupata nyaraka hizo ikiwa ni sehemu ya kukamilisha upelelezi.

Katika kesi ya msingi, Aveva na makamu wake Kaburu wanakabiliwa na mashtaka matano ya kughushi, kuwasilisha nyaraka ya uongo na kutakatisha fedha dola za Marekani 300,000.

Washtakiwa hao wanadaiwa kula njama ya kughushi fomu ya maombi ya kuhamisha fedha ya Machi 15,2016 wakionesha Klabu ya Simba inalipa mkopo wa  dola 300,000 kwa Evans Aveva wakati si kweli.

Swahiba Amtandika Mshale Na Kumuua Rafiki Yake Kisa Deni la Sh, 4,000

$
0
0
Mkazi wa Mtaa wa Kilimahewa katika Halmashauri ya mji wa Bunda mkoani Mara, Paul Juma (38), ameuawa kwa kuchomwa mshale na rafiki yake, baada ya kutokea ugomvi kati yao.

Inadaiwa ugomvi huo ulitokana na kumdai amuongeze Shilingi 4,000 kutokana na kumuuzia mabati manne chakavu kwa jumla ya Sh. 20,000.

Kamanda wa Polisi mkoani Mara, Kamishna Msaidizi wa Polisi Jafari Mohamed, jana alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kumtaja mtuhumiwa kuwa ni Julius Mtoni (48) mkazi wa mjini Bunda na watu hao walikuwa ni marafiki.

Kamanda Mohamed alisema tukio hilo lilitokea Desema 26 majira ya mchana wakati watu hao walipokuwa wanakunywa pombe ya kienyeji kwa mwanamke ambaye ni jirani yao.

Polisi wilayani hapa walisema Desemba 25, marehemu alimuuzia mtuhumiwa mabati manne chakavu kwa makubaliano ya kila bati Sh. 7,000.

Walisema kuwa siku hiyo mtuhumiwa huyo alimpatia marehemu Sh. 20,000 taslimu na kukubaliana kuwa atalipwa kiasi kingine cha Shilingi 8,000 kilichobakia siku nyingine.

Walisema Desemba 26 wakiwa wanakunywa pombe, marehemu alimdai mtuhukiwa amlipe Sh. 8,000 zilizokuwa zimesalia, lakini alimpatia Sh. 4,000 ndipo wakaanza kuzozana huku marehemu akishinikiza alipwe deni lake lote la Sh. 8,000.

Aidha, ilielezwa kutokana na kutokuelewana, marehemu alianza kumkaba mtuhumiwa, kisha kukimbilia nyumbani kwake na kuchukua upinde na kumfyatulia mshale ambao ulimpata begani.

Polisi walisema kuwa baada ya marehemu kuchomwa mshale huo aliuvunja na kubakiza kipande cha mshale huo mwilini mwake na kukimbilia polisi, lakini  alipoteza maisha kutokana na kutokwa na damu nyingi.

“Baada ya kuchomwa mshale huo marehemu aliuvunja na kubakiza kipande kikiwa mwilini mwake na kuja hapa polisi kisha hospitalini, lakini taarifa ya hospitali inaeleza alikufa baada ya kutokwa na damu nyingi,” alisema ofisa mmoja wa polisi ambaye hakuwa tayari kutaja jina lake kwa madai sio msemaji wa jeshi hilo.

Hussein Bashe : "Taasisi za Dini zina haki ya kutoa maoni yao juu ya siasa"

$
0
0
Wakati Jeshi la Polisi Tanzania kupitia kanda maalum ya Dar es salaam likitangaza kuwa lazima litamhoji Askofu na kiongozi wa kanisa la Full Gospel Bible Fellowship Zachary Kakobe kwa madai ya kutoa maneno ya kashfa kwenye mahubiri yake, wapo Wanasiasa walioguswa na taarifa hii na mmoja wapo ni Mbunge wa Nzega Mjini Hussein Bashe.

Kupitia akaunti ya twitter Mbunge Hussein Bashe ameandika ;"Kesho tutazitaka Taasisi za Dini zihamasishe amani,Maendeleo, zipongeze ni muhimu kukubali kukosolewa, Serikali haitakiwi kufanya hivi kama hazivunji sheria.

"Taasisi za Dini zina haki ya kutoa maoni yao juu ya siasa,Uchumi na maswala yote ya kijamii, viongozi wa Dini wana nafasi yao"


Habari Zilizopo Katika Magazeti ya Leo Jumamosi ya Disemba 30

Serikali yawatoa hofu wananchi kuhusu deni la Taifa

$
0
0
Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango imewatoa hofu wananchi kuhusu uvumi wa kuongezeka kwa deni la Taifa kwamba deni hilo ni himilivu na liko chini ya ukomo wa hatari.

Hayo yamesemwa Jijini Dar es Salaam  na Waziri wa Fedha na Mipango Dkt. Philipo Mpango wakati akitoa mwenendo wa  hali ya uchumi na utekelezaji wa bajeti  ya Serikali kwa mwaka 2017/2018.

Dkt. Mpango alisema kuwa katika tathimini iliyofanyika mwezi Novemba mwaka huu inaonesha kuwa uwiano wa deni hilo na pato la Taifa ni asilimia 32.5 likilinganishwa na ukomo wa asilimia 56.

“Katika kuangalia ukomo wa deni hili ambao uko chini, inaonesha kuwa deni hili ni himilivu  katika kipindi cha muda wa kati na muda mrefu,” alisema Dkt. Mpango.

Akieleza takwimu hizo, Waziri Mpango amesema kuwa mwishoni mwa mwezi Septemba mwaka huu, deni la Taifa lilifikia shilingi bilioni 47,823.1 ikilinganishwa na bilioni 42,552.4 katika kipindi kama hicho mwaka 2016 ambapo kati ya kiasi hicho, shilingi bilioni 13,417.5 ni deni la ndani sawa na asilimia 28.1 na shilingi bilioni 34,405.6 ni deni la nje ambalo ni sawa na asilimia 71.9.

Dkt. Mpango alisisitiza kuwa ongezeko hilo lilitokana na kupatikana kwa mikopo mipya ya nje na ndani ya nchi kwa ajili ya kugharamia miradi ya maeneeleo.

Aliitaja miradi hiyo kuwa ni ujenzi wa mradi wa umeme Kiwira (Kiwira Coal Mine), miradi ya uboreshaji wa huduma za maji kwa jamii, mradi mkubwa wa kuzalisha umeme wa kinyerezi na ujenzi na ukarabati wa viwanja vya ndege ambapo miradi hiyo  itawezesha watanzania kufika uchumi wa kati wenye viwanda.

“Mambo muhimu ya kujiridhisha nayo ni kwamba mikopo inayokopwa itumike katika kujenga uwezo zaidi wa kuzalisha mali na huduma nzuri kwa watanzania,” alisisitiza Dkt. Mpango.

Aidha Waziri Mpango amesema kuwa kufuatia hatua zinazochukuliwa na Serikali, ukwasi kwenye benki za biashara uliongezeka na kusaidia kupungua kwa riba ya mikopo baina ya mabenki na kufikia wastani wa asilimia 3.53 mwezi Novemba mwaka huu kutoka wastani wa asilimia  14.93 kwa nusu ya kwanza ya mwaka 2016/2017.

Vilevile riba za dhamana za Serikali zilishuka kutoka wastani wa asilimia 15.56 katika nusu ya kwanza ya mwaka 2016/2017 hadi asilimia 8.76 mwezi Novemba, 2017 na kuongeza kuwa Serikali inatarajia kasi ya ukuaji wa mikopo kwa sekta binafsi itaanza kuimarika.

Aidha, Dkt. Mpango amewaonya watu wanaotoa takwimu za uongo kuacha mara moja kwani wanaipotosha jamii, huku akiwataka waandishi wa habari kupata takwimu maalumu kutoka Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) ili kuweka takwimu sahihi.

Waziri Mkuu apokea wanachama 60 wa CUF

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amepokea wanachama wapya 60 kutoka Chama cha Wananchi (CUF) ambao wameamua kurejea Chama cha Mapinduzi (CCM).

Wanachama hao wamepokelewa jana mchana (Ijumaa, Desemba 29, 2017) kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Nkowe kata ya Nkowe, wilayani Ruangwa mkoani Lindi.

Kabla ya kuwakabidhi kadi za CCM, Waziri Mkuu alipokea kadi za CUF kutoka kwa vijana saba kwa niaba ya wenzao 60. Vijana hao ni Hamisi Juma, Fatuma Abdallah, Mwajuma Mohammed, Thomas Moto, Zainab Nachiluku, Samia Said na Juma Said.

Vijana hao saba waliokabidhiwa kadi mpya za CCM pamoja na wenzao 53, walikula kiapo cha uaminifu.

Kwa mujibu wa Katibu wa CCM wa wilaya hiyo, Bw. Barnabas Essau wanachama wote ni vijana ambao wanajishughulisha na shughuli mbalimbali na wameridhishwa na utendaji wa Serikali ya awamu ya tano.

Bw. Essau alisema wanachama hao wote wametoka vijiji vya Kipindimbi, Nkowe na Mpumbe.

Novemba 5, mwaka huu, Waziri Mkuu alipokea wanachama 37 kutoka vyama vya CUF na CHADEMA kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kijiji cha Mbekenyera, wilayani Ruangwa.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Waziri Mkuu Awasilisha Tamko La Maadili Ya Viongozi Wa Umma

$
0
0
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema amekwishawasilisha tamko la maadili ya viongozi wa umma kwenye Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma tangu  Alhamisi Desemba 28, 2017.

Akizungumza na waandishi wa habari kijijini kwake Namahema ‘A’ wilayani Ruangwa mkoani Lindi jana jioni (Ijumaa, Desemba 29, 2017), Waziri Mkuu alisema fomu hizo zilipokelewa  na amekwishapatiwa barua ya kupokea tamko hilo.

“Nimewaita hapa ili kuthibitisha kuwa nimetekeleza takwa hilo la kisheria na tayari Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi ya Umma imekiri kupokea tamko langu kwa barua hii hapa,” alisema Waziri Mkuu huku akionyesha barua hiyo ambayo ilisainiwa na Jaji Harold Nsekela, Desemba 28, 2017.

“Kwa kuzingatia mfano ulioonyesha na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli, ninawaagiza viongozi wote wanaotakiwa kujaza fomu hizo kwa mujibu wa sheria wafanye hivyo na kuziwasilisha ifikapo tarehe 31 Desemba, 2017 saa 10 jioni,” alisisitiza Waziri Mkuu.

Alisema anawakumbusha Mawaziri, Naibu Mawaziri, Makatibu Wakuu, Naibu Makatibu Wakuu wote na viongozi wote walioko kwenye ngazi za uteuzi wahakikishe wanatimiza takwa ambalo liko kwa mujibu wa kifungu cha 9 na cha 11 cha Sheria ya Maadili ya Viongozi wa Umma Na. 13 ya Mwaka 1995.

Wakati huohuo, Waziri Mkuu ametumia fursa hiyo kuwatakia Watanzania wote heri wakati wanaposubiri kumaliza mwaka 2017 na kuwatakia heri na fanaka katika maeneo waliyopo wanapojiandaa kuupokea mwaka 2018.

IMETOLEWA NA:
OFISI YA WAZIRI MKUU,

Serikali Yasikia Kilio Cha Wadau Wa Sekta Ya Uwindaji Wa Kitalii Nchini, Yaongezea Miaka Miwili Ya Umiliki Wa Leseni Za Vitalu

$
0
0
Serikali imesikia kilio cha wadau wa sekta ya uwindaji wa kitalii nchini na kuamua kuongeza muda wa miaka miwili ya umiliki wa leseni za vitalu 95 vya uwindaji wa kitalii ambazo zilikuwa ziishe muda wake tarehe 31 Desemba mwaka huu (2017).

Uamuzi huo umefikiwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla wakati wa kikao cha majumuisho na watendaji wa Wizara hiyo muda mfupi baada ya kumalizika kwa mkuano wa wadau wa sekta hiyo ulioandaliwa na Wizara hiyo mjini Dodoma jana.

Akizungumzia uamuzi huo Dk. Kigwangalla alisema, lengo ni kuwapa muda wawekezaji hao ili waweze kujiandaa na mabadiliko ya mfumo mpya wa utowaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada ikiwemo kurudisha baadhi ya gharama za uwekezaji walizoweka katika vitalu hivyo.

Awali akizungumza katika mkutano huo wa wadau Mwenyekiti wa Chama cha Wamiliki wa Kampuni za Uwindaji wa Kitalii nchini, Michael Mantheakis alimuomba Waziri Kigwangalla kuwaongezea muda wa umiliki wa leseni zao kuanzia miaka mitano au mitatu na nusu ili waweze kurudisha gharama za uwekezaji walizowekeza katika vitalu hivyo ikiwemo ujenzi wa miundombinu, makambi na vifaa vyake pamoja na maji.

Hata hivyo, Waziri Kigwangalla aliweka wazi msimamo wa Serikali wa kutimiza azma yake ya kuingia kwenye utaratibu mpya wa utoaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada na kusema kuwa kamwe haitorudi nyuma na kwamba utekelezaji wa zoezi hilo hauwezi kusubiri muda mrefu kiasi hicho.

Akizungumzia kuhusu hatua ya utekelezaji wa utaratibu huo,
Waziri Kigwangalla alisema kwa sasa taratibu za kuandaa Sheria za usimamizi zinaendelea na zinatarajiwa kukamilika mwezi Februari 2018 pamoja na kanuni zake zinazotarajiwa kukamilika mwezi Aprili 2018.

Aidha, alisema mfumo maalumu wa kielektroniki unaandaliwa ambapo maombi yote ya leseni za umiliki wa vitalu vya uwindaji kwa njia ya mnada yatafanyika kwa uwazi kwa njia ya mtandao.

Alisema baada ya kukamilika kwa taratibu zote na mfumo huo mpya wa utoaji wa leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii kwa njia ya mnada na maombi kuwasilishwa, mnada wa kwanza utaanza tarehe 1 Julai, 2018 kwa kuanza kunadi vitalu 61 ambavyo kwa sasa havina wawekezaji.

Mnada wa pili utafanyika mwaka 2020 baada ya kuisha kwa muda huo wa nyongeza wa miaka miwili ukihusisha vitalu 95 vilivyoongezewa muda wa umiliki wa leseni pamoja na vitalu vingine endapo vitabaki katika mnada huo wa kwanza kwa sababu mbalimbali.

Alisema sheria na kanuni zinazoandaliwa hivi sasa zitazingatia mambo muhimu ikiwemo kuwapa nafasi watanzania wenye mitaji midogo kuweza kuingia kwenye biashara hiyo pamoja na kuweka adhabu kali dhidi ya wafanyabiashara watakaohujumu biashara hiyo kwa makusudi.

Mkutano huo wa siku moja ulihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Meja Jenerali Gaudence Milanzi, Naibu Katibu Mkuu, Dk. Aloyce Nzuki, wakurugenzi, wakuu wa vitengo na wakuu wa taasisi zilizopo chini ya wizara hiyo na waandhishi wa habari.

Oktoba 22 mwaka huu (2017) wakati akiongoza kikao cha wadau wa sekta ya Maliasili na Utalii mjini Dodoma, Waziri Kigwangalla alitangaza kufuta leseni za vitalu vya uwindaji wa kitalii zilizokuwa zianze mwezi Januari, 2018 ili kupisha utarartibu mpya wa utoaji wa leseni hizo kwa njia ya mnada ikiwa ni mkakati wa Serikali wa kuimarisha sekta hiyo.

Taarifa Ya Serikali Kuhusu Mwenendo Wa Hali Ya Uchumi Na Utekelezaji Wa Bajeti Ya Serikali Kwa Mwaka 2017/18

$
0
0
UTANGULIZI
Nashukuru sana kupata fursa nyingine ya kuzungumza nanyi leo tunapokaribia mwisho wa mwaka 2017. Lengo la Serikali ni kuwapatia Watanzania taarifa rasmi kuhusu (i) mwenendo wa uchumi wa Taifa kwa kipindi cha Januari hadi Juni 2017 na kwa miezi ya hivi karibuni pale ambapo tunazo takwimu, (ii) utekelezaji wa bajeti ya Serikali 2017/18 hadi sasa, (iii) changamoto zilizopo mbele yetu na matarajio mpaka Juni 2018. Aidha, nitatoa ufafanuzi kwa lugha nyepesi katika baadhi ya maeneo ambayo yamekuwa hayaelezwi ipasavyo au yanapotoshwa hususan katika mitandao ya kijamii na baadhi ya vyombo ya habari.

1.   MWENENDO WA UCHUMI WA TAIFA
Tunapozungumzia mwenendo wa uchumi tunaangalia viashiria mbalimbali. Niruhusuni nieleze baadhi ya viashiria muhimu kama ifuatavyo:
 
1.1        Ukuaji wa Uchumi
Kiashiria kimojawapo kinachotumika sana kimataifa kupima mwenendo wa uchumi ni ukuaji wa Pato la Taifa. Ukuaji wa Pato la Taifa ni badiliko (katika asilimia) la thamani ya bidhaa na huduma zilizozalishwa kutokana na shughuli mbalimbali za kiuchumi katika nchi zilizofanyika katika kipindi husika ikilinganishwa na kipindi sawia cha nyuma. Shughuli za kiuchumi zinajumuisha kilimo cha mazao, misitu, ufugaji na uvuvi; uzalishaji viwandani; biashara; ujenzi wa nyumba na barabara; huduma za fedha; habari na mawasiliano; usafiri na usafirishaji; huduma za utalii; na utoaji wa huduma nyingine kwa jamii ikiwa ni pamoja na afya, elimu na maji. Kiashiria hiki ni cha msingi kwa sababu kina uhusiano wa moja kwa moja na viashiria vingi vya mwenendo wa uchumi.
 
Katika nusu ya kwanza ya mwaka 2017 (Januari - Juni), Pato la Taifa (kwa bei za mwaka husika) liliongezeka na kufikia shilingi milioni 25,535,852 ikilinganishwa na shilingi milioni 23,915,750 katika kipindi kama hicho mwaka 2016. Hata hivyo, katika kipindi cha nusu ya kwanza ya mwaka 2017, Pato la Taifa lilikua kwa asilimia 6.8 ikilinganishwa na asilimia 7.7 katika kipindi kama hicho mwaka 2016. 
 
Ufafanuzi: (a) Ukuaji wa uchumi hauendi wima au katika mstari ulionyooka. Mara zote huenda kama wimbi lenye ukubwa tofauti tofauti hasa pale ambapo uzalishaji wa bidhaa au huduma unapokuwa wa msimu (mfano msimu wa mavuno ya mazao ya kilimo au utalii). Hivyo wale wanaodhani ukuaji wa uchumi unatakiwa uongezeke katika kila kipindi wanakosea. (b) Aidha, pale ambapo kasi chanya ya ukuaji wa uchumi imepungua, haimaanishi kuwa uchumi umeporomoka. La hasha! Uchumi unakuwa umeporomoka kama unakua kwa kiwango hasi (negative GDP growth). Kasi ya ukuaji wa uchumi inaweza kufananishwa na mwendo wa gari. 

Gari linalokwenda mwendo kasi maana yake gari hilo hutumia muda mfupi kufika mwisho wa safari lakini kama gari hilo litakwenda kwa mwendo mdogo haina maana kwamba haliendi mbele au linarudi nyuma bali litachukua muda zaidi kufika. (c) Pamekuwepo hoja kuwa kasi hii kubwa ya ukuaji wa uchumi ni ya kitakwimu tu na haiakisi hali halisi ya maisha ya watu. Hili ni suala pana kidogo. 

Kwanza, ili kasi kubwa ya ukuaji wa uchumi iweze kuwanufaisha wananchi wengi sharti wananchi wengi wawe wanafanya kazi katika sekta zinazokua haraka ili kujipatia kipato. Lakini ilivyo hapa nchini kwa sasa wananchi wengi wanaishi vijijini na wanategemea kilimo ambacho kasi ya ukuaji wake bado ni ndogo (asilimia 2.1 mwaka 2016) kutokana na tija ndogo na kutegemea mvua. Sekta zinazokua haraka (Ujenzi 13%, Habari & Mawasiliano 13%, Usafirishaji na Uhifadhi wa Mizigo 11.8%, Uchimbaji wa Madini na Mawe 11.5%, Shughuli za Fedha & Bima 10.7%) haziajiri wananchi wengi. 

 Kwa maneno mengine kasi kubwa ya ukuaji wa Pato la Taifa utawagusa wananchi wengi kutegemea na mgawanyo wa hilo Pato la Taifa. Pili, kasi ya ongezeko la watu hapa nchini ni kubwa (2.7%) na hivyo inatengeneza idadi kubwa ya watu kugawana Pato dogo la Taifa. Tatu, pamoja na changamoto hizo nilizoeleza, napenda nisisitize kuwa kasi kubwa ya ukuaji wa uchumi ndiyo msingi wa kuboresha hali ya maisha katika nchi. Hili halina mbadala. Kama uchumi haukui, kipato hakiwezi kuongezeka!
 
Pamoja na kasi ya ukuaji wa uchumi kupungua kidogo katika kipindi cha nusu ya kwanza ya 2017 ikilinganishwa na kipindi kama hicho mwaka 2016, bado Tanzania ndiyo nchi iliyokuwa na kiwango kikubwa cha ukuaji wa uchumi ukilinganisha na nchi nyingine wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (Jedwali Na. 1). 
 
NB: Chanzo cha takwimu hizi ni Benki ya Dunia ambao hivi majuzi Mwakilishi wake hapa nchini alikiri kuwa Tanzania ni moja ya nchi za Afrika yenye takwimu bora.
 
Jedwali Na. 1: Ukuaji wa Pato la Taifa Katika Baadhi ya Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki katika kipindi cha nusu mwaka (%)
NCHI
2016
2017
Kenya
5.9
4.9
Rwanda
8.1
2.9
Tanzania
7.7
6.8
Uganda
3.8
4.9
Ethiopia
10.5
7.5
Democratic Republic of the Congo
8.5
9.0
Cote d’Ivoire
7.7
7.5
Mozambique
7.3
7.3
Chanzo: Ofisi ya Taifa ya Takwimu; na CIA World Factbook
 
Hata kwa bara la Afrika na dunia kwa ujumla, Tanzania inabaki kuwa miongoni mwa nchi 10 bora kwa kuwa na kasi kubwa ya ukuaji wa uchumi. Kwa mwaka mzima wa 2017, uchumi unatarajiwa kukua kwa asilimia 7.0 na kuendelea kukua kwa wastani wa asilimia 7.4 katika kipindi cha muda wa kati. 

==>Endelea Nayo Kwa Kubofya  <<HAPA>>

Waziri Jafo Avitaka Vituo Vyote Vya Afya Kutengeneza Bustani Za Kupumzikia!

$
0
0
Nteghenjwa Hosseah, TAMISEMI.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amevitaka vituo vyote vya Afya Nchini sambamba na hospital za Wilaya kutengeneza bustani ya kupumzikia kwa wagonjwa wanaosubiria matibabu katika maeneo hayo.

Waziri jafo ameyasema hayo wakati akikagua Ujenzi wa miundombinu ya Afya katika Kituo cha Afya Makole kilichopo Manispaa ya Dodoma na kuutaka uongozi wa Kituo hicho kutenegenza bustani ya kisasa pamoja na kupanda miti ya kutosha ili kutunza matunzingira lakini kupendezesha eneo la hospital.

“Hili Agizo liende kwa Vituo vyote Nchini pamoja na Hospital za Wilaya zilizoko chini ya TAMISEMI kuhakikisha wanaekeleza maelekezo haya katika ameneo yote nataka hospital iwe sehemu ya kupa faraja mgonjwa kwa kupata huduma nzuri lakini pia kusubiria huduma hiyo katika maeneo yanayovutia wakati wote” Alisema Waziri Jafo.

Akikagua majengo matano yanayojengwa katika Kituo hicho cha Afya na kusimamiwa na TAMISEMI Waziri Jafo amesema ameridhishwa na Ujenzi wa miundombinu hiyo ya Afya katika Hospital ya Makole  kwani umefuata ramani zilizotolewa na Wizara, unajengwa kwa ubora na uko ndani ya muda wa Utekelezaji.

“Hivi ndio ninavyotaka wataalamu wangu kujiongeza katika baadhi ya maeneo mfano hapa Mmejenga Mabara kubwa kulingana na wingi wa wagonjwa mnaowahudumia kwa siku sasa sio kwa sababu ramani imeonyesha maabara ndogo basi kila mtu anafuata hivyo hivyo ni lazima tujiongeze kulingana na mahitaji ya ameneo yetu ya huduma” Alisema Waziri Jafo.

Akizungumzia maendeleo ya mradi Mganga Mfawidhi wa  Kituo cha  Afya Makole  amesema Ujenzi huu umesema ujenzi wa Maabara, chumba cha Upasuaji, Wodi ya Kina Mama, Nyumba ya Mganga pamoja na Ukarabati wa Kichomea Taka utakamilika mapema mwezi February 2017 na Fedha zilizopokelewa kwa ajili ya ujenzi huo zitatosha na kukamilisha ujenzi wa miundombinu yote.

Kituo cha Afya Makole ni miongoni mwa vituo 211 Nchini vilivyopokea/vitakavyopokea  Fedha kwa ajili ya ujenzi wa miundombinu mbalimbali ya Afya lengo ikiwa ni kuboresha Miundombinu ya Afya ili kuweza kutoa huduma bora kwa watanzania.

PolePole: Hakuna Kiongozi wa Dini ametishwa kwa kusema ukweli Tanzania

$
0
0
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Humphrey Polepole amewazungumzia Askofu Zakaria Kakobe pamoja na baadhi ya viongozi wengine wa dini na kusema kuwa hakuna mtu ambaye amezuiliwa kuongea Tanzania na kuwa wapo huru kutoa maoni yao.

Polepole alisema hayo juzi wakati akihojiwa na kituo kimoja cha Television na kusema hakuna mtu ambaye ametishwa kwa kusema ukweli juu ya jambo fulani ambalo huenda lipo au linatokea Tanzania.

"Hakuna mtu amezuiliwa kuongea ukweli ndani ya nchi ya Tanzania, hakuna mtu ametishwa kwa kusema ukweli na hasa katika uongozi wa awamu ya tano chini ya Rais Dkt. John Pombe Magufuli, anayesema mtu Tanzania kuna mtu kazuiliwa kuzungumza uhuru wake wa maoni nadhani atakuwa na matatizo ila nachofahamu kwamba mtu kuzungumza lugha ya matusi kwa mujibu wa Katiba yetu na sheria zetu ni makosa" alisema Polepole

Polepole aliendelea kusisitiza kuwa viongozi hao wa dini wapo wazi na huru kusema chochote kile kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 

"Wapo huru kusema chochote kwa mujibu wa Katiba yetu ya nchi na sheria za nchi na nitasema neno moja dogo kitu ambacho na mimi ninatoa rai, nitakapokaa vizuri nitafafanua vizuri mambo haya lakini ukiwa kiongozi yoyote yule kauli ni jambo la msingi sababu una watu wanakufuata" alisisitiza Polepole

Juzi Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Ndani, Meja Jenerali Mst. Projest Rwegasira, ilitoa onyo na kuwataka viongozi wa jumuiya za kidini kutotumia mahubiri yao ya ibada kwa kufanya uchambuzi wa masuala ya siasa.

Mkuu wa Mkoa wa Arusha Ampa Makavu Askofu Kakobe

$
0
0
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo amesema kuwa kuna haja kubwa ya kuyafanyia uchanguzi makanisa ili kuweza kujua makanisa halisi ili kuweza kutofatisha na mawakala wa shetani.

Ameyasema hayo jijini Arusha ambapo amesema kuwa baadhi ya makanisa yamekuwa yakiwapotosha wananchi kwa kuwajaza imani isiyokuwa ya kibinadamu.

Amesema kuwa historia ya mchungaji Kakobe inatia mashaka kwani amebeba vyeo vyote vya kanisa hata anaposafiri huwawekea waumini wake ‘Cassete’ ili wamsikilize akiwa safarini.

“Kuna watu wengine ni mawakala wa shetani, hivyo kuna kila haja ya kuanza kufanya uchambuzi wa makanisa haya ambayo yamekuwa yakipotosha Watanzania, unaofanywa na anayejiita Askofu Kakobe ni umburula,”amesema Gambo

Hata hivyo, ameongeza kuwa taasisi ya dini ina utaratibu wake inaheshimika, ina mfumo wake na inathaminika katika jamii.

==>Msikilize hapo chini

Benki Kuu ( BOT ) yaiagiza Airtel kupeleka taarifa zake za Fedha tangu mwaka 2000

$
0
0
Kufuatia sakata la umiliki wa kampuni ya mawasiliano ya Airtel, Benki Kuu ya Tanzania (BoT) Disemba 28, 2017 iliziandikia benki zote na taasisi za kifedha ambazo zimekuwa zikisimamia akaunti za iliyokuwa Celtel, Zain au Airtel kuwasilisha taarifa hizo.

BoT imezitaka taasisi hizo ama benki kueleza kama zimewahi kuendesha ama zinaendesha akaunti zinazohusiana na kampuni tajwa.

Aidha, taasisi zote ambazo zitakuwa zina akaunti za kampuni hiyo tajwa, zimetakiwa kuwasilisha jina la akaunti, namba ya akaunti, aina ya fedha zilizomo kwenye akaunti na kiwango cha mwisho kilichokuwemo kwenye akaunti hadi Disemba 27, 2017.

Taarifa za akaunti hizo zinazotakiwa kuwasilishwa ni kaunzia Januari 1, 2000 hadi Disemba 27, 2017.

Taarifa zinazotakiwa kuwasilisha zinatakiwa kuwa katika nakala ngumu (hardcopy) na nakala teke (soft copy) na zilitakiwa kuwasilishwa  jana saa 5 asubuhi.

Tundu Lissu atoa waraka mzito

$
0
0
Ikiwa imebaki siku moja kabla ya kuuaga mwaka 2017, mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu ametoa waraka akilaani ukiukwaji wa haki za binadamu na kuminywa kwa uhuru wa kutoa mawazo.

Waraka huo alioutoa jana Alhamisi Desemba 28,2017 akiwa katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya anakopatiwa matibabu tangu Septemba 7,2017 aliposhambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi kwenye makazi yake Area D mjini Dodoma.

Lissu pia amezungumzia tukio la kutoweka mwandishi wa habari wa kujitegemea wa kampuni ya Mwananchi Communications Ltd (MCL), Azory Gwanda ambaye leo ni siku ya 39 tangu alipotoweka akiwa wilayani Kibiti mkoani Pwani anakofanyia kazi zake.

“Watanzania ambao wamekuwa wakitumia uhuru wao wa maoni kutoa mawazo wamekuwa wakikamatwa na kushtakiwa mahakamani... mwanachama wa Chadema, Ben Saanane na mwandishi wa Mwananchi (Azory Gwanda) wametoweka na hawajulikani walipo. Hakuna uchunguzi au taarifa za kutoweka kwao,” amesema. 

Lissu ambaye pia ni mwanasheria wa Chadema amesema vyombo vya habari  vimekuwa katika wakati mgumu baada ya kukutana na mkono wa sheria, ikiwamo kufungiwa pale vinapoandika habari zinazotafsiriwa kuwa ni za kichochezi au uongo.

Kupitia waraka huo alioupa jina ‘Barua kutoka kitanda cha Hospitali ya Nairobi’ amezungumzia pia mambo yaliyojitokeza na yanayoendelea katika kipindi cha miaka miwili ya utawala wa Serikali ya Awamu ya Tano.

Waraka huo ameutoa siku tatu baada ya kusimama kwa mara ya kwanza tangu Septemba 7,2017 aliposhambuliwa na kujeruhiwa kwa risasi.

Amesema kumekuwa na ukiukwaji wa haki za binadamu na utawala bora, huku viongozi wa upinzani na wanaharakati wakikamatwa na kuwekwa mahabusu.

Lissu amesema kutokana na watawala kuwashughulikia wanaowakosoa, uhuru wa kutoa maoni umeminya na mijadala haipo.

“Mikutano ya kisiasa imezuiwa na polisi, viongozi wanakamatwa, wabunge nikiwemo mimi (Lissu) tumekamatwa mara nyingi kwa sababu zinazohusu majukumu yetu ya kazi,” amesema.

Amesema, ‘’Hakuna njia rahisi kufikia uhuru sehemu yoyote na wengi wetu tutapitia bonde la kivuli cha kifo kabla ya kufikia mlima wa matamanio yetu.”

Pia, amevilaumu vyombo vya dola akisema tangu Septemba 7,2017 aliponusurika kuuawa akiwa eneo lenye ulinzi mpaka sasa hakuna mtuhumiwa hata mmoja anayeshikiliwa kuhusika na tukio hilo.

Kuhusu onyo la Serikali kwa viongozi wa dini kutojihusisha na masuala ya kisiasa lililotolewa  Alhamisi Desemba 28,2017 na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Lissu amesema ni mwendelezo wa kuwazuia watu wasitumie uhuru wao kuzungumza na kukosoa.

PICHA: Tundu Lissu Ameweza Kukaa Mwenyewe

$
0
0
Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu (Chadema) amekaa mwenyewe pasipo msaada wa madaktari katika Hospitali ya Nairobi nchini Kenya, anakotibiwa baada ya kushambuliwa kwa risasi nyumbani kwake, Area D, Dodoma huku hali yake ikizidi kuimarika kila kukicha.

Desemba 26, mbunge huyo alisimama kwa mara ya kwanza na kuanza rasmi kufanya mazoezi ya viungo katika Hospitali hiyo kwa msaada wa madaktari. Lissu anaendelea na mazoezi madogo ya kuimarisha misuli ya miguuni ili aweze kutembea.

Akielezea hali yake, Mhe. Tundu Lissu amesema kwa sasa anauwezo wa kukaa bila kuegemea kwenye kitu chochote, hali ambayo awali alikuwa anashindwa kufanya hivyo.

“Ninawashukuru kwa sala na maombi yenu. Sasa ninaweza kukaa bila ya kuegemea kitu.“ameandika Mhe. Lissu kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Mwanasheria mkuu huyo wa Chadema, ambaye alishambuliwa kwa risasi akiwa ndani ya gari mara baada ya kufika nje ya makazi yake mjini Dodoma Septemba 7, hivi karibuni alisema bado ana risasi moja mwilini mwake ambayo haijatolewa.

Viewing all 45270 articles
Browse latest View live




Latest Images